018-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Kutaka Talaka Bila Ya Kuwepo Tatizo Ni Jambo Lililoharamishwa Kishari’ah

KUTAKA TALAKA BILA YA KUWEPO TATIZO NI JAMBO LILILOHARAMISHWA KISHARI’AH

Mara nyingi mwanamke anataka talaka kwa mume wake pindi wanandoa wawili wanapomwachia Shaytwaan nafasi na pindi ghadhabu ya mwanamke inaposhtadi, lau angesubiri kidogo na kuzuia ghadhabu zake na kupata utulivu angeona kuwa hakukuwa na sababu ya hilo, talaka si jambo la mzaha wakalichezea wanandoa, akawa mmoja wao akighadhibika anamtishia mwenzake kwa talaka na mwengine akisema anapoghadhibika, ‘Nitaliki’.

 

Wanandoa wanatakiwa kuwa ni werevu kuliko matatizo yanayowakabili, wakishirikiana katika kutatua matatizo na wakifahamiana vizuri kwa hilo, na kila mmoja anajaribu kushusha mahitaji yake na kuachana na misimamo yake ili jahazi lisije likazama. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam.) amemtahadharisha mke asidai talaka kama hamna tatizo la msingi kwa kusema,

“Mwanamke yeyote atakaye talaka kutoka kwa mume wake bila ya tatizo la msingi basi ni haramu kwake kunusa harufu ya pepo”[1]

 

Hata hivyo kungekuwa na jambo lingine linalopelekea jambo hili kwa mfano mume kuwa na tabia mbaya kiasi cha kuwa mke wake hawezi kuvumilia, au ni mtu fasiki asiyetekeleza haki za mke wake na watoto wake, au mfano wa hayo katika mambo yanayofahamika kisheria na desturi.

 

Mke anaweza kudai talaka ikiwa njia zote za kufanya suluhu baina yao ndani ya nyumba na hata nje zimeshindikana ambazo katika utatuzi wenyewe na suluhu yenyewe hushiriki hakimu kutoka upande wa mume na hakimu kutoka upande wa mke kushindikana.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema,

Na mkichelea kuwepo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Mwenyezi Mungu Atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye khabari.(4:35)

 

 

 





[1] Imepokewa na Ahmad na At-Tirmidhiy na wengineo

 

Share