01-Imaam Ibn Baaz: Hijjah Ya Muislamu Asiyeswali

 

 

 

Hijjah Ya Muislamu Asiyeswali

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nini hukmu ya mwenye kufanya Hajj lakini hakuwa akiswali aidha kwa makusudi (akiwa anaamini kuwa haikuwa ni wajib kwake kuswali) au kwa kudharau? Je, Hajj yake inakubaliwa?

 

JIBU:

 

Yeyote mwenye kufanya Hajj ambaye hakuwa akiswali, kwa sababu akiamini kuwa sio fardhi kwake, basi amekufuru kutokana na rai waliokubaliana ‘Ulamaa, na Hajj yake haikubaliwi. Lakini ikiwa hakuwa anaswali kwa sababu ya uvivu na dharau, basi kwa hali hii, kuna rai tofauti baina ya ‘Ulamaa. Baadhi ya rai zao ni kuwa Hajj yake inafaa na pia kuna baadhi ambao rai zao ni kuwa Hajj yake haifai. Na rai iliyo sahihi kabisa ni kwamba Hajj yake haifai kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

 (( إن العهد الذي بيننا و بينهم الصلاة فمن تركها فقد كفر )) أخرجه أصحاب السنن

((Mafungamano baina yetu na wao (Makafiri) ni Swalaah, atakayeiacha amekufuru)) [Aswhaabus-Sunan]

 

Vile vile amesema:

 

  ((بين الرجل و الكافر و الشرك ترك الصلاة))   أخرجه مسلم في صحيحه

((Baina ya mtu na kafiri na shirki ni kuacha Swalaah)) [Muslim katika Swahiyh yake]

 

Hii ni kwa ujumla na inawahusu wote; mwenye kuamini kuwa Swalaah sio fardhi na asiyeswali kwa sababu ya uvivu au dharau.

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

[Fataawa Al-Hajj Wal-'Umrah waz-Ziyaarah Uk. 15]

 

Share