09-Wasiya Wa Mwisho Wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Ni Sunnah Moja Au Mbili?

 

Ni Sunnah Moja (Njia) Au Mbili?

 

Ni Sunnah moja, kwani Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: “Na ing’ateni (yaani Sunnah) kwa magego yenu.” Imekusudiwa kwa “umoja’ (singular). Yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakusema “Yang’ateni (yaumeni), kwa kutumia “uwingi”; bali alisema, “hicho” (i) –inayoashiria “umoja’ kuthibitisha kuwa ni Sunnah moja. Kufuata Sunnah ya Makhalifah waogofu ina maana kufuata Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa sababu Sunnah yao haikuwa nyingine ila Sunnah ya Mtume.

 

Kwani “Ing’ate au Iume” ni tamathali ya usemi, ambayo inaelezea kushikamana kwa dhati na Sunnah, aidha ndio njia sahihi ya kufuatwa. Njia pekee ya kufikia ufanifu ni kufuata njia ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na njia ya Makhalifah waongofu, hasa tukizingatia njia nyingi zilizozuka na zinafuatwa na watu wanaoongozwa na utashi wa kiu yao.

 

Mtu lazima ajitahidi sana ili kushikamana na Sunnah – kwa kuchelea kupotea kwake – kuliko Mwarabu wa Jangwani anayetafuta chakula chake na maji yake, kwa sahabu huyu wa pili anaupatia uhai wa mwili wake, ambapo yule wa mwanzo anaupatia uhai moyo wake.

 

“Na tahadharini na mjiepushe na mambo yaliyozuliwa.” (Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakukoma kutuamuru tufuate Sunnah zake na Sunnah za Makhalifah waongofu, badala yake Yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitukataza mambo yaliyozuliwa. Watu wanaweza wasitambue kuwa kuleta uzushi katika maisha, ni kuwa wanaondoa Sunnah; kila uzushi unasababisha Sunnah kufa (Na tunaomba hifadhi ya Allaah!)

 

Neno ‘bid’ah’ lina maana ya kitu kipya na hakijawahi kutokea kabla yake, na watu wanaridhia vyote vilivyo vipya. Ama kupata ridhaa ya Dini, ni kwa kufuata vya zamani, maana iliyoelezwa kwa maneno yafuatayo ya Ibn Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu).

“Fuata na usizue, kwani mliyopewa yanatosha: kwenu nyie kufuata mambo yaliyoanzishwa zamani.”

 

Hadiyth sahihi iliyosimuliwa kutoka kwa Ibn Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu) – katika masimulizi yanayoweza kuhusishwa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

 

“Utakuaje wakati utakapogubikwa na mtihani (kupitia kwayo) wakubwa (wazee) watafikia ukongwe na vijana watakua. Watu watachukulia ya kuwa ni Sunnah, na sehemu yoyote ikiachwa, itasemwa, “Je Sunnah imeachwa?” Watauliza, “Na ni lini?” Alisema, “Wanachuoni wenu wakiondoka; wasomaji wenu watakapoongezeka, Fuqahaa watakapokuwa wachache, watawala watakapoongezeka; waaminifu watakapokuwa wachache; dunia itakapotafuta kupitia vitendo vya Siku ya Qiyaamah; na wakati maarifa ya Dini yatakapotafutwa lakini si kwa ajili ya Dini.”[1]

 

Allaah Amuwie radhi Hudhayfah (Radhiya Allaahu ‘anhu), mtunza siri za Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Yeye (Radhiya Allaahu ‘anhu) alisema: “Msifanye ibada yoyote ambayo haikufanywa na Maswahaba wa Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).”

 

Na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) amrehemu Tab’i maarufu, Hassan bin ‘Atwiyyah Al-Maharibi, ambaye alisema, “Pindi watu watakapoanzisha bida’h katika Dini yao, Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Ataondosha Sunnah yao iliyokuwa sawa nayo; na hatawarudishia (yaani Sunnah) mpaka Siku ya Malipo.”[2]





[1] Imesimuliwa na Ad-Daarimiy (1/64) kwa silsilah mbili, moja ambayo ni Swahiyh na nyingine ni hasan; cha al-Haakim (4/514), na kwa wengineo, kama ilivyoelezwa na Shaykh wetu, Al-Albaaniy (Allaah amrehemu) katika Qiyaamu Ramadhaan.

[2] Ilisimuliwa na Ad-Daarimiy yenye Silsilah Swahiyh, kama Shaykh wetu Al-Albaaniy (Allaah Amrehemu), alisema kwenye Al-Mishkaat (188). Na alisema, “Ilisimuliwa pia kutokana na Hadiythi ya Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambayo ilisimuliwa na Abu Al-‘Abbaas Al-Asm katika Hadiyth yake.”

 

Share