227-Aayah Na Mafunzo: Haramisho La Mwanamke Kuomba Talaka Bila Sababu

Aayah Na Mafunzo

Al-Baqarah

Haramisho La Mwanamke Kuomba Talaka Bila Sababu

 

 

 

وَإِنْ عَزَمُوا الطَّلَاقَ فَإِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ﴿٢٢٧﴾

227. Na wakiazimia talaka, basi hakika Allaah ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote.

 

Mafunzo:

 

Mwanamke haifai kuomba talaka bila ya sababu:  

 

عَنْ ثَوْبَان مَوْلَى رَسُول اللَّه – صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ – عَنْ النَّبِيّ – صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ – أَنَّهُ قَالَ :((أَيّمَا اِمْرَأَة سَأَلَتْ زَوْجهَا الطَّلَاق فِي غَيْر مَا بَأْس حَرَّمَ اللَّه عَلَيْهَا رَائِحَة الْجَنَّة))  الترمذي و قال حديث حسن

Kutoka kwa Thawbaan amesema kwamba: Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwanamke yeyote anayemuomba mumewe talaka bila ya sababu yoyote, Allaah Amemharimishia harufu ya Pepo” [At-Tirmidhiy na kasema Hadiyth Hasan]

 

Na riwaayah nyengine amesema:

 

“Mwanamke yeyote mwenye kumuomba mumewe talaka pasi na kosa lolote basi Jannah itakuwa haram kwake wala hatosikia harufu yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim, Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah].

 

 

 

 

Share