15-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Swalaah: Mlango Wa Swalaatul-Kusuwf (Swalaah Ya Kupatwa Jua Au Mwezi)

 بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلصَّلَاةِ

Kitabu Cha Swalaah

 

بَابُ صَلَاةِ اَلْكُسُوفِ

15-Mlango Wa Swalaatul-Kusuwf [1] (Swalaah Ya Kupatwa Jua Au Mwezi)

 

 

 

401.

 عَنِ اَلْمُغِيرَةِ بْنِ شُعْبَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ  قَالَ: {اِنْكَسَفَتِ اَلشَّمْسُ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم   يَوْمَ مَاتَ إِبْرَاهِيمُ، فَقَالَ اَلنَّاسُ: اِنْكَسَفَتِ اَلشَّمْسُ لِمَوْتِ إِبْرَاهِيمَ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم   "إِنَّ اَلشَّمْسَ وَالْقَمَرَ آيَتَانِ مِنْ آيَاتِ اَللَّهِ لَا يَنْكَسِفَانِ لِمَوْتِ أَحَدٍ وَلَا لِحَيَاتِهِ، فَإِذَا رَأَيْتُمُوهُمَا، فَادْعُوا اَللَّهَ وَصَلُّوا، حَتَّى تَنْكَشِفَ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ 

وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ: «حَتَّى تَنْجَلِيَ»

وَلِلْبُخَارِيِّ مِنْ حَدِيثِ أَبِي بَكْرَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ  {فَصَلُّوا وَادْعُوا حَتَّى يُكْشَفَ مَا بِكُمْ}

Kutoka kwa Al-Mughiyrah bin Shu’bah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Jua lilipatwa wakati wa uhai wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), siku alipofariki (mwanae) Ibraahiym,[2] watu wakasema: Jua limepatwa kwa sababu ya kifo cha Ibraahiym. Akasema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): Jua na mwezi ni Aayaat (ishara) mbili kati ya Aayaat za Allaah. Havipatwi kwa sababu ya kufa yeyote wala kwa uhai wake.[3] Kwa hivyo munapoona kupatwa kwake, muombeni Allaah na mswali hadi kupatwa huko kuondoke.”[4] [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Na katika Riwaayah ya Al-Bukhaariy: “Mpaka pawe paangavu.”

 

 

Na katika upokezi wa Al-Bukhaariy kutoka kwa Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ): “Swalini na ombeni hadi kuondoke kilichokufikeni.”

 

 

 

402.

وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا: {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم  جَهَرَ فِي صَلَاةِ اَلْكُسُوفِ  بِقِرَاءَتِهِ، فَصَلَّى أَرْبَعَ رَكَعَاتٍ فِي رَكْعَتَيْنِ، وَأَرْبَعَ سَجَدَاتٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَهَذَا لَفْظُ مُسْلِمٍ 

وَفِي رِوَايَةٍ لَهُ: {فَبَعَثَ مُنَادِيًا يُنَادِي: اَلصَّلَاةُ جَامِعَةٌ}

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisoma kwa sauti[5] kisomo chake cha Swalaatul-Kusuwf (Swalaah ya kupatwa jua au mwezi), akaswali Rakaa mbili ambamo alirukuu mara nne[6] na alisujudu mara nne.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]

 

Na katika mapokezi mengine: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akatuma mtu akaenda kutangaza: “Njooni kwenye Swalaah ya Jamaa.”[7]

 

 

 

403.

وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {اِنْخَسَفَتِ الشَّمْسُ عَلَى عَهْدِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم   فَصَلَّى، فَقَامَ قِيَامًا طَوِيلًا، نَحْوًا مِنْ قِرَاءَةِ سُورَةِ اَلْبَقَرَةِ، ثُمَّ رَكَعَ رُكُوعًا طَوِيلًا، ثُمَّ رَفَعَ فَقَامَ قِيَامًا طَوِيلًا وَهُوَ دُونَ اَلْقِيَامِ اَلْأَوَّلِ، ثُمَّ رَكَعَ رُكُوعًا طَوِيلًا، وَهُوَ دُونَ اَلرُّكُوعِ اَلْأَوَّلِ، ثُمَّ سَجَدَ، ثُمَّ قَامَ قِيَامًا طَوِيلاً، وَهُوَ دُونَ اَلْقِيَامِ اَلْأَوَّلِ، ثُمَّ رَكَعَ رُكُوعًا طَوِيلًا، وَهُوَ دُونَ اَلرُّكُوعِ اَلْأَوَّلِ، ثُمَّ رَفَعَ، فَقَامَ قِيَامًا طَوِيلًا، وَهُوَ دُونَ اَلْقِيَامِ اَلْأَوَّلِ، ثُمَّ رَكَعَ رُكُوعًا طَوِيلاً، وَهُوَ دُونَ اَلرُّكُوعِ اَلْأَوَّلِ، ثُمَّ سَجَدَ، ثُمَّ انْصَرَفَ وَقَدْ تَجَلَّتِ اَلشَّمْسُ. فَخَطَبَ اَلنَّاسَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ 

وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ: {صَلَّى حِينَ كَسَفَتِ اَلشَّمْسُ ثَمَانَ رَكَعَاتٍ فِي أَرْبَعِ سَجَدَاتٍ}

وَعَنْ عَلِيٍّ مِثْلُ ذَلِكَ 

وَلَهُ: عَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ {صَلَّى سِتَّ رَكَعَاتٍ بِأَرْبَعِ سَجَدَاتٍ}  

وَلِأَبِي دَاوُدَ: عَنْ أُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ: {صَلَّى، فَرَكَعَ خَمْسَ رَكَعَاتٍ وَسَجَدَ سَجْدَتَيْنِ، وَفَعَلَ فِي اَلثَّانِيَةِ مِثْلَ ذَلِكَ} 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Jua lilipatwa wakati wa uhai wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), akaswali na akasimama kisomo kirefu, kadiri ya kuweza kusoma Suwratul-Baqarah, kisha akarukuu Rukuu ndefu, akainua kichwa na kusimama kisimamo kirefu, chini ya kisimamo cha kwanza, kisha akarukuu Rukuu ndefu chini ya Rukuu ya kwanza, akasujudu na akasimama kisimamo kirefu chini ya kisimamo cha kwanza, kisha akarukuu Rukuu ndefu chini ya Rukuu ya kwanza, kisha akainua kichwa, kisha akasujudu, kisha akaondoka, na jua lilishafunguka. Akatoa Khutbah.”[8] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]

 

 

Na katika Riwaayah ya Muslim: “Jua lilipopatwa, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliswali Rakaa nane katika Sijdah nne.” Na ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alisimulia Hadiyth nyingine kama hiyo.

Yeye (Muslim) tena amemnukuu Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kuwa: “(Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)) aliswali kwa Rakaa sita na Sijdah nne.”

 

 

Na Abuu Daawuwd amepokea masimulizi ya Ubayy bin Ka’b (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kuwa: “(Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)) aliswali na akarukuu mara tano na akasujudu mara mbili, na katika Rakaa ya pili alifanya hivyo hivyo.”

 

 

 

404.

وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {مَا هَبَّتْ رِيحٌ قَطُّ إِلَّا جَثَا اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم   عَلَى رُكْبَتَيْهِ، وَقَالَ: "اَللَّهُمَّ اجْعَلْهَا رَحْمَةً، وَلَا تَجْعَلَهَا عَذَابًا"} رَوَاهُ اَلشَّافِعِيُّ وَالطَّبَرَانِيُّ 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Upepo haukuvuma kamwe, isipokuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipiga magoti na kusema: Ee Allaah! Ujaalie uwe Rahmah wala Usiujaalie uwe adhabu.” [Imetolewa na Ash-Shaafi’iyy na Atw-Twabaraaniyy]

 

 

 

405.

وَعَنْهُ: أَنَّهُ صَلَّى فِي زَلْزَلَةٍ سِتَّ رَكَعَاتٍ، وَأَرْبَعَ سَجَدَاتٍ، وَقَالَ: هَكَذَا صَلَاةُ اَلْآيَاتِ  رَوَاهُ اَلْبَيْهَقِيُّ 

وَذَكَرَ اَلشَّافِعِيُّ عَنْ عَلِيٍّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ  مِثْلَهُ دُونَ آخِرِهِ 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema tena: “(Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)) aliswali pindi ilipotokea tetemeko la ardhi Rakaa sita na Sijdah nne, na akasema: Hivi ndivyo namna ya kuswali Swalaatul-Aayaat (Swalaah ya ishara  (ya Maafa).”[9] [Imetolewa na Al-Bayhaqiyy]

 

Na Ash-Shaafi’iyy ametaja Hadiyth ya ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kama hiyo pasi na kutaja mwisho wake.

 


[1] Maana ya neno hilo ‘Kusuwf’ na ‘Khusuwf’ (kushikwa kwa jua na kushikwa kwa mwezi) ni “kubadilika”. Maneno haya yaweza kuwa kinyume cha hivi.

 

[2] Mama yake Ibraahiym alikuwa Maria, Mmisri aliyewahi kuwa mtumwa ambaye Al-Muqawqis mtwawala wa Alexandria na Misri alimpa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kama zawadi amuoe. Ibraahiym alizaliwa mnamo mwezi wa Jumaadal-Uwlaa mwaka wa 9A.H., na akafariki mnamo tarehe 29 Shawwaal mwaka 11 A.H. akiwa na umri wa miezi kumi na nane. Alizikwa Al-Baqi’, na yeye (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema kuwa: “Anaye wa kumkamilishia kunyonya kwake huko Jannah.”

 

[3] Siku za Jaahiliyya (kipindi kabla ya ujio wa Uislamu), watu walikuwa wakiamini kuwa kila mtu mashuhuri anapozaliwa au anapokufa, jua au mwezi hupatwa. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikanusha itikadi hii.

 

[4] Al-Bukhaariy na Muslim.

 

[5] Hoja ya kama Swalaatul-Kusuwf (Swalaah ya kupatwa kwa jua au mwezi) bora iswaliwe kwa sauti kubwa au sauti ndogo, nayo imetofautiana. Lakini kuswali kwa sauti kubwa ndiko kumethibitishwa kwa Hadiyth Marfuw’.

 

[6] Kinyume na Swalaah zingine, Swalaah hii ina kurukuu mara mbili kila Rakaa.

 

[7] Kwa mujibu wa Hadiyth Swahiyh kutangaza au kuita watu kwa ajili ya Swalaah yoyote hairuhusiwi isipokuwa Swalaatul-Kusuwf (Swalaah ya kupatwa kwa jua au mwezi).

 

[8] Inaeleweka kutokana na Hadiyth kuwa Khutbah hutolewa pia katika Swalaatul-Kusuwf (Swalaah ya kupatwa jua au mwezi).

 

[9] Hadiyth hii inatufunza kuwa, kukizuka balaa, liwe ni janga la ardhini kama tetemeko la ardhi, au kuporomoka kwa milima ya theluji na barafu, n.k; au maangamizi ya kutoka angani tufani, kimbunga cha mchanga, au kimbunga cha theluji, vinavyoathiri viumbe kwa maumivu na huzuni, watu sharti wajitume wenyewe kuswali Swalaah hii inayoitwa Swalaatul-Aayaat (Swalaah ya ishara za Allaah (عزّ وجلّ).

 

Share