06-Hadiyth Al-Qudsiy: Mmoja Katika Waja Wangu Ameniamini Na Mwengine Amenikufuru

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 6

 Mmoja Katika Waja Wangu Ameniamini Na Mwengine Amenikufuru

 

عَنْ زَيْدِ بْنِ خَالِدٍ الْجُهَنِيِّ قَالَ صَلَّى لَنَا رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ صَلَاةَ الصُّبْحِ بِالْحُدَيْبِيَةِ عَلَى أَثَرِ سَمَاءٍ كَانَتْ مِنْ اللَّيْلِ فَلَمَّا انْصَرَفَ أَقْبَلَ عَلَى النَّاسِ قَالَ: ((هَلْ تَدْرُونَ مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ؟)) قَالُوا اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ قَالَ :((أَصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي وكَافِرٌ,  فَأَمَّا مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِفَضْلِ اللَّهِ وَبِرَحْمَتِهِ فَذَلِكَ مُؤْمِنٌ بِي كَافِرٌ بِالْكَوْكَبِ وَأَمَّا مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِنَوْءِ كَذَا وَكَذَا فَذَلِكَ كَافِرٌ بِي مُؤْمِنٌ بِالْكَوْكَبِ)) البخاري والنسائي

Kutoka kwa Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu)  ambaye amesema:  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  alituswalisha Swalaah ya Alfajiri (huko) Al-Hudaybiyah baada ya kunyesha mvua usiku. Alipomaliza aliwaelekea watu akasema: ((Je, mnajua Rabb wetu Amesema nini?)) Watu wakasema Allaah na Rasuli Wake ni Wajuzi zaidi. Akasema: ((Mmoja katika waja Wangu ameamka asubuhi akiwa ameniamini na mwengine amenikufuru. Ama aliyesema: tumepewa mvua kwa fadhila za Allaah na Rahmah Zake, huyo ameniamini na amezikanusha nyota; ama aliyesema: tumepewa mvua kwa nyota kadhaa wa kadhaa huyu amenikufuru na ameamini nyota)). [Al-Bukhaariy na An-Nasaaiy]

 

 

 

Share