31-Zawadi Kwa Wanandoa: Kuondosha Nguo Zote

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

31-Kuondosha Nguo Zote

 

التجرّد من الملاب

 

 

Ukweli ni kuwa nguo zina nafasi yake katika kuonyesha uzuri na kusisimsha, na kuonesha mandhari nzuri kwa wanandoa wawili. Vile vile kama zilivyo nguo nzuri na zaidi, uchi huonyesha uzuri, husisimsha na huvutia katika kufanya kazi ya kuamsha hisia na matamanio.

 

Kama ilivyokuwa maarufu kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  alivua nguo zake alipokuwa akioga sehemu moja na Bibi 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha) . Tunachoweza kutolea dalili hapa ni neno lake Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Surat al-Baqarah Aliposema:

 

هن لباس لكم وأنتم لباس لهن

 

“…Wao ni (kama) nguo kwenu (zilizokugandeni mwilini), na ninyi ni (kama) nguo kwao…” (Al-Baqarah: 187)

 

Nako huku kuwa uchi kabisa kunapendezesha na kuwezesha kufikia kilele za raha za kimwili azipatazo mtu, hivyo basi hufanikisha kufikia lengo lililokusudiwa la kila mmoja wa wanandoa kuwa ni nguo kwa mwenzake!

 

Share