Mwanamke Aliyesilimu Lazima Awe Na Walii? Ameoa Bila Ya Kuwajulisha Wazazi Wa Mke

SWALI  

 

Assalam Alaykum? I would like to ask the following questions:- a) I have married a converted girl, before wedding she pronounced the shahada and she didn’t want her family to know either being a Muslim or getting married I was told that my marriage is not accepted because non of her family knows although she selected someone to be her Wali, from what I know is that walii cannot be a Christian and a single girl can not be married except from his decision, but I was told the family must know, if so do I have to remarry or I will be in the section of Quran where it says:(ILLA MA QAD SALAF) EXEPT FOR WHAT HAS HAPPENED BEFFORE)?

 

 


 

 

 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako hilo kuhusu ndoa. Tufahamu kuwa ndoa ya Kiislamu kukubalika kisheria inafaa itimize masharti yafuatayo:

 

1.    Kukubali kwa msichana anayeolewa.

2.    Bwana harusi kukubali kwa ndoa hiyo.

3.    Bibi harusi kupewa mahari yake.

4.    Kuwepo kwa mashahidi wawili waadilifu.

5.    Kuwepo na kupatikana idhini ya walii.

 

Kwa hiyo, Mkristo hawezi kuwa ni walii wa msichana aliye Muislamu. Sheria imeweka mipangilio madhubuti kuhusu binti kama huyo. Walii katika nikaha ya msichana aliyesilimu anakuwa ni Qadhi au Shaykh mcha Mungu au Muislamu muadilifu atakayesimama mahali pa baba yake. Kwa mujibu wa sheria ndoa hiyo iliyofungwa ni sahihi kabisa haina haja ya kufungwa tena.

 

Hata hivyo, kosa lililofanyika ni kutowajulisha wazazi wake. Hakika ni kuwa wazazi huwa na uchungu na watoto ambao wameuchukua kumlea mtoto wao mpaka akafika maksada ya kuolewa. Si ubinadamu, si Uislamu wala si utu kwa wewe kufanya hivyo. Je, wazazi wakijua kuwa binti yao ameolewa na Muislamu naye amekuwa Muislamu, mkeo huyo atarudi katika Ukristo.

 

Ni busara kwako kwenda kwa wazazi wa mke wako na kuwaeleza. Na msichana ikiwa ameingia Uislamu kwa sababu ya uzuri wake (yaani Uislamu) hataweza kushawishika lakini kama ameingia katika Uislamu kwa ajili yako huenda ukapata matatizo yatakayotoka kutoka wazazi wake. Hivyo jaribu utumie busara ili usalimishe ndoa yako.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share