Wali Wa Mboga Mchanganyiko Kwa Mayai Ya Kuchemsha

Wali Wa Mboga Mchanganyiko Kwa Mayai Ya Kuchemsha

 

Vipimo

Mchele (Basmati) - 3 vikombe

Mbogamboga za barafu

(karot, njegere, spring beans na mahindi) - 1 kikombe

Kuku  Kidari - 1 LB (ratili)

Mayai - 2 mayai

Vitunguu (vikubwa) - 2 au 3 vidogo       

Pili pili manga - 1 kijiko cha chai

Paprika - 1 kijiko cha chai

Chumvi - Kiasi

Mafuta - 1/3 kikombe cha chai

Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 kijiko cha supu

Tangawizi - 1 kijiko cha chai    

Kidonge cha supu - 1

Soy sauce - 2 vijiko vya supu                                                            

 

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

  1. Kata kidari cha kuku vipande vidogo vidogo vya kiasi. 
  2. Tia mafuta kidogo katika wok (aina ya karai)
  3. Kisha mtie kuku, thomu, tangawizi, soy sauce, pilipilimanga, paprika  chumvi.
  4. Tia mboga za barafu, kidonge cha supu, kaanga  kuku na mboga viwive yitu vyote na mchanganyiko ukauke.  

 

Namna Ya Kutayarisha Na kupika Wali

  1. Roweka mchele wa basmati kwa muda wa saa au zaidi.
  2. Halafu chemsha mchele pamoja na chumvi
  3. Wacha uchemke asilimia 70%
  4. Chuja maji na weka kando
  5. Katika sufuria, tia mafuta kidogo tu
  6. Kisha tia mayai mawili ukaange haraka haraka (crumbled egg)
  7. Changanya mchanganyiko wa kuku na mboga
  8. Kisha tia wali changanye vizuri
  9. Rudisha katika moto, funika upikike kidogo hadi uive
  10. Kisha pakua katika sahani  na tolea na mayai ya kuchemsha ukipenda.

 

Share