07-Matendo Mema Na Athari Yake Katika Utajiri Na Ukunjufu Wa Rizki: Madhara Ya Chumo La Haramu

 

MADHARA YA CHUMO LA HARAMU

 

(1). MOJA YA SABABU YA KUINGIA MOTONI

 

 

“Enyi mlioamini, msiliane mali zenu kwa batili, isipokuwa iwe biashara kwa kuridhiana baina yenu. Wala msijiue (wala msiue wenzenu). Hakika Allaah ni mwenye kukuhurumieni. Na Atakayefanya haya kwa uadui na dhulma, basi huyo Tutamwingiza motoni, na hayo ni rahisi kwa Allaah.” An-Nisaa: 29-30

 

 

Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam) alimwambia Ka’ab bin ‘Umar: “Ewe Ka’ab bin ‘Umar,hatoingia peponi ambaye nyama yake imeota kutokana na haramu, na moto ni bora kwake.” Musnad Ahmad

 

 

 Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema, amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam)

 

 

           

 “Asione vizuri mwenye kukusanya mali isiyo halali yake (isiyo haki yake) akitoa sadaka haitokubaliwa na kinachobakia ni mzigo wa kwendea motoni.”

 

 

(2). HESABU NZITO SIKU YA QIYAAMAH

 

(3). KUTOJIBIWA DU’AA

 

(4). MARADHI YA NAFSI NA MWILI

 

 

3. KUTOHUSUDIANA

 

Kutoka kwa Abu Hurayrah amesema, amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam):

 

“Angalieni aliyekuwa chini yenu wala msitazame aliye juu yenu itawapelekea msijizidishie neema ya Allaah.”

 

 

4. KUTOSHEKA

 

Anasema  Allaah:

 

“Wala usifanye mkono wako kama (uliofungwa shingoni mwako wala usiukunjuwe ovyo ovyo, utakuwa ni mwenye kulaumiwa (ukifanya hivyo) na kufilisika (ukiukunjua ovyo ovyo). Israa: 29

 

Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam):

 

“Kuleni, kunyweni, vaeni, toeni sadaka bila israfu wala kujionyesha.” Al-Bukhaariy

 

 

6. KUWA MBALI NA UFEDHULI NA DHULMA

 

Anasema Allaah:

 

“Na saidianeni katika wema na uchaji Allaah, wala msisaidiane katika dhambi na uadui.” Al-Maaidah: 2

 

Neema ya Allaah inapasa kushukuru na katika kushukuru ni kutodhulumu,na kudharau watu, kutoa katika kumtii Allaah na kujisaidia katika njia za kheri sio za dhulma na shari.

 

Anasema Allaah:

 

“Basi Hatukumtuma (Hatukumpeleka) muonyaji katika mji wowote ule ila wenyeji wake wajipatao wakisema “bila shaka sisi tunakataa haya mliyotumwa nao”

Na wakasema “sisi tunayo mali nyingi na watoto wengi wala sisi hatutaadhibiwa.” Sabaa: 34

 

Yaani walijifakharisha kwa wingi wa mali na watoto wakadhani hiyo ni dalili ya kupendwa na Allaah na Anawajali.

 

Anasema Allaah:

 

“Hakika wale waliokufuru hutoa mali zao ili (kuzuilia watu) wasipate kuamini njia ya Allaah basi watazitoa, kisha zitakuwa majuto juu yao kama kisha watashindwa. Na wale waliodumu katika ukafiri watakusanywa katika jahannam (watakaosilimu baadaye Allaah Atawasamehe.)” Al-Anfaal: 36 

 

Anasema Allaah:

 

“Na Tunapomneemesha mwanaadamu, hugeuka na kujitenga upande, (hana haja ya kutuabudu) inapomgusa shari, mara hugeuka akawa na madu’aa marefu marefu.”

Fusswilat: 51

 

Anaonya Allaah katika hizi aya na zinginezo kwa mwenye kutumia neema ya Allaah na mali katika kuwadhulumu watu, na kufanya ufisadi katika ardhi na kiburi kwamba watapata hasira ghadhabu, na adhabu ya Allaah.

 

 Na Qur-aan Tukufu na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam) wanatuonyesha yaliyowapata umma zilizopita kama ‘Aad, Thamuud na yaliyowapata waovu kama Fir’awn, Abu Jahal, Qaaruun na wengineo, walipata maangamivu ili iwe ni mazingatio kwa watakaokuja baada yao, na huu ni mwendo wa Allaah katika adhabu kwa wanaokanusha na makafiri mpaka siku ya Qiyaamah.

 

 

WabiLlaahi At-Tawfiyq

 

 

Share