10-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Amefanya Twawaaful-Widaa'i Kisha Hakuweza Kuondoka Makkah Wakati Huo

 

Amefanya Twawaaful-Widaa'i Kisha Hakuweza Kuondoka Makkah Wakati Huo

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Mtu amefanya Hajj, alipomaliza kafanya twawaaful-widaa'i usiku lakini akashindwa kuondoka Makkah baada ya twawaaf, hivyo akabakia Makkah hadi asubuhi kisha akasafiri. Nini hukmu ya yake?

 

JIBU:

 

Shariy’ah inavyopasa ni kuwa twawaaful-widaa'i iwe pindi mtu anapokuwa tayari kuondoka Makkah pale pale kutokana na Hadiyth kutoka kwa Ibn 'Abbaas: "Watu waliamrishwa kuwa kitendo chao cha mwisho (kabla ya kuondoka Makkah) kiwe ni twawaaf katika Ka'abah, isipokuwa kwa wanawake wenye hedhi". [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

Hivyo ikiwa alifanya twawaaf kwa niyyah ya kuondoka usiku kisha akazuilika hadi asubuhi, basi hakuna ubaya In Shaa Allaah. Akiweza kurudia twawaaful-widaa'i kabla ya kuondoka ni bora zaidi.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 [Fataawa al-Hajj wal-'Umrah waz-Ziyaarah – Uk.84]

 

 

 

Share