019-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kuchanganya Kwake (صلى الله عليه وآله وسلم) Baina Ya Surah Zinazofanana Na Nyinginezo Katika Rakaa

 

KUCHANGANYA KWAKE (صلى الله عليه وآله وسلم) BAINA YA SURAH ZINAZOFANANA NA NYINGINEZO KATIKA RAKAA

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akiunganisha baina ya An-Nadhwaair([1])  miongoni mwa Surah za Mufasswal([2]), hivyo basi alikuwa akisoma jozi mojawapo za Surah zifuatazo katika Rakaa moja([3]):

 

Ar-Rahmaan (55: 78) ([4]) na An-Najm (53: 62).

Al-Qamar (54: 55) na Al-Haaqqah (69: 52).

At-Twuur (52: 49) na Adh-Dhaariyaat (51: 60).

Al-Waaqi'ah (56: 96) na Al-Qalam (68: 52).

Al-Ma'arij (70:44) na An-Naazi'aat (79:46).

Al-Mutwaffifiyn (83: 36) na 'Abasa (80: 42).

Al-Muddaththir (74: 56) na Al-Muzzammil (73: 20).

Ad-Dahr (76: 31) na Al-Qiyaamah (75: 40).

An-Nabaa (78: 40) na Al-Mursalaat (77: 50).

Ad-Dukhaan (44: 59) na At-Takwiyr (81: 29).

 

Mara nyingine alikuwa akiunganisha baina ya Surah kutoka Sab'at-Twiwaal (Surah Saba ndefu); kama al-Baqarah, an-Nisaa na aal-'Imraan katika Rakaa moja kwenye Swalah ya usiku kama itakavyokuja. Na alikuwa akisema:

((Swalah bora kabisa ni yenye kisimamo kirefu)).([5])

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) anaposoma:

 

((أَلَيْسَ ذَلِكَ بِقَادِرٍ عَلَى أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَى))

 

Alaysa dhaalika biqaadirin ‘alaa-an Yuhyiyal Mawtaa

 

((Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu)). [Al-Qiyaamah 75: 40)

 

Husema:

 

Sub-haanak fabalaa

Utukufu ni Wako Ndio hapana shaka

 

Na anaposoma:

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى

 

Sabb-hisma Rabbikal A’laa

((Litakase Jina la Mola wako Mlezi Aliye juu kabisa)). [Al-A'laa 87: 1)

 

Husema:

Sub-haana Rabbiyal A’laa

Ametakasika Mola wangu Aliye juu([6]).

 

 

 

 





[1] "An-Nadhwaair": Ni Surah zilizofanana katika maana. Ni kama zile ambazo zote zina nasaha, maamrisho au visa.

[2] Mufasswal, hizi zimekubalika kuwa zinazomalizia Qur-aan mwisho, na mwanzo wake ni Surat Qaaf (Namba 50) kwa rai iliyo sahihi zaidi.

[3] Al-Bukhaary na Muslim.

[4] Namba ya mwanzo inamaanisha Surah, na ya pili ni idadi ya Aayah za hiyo Surah. Na namba zenye kumaanisha Surah, zimetuwekea wazi kuwa  hakuwa

(صلى الله عليه وآله وسلم) akifuata katika kuunganisha baina ya Surah nyingi za An-Nadhwaair utaratibu wa Surah ulivyo katika Msahafu. Hivyo inaonyesha kuwa ni jambo lenye kuruhusiwa. Hali kama hiyo itaonekana katika Swalah ya Usiku, japokuwa ni bora zaidi kufuata mpangilio wa Qur-aan.

[5] Muslim na Atw-Twahaawiy.

[6]  Abu Daawuud na al-Bayhaqiy kwa isnaad Swahiyh. Hadiyth hii ni ya kawaida, hivyo inajumuisha kisomo kwenye Swalah na nje ya Swalah, au Swalah hiyo iwe ni ya Sunnah au ya Faradhi.  Ibn Abi Shaybah (2/132/2) amesimulia kutoka kwa Abu Muusa Al-Ash'ariyy na Al-Mughiyrah kwamba wao wawili walikuwa wakisema hivyo katika Swalah ya Faradhi. Na ameipokea kutoka kwa 'Umar na 'Aliy bila ya maelezo hayo.      

 

Share