Skip navigation.
Home kabah

Chemsha Bongo Ya Ramadhaan 1

Asalam alecum ndugu zangu wa

Asalam alecum ndugu zangu wa imani..nashukuru sana kwa hii website mliyo tuandalia...iko na faida mingi na muongozo bora katika maisha na mfumo wa mwanadamu....Nashukuru sana..Na MOLLA awape akili zaidi ya kutupa mazuri kwa wingi,,amiin

Asalam alekum warahmatulahi

Asalam alekum warahmatulahi wabarakatuh..Ndugu zangu wa imani,naomba kama mna weza kunitumia chemsha bongo kwa email yangu,yani mimi huingia mara kwa mara kwa paltalk,tuko na room kwa luga ya kiswahili,tunakutana hapo na kubadilishana ma wazo.Na tuna peana au kufaidishana na maswali kuhusu dini,so nafurahi kuona mumetuandikia kwa alhidaya,so mimi nikiwa naongea kwa kutumia mic nawasomea yale mlio tuandalia mfano moja wapo kama chemsha bongo.Na pia nawaashia mawaida za ma Sheikh aina mbalimbali..Lakini naomba mnitumie chemshabongo kwa wingi ili niwapime akili zao pamoja na mimi,yani tufaidike sote kwa huu mwezi MTUKUFU,Amiin.Na pia tumefaidike sana kwa namna mlivyo tuandalia namna ya vipimo ya vyakula aina mbalimbali...WAABILAHI TAWFIK

Asalaam Aleykum Nashukuru

Asalaam Aleykum

Nashukuru saana kwa ninyi ndugu zetu kutupatia chemsha Bongo hii hususani ndani ya mwezi huu wa Ramadhaani... ila Tunaomba pia kama inawezekana mtu anapojibu basi apewe majibu yote aliyopata na aliyokosa na masahihsho yake. Utaratibu huu nimeuona kwenye Islamic Quiz ya ******* na naona unafaa sana hususani kwa Lugha yetu ya Kiswahili.

Allah awajaalie Kila Kheri katika hili na mengineyo Insha'allah

Assalaam alaykum. Ningependa

Assalaam alaykum.
Ningependa niwekewe majibu ambayo nimekosea ili nipate uhakika wa masuala hayo inshallah.

Alhidaaya.com Alhidaaya.com T

Alhidaaya.com

Alhidaaya.com

Tunashukuru kwa ombi lako. Hakika ilikuwa tufanye hivyo mapema ila kutokana na wingi wa hizi kazi na uchache wa watendaji tumeshindwa kutekeleza jambo hili mapema. Hivi sasa tumeshaweka majibu chini yake kuna kiungo kifuatacho:

BONYEZA UPATE MAJIBU YA CHEMSHA BONGO

Tunazidi kuomba du’aa zenu Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kwa wepesi kuwatayarishia manufaa mengi na Atutaqabalie hizi juhudi.

Ndugu Zako

AL HIDAAYA