19-Zawadi Kwa Wanandoa: Adabu Za Kuingiliana

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

19-Adabu Za Kuingiliana

 

أدب الجماع

 

Imepokewa vile vile kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu 'anhu)  kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  amesema:

 

   إذا جامع أحدكم أهله فليصدقها , فإذا قضى حاجته قبل أن تقضي حاجتها فلا يعجلها حتى تقضي حاجته

“Atakapomuingilia mmoja wenu mkewe na amsadikishe (yaani wote wafikie kilele cha ladha ya kitendo cha ndoa), atakapomaliza haja yake kabla ya mke wake kumaliza ya kwake basi asifanye haraka hadi mke wake nae amalize haja yake.” (Abu Ya'ala)

 

Tunajifunza katika hadithi hii mafundisho ya kisheria yenye kumtaka mume amsubiri mke wake nae amalize haja yake, amshibishe na afikie kilele kama alivyofika yeye. Mafundisho haya ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) yanatufundisha kujali hisia za mwanamke na kuziheshimu.

 

Share