58-Mukhtasari Aqiydah Ya Muislamu: Wepi ni Maswahaba bora kabisa?

Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

58-Wepi ni Maswahaba bora kabisa?

 

Maswahaba bora kabisa ni Makhulafaa Ar-Raashiduwn nao ni: Abuu Bakr, kisha ‘Umar, kisha ‘Uthmaan, kisha ‘Aliy (Radhwiya Allaahu ‘anhum)

 

إِلَّا تَنصُرُوهُ فَقَدْ نَصَرَهُ اللَّـهُ إِذْ أَخْرَجَهُ الَّذِينَ كَفَرُوا ثَانِيَ اثْنَيْنِ إِذْ هُمَا فِي الْغَارِ إِذْ يَقُولُ لِصَاحِبِهِ لَا تَحْزَنْ إِنَّ اللَّـهَ مَعَنَا ۖ

Msipomnusuru (Rasuli), basi Allaah Amekwishamnusuru, pale walipomtoa (Makkah) wale waliokufuru akiwa wa pili katika wawili; walipokuwa katika pango, alipomwambia swahibu yake: ““Usihuzunike, hakika Allaah Yu Pamoja nasi.”[At-Tawbah: 40]

 

((فَعَلَيْكُمْ بِسُنَّتِي وَسُنَّةِ الْخُلَفَاءِ الْمَهْدِيِّينَ الرَّاشِدِينَ، تَمَسَّكُوا بِهَا وَعَضُّوا عَلَيْهَا بِالنَّوَاجِذِ)) رواه أبو داوود والترمذي وقال حديث حسن صحيح

((Kwa hiyo, shikamaneni na mwenendo wangu na mwenendo wa Makhalifa waongofu, yashikilieni na yakamateni barabara kwa magego)) [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Share