39-Zawadi Kwa Wanandoa: Uwastani Wa Kutoa Katika Matumizi

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

39-Uwastani Wa Kutoa Katika Matumizi

 

 الاعتدال في النفق

 

 

Ni kutofanya Israafu na kutokuwa bakhili, bali kinachohitajika hapa ni suluhisho la kati kwa kati nalo ni lile Analolisema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) :

 

وكلوا واشربوا ولا تسرفوا إنه لا يحب المسرفين 

 

“ … na kuleni (vizuri) na kunyweni (vizuri). Lakini msipite kiasi tu…” (Al-A'raaf: 31)

 

Na Maneno Yake Mengine Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

ولا تجعل يدك مغلولة إلى عنقك ولا تبسطها كل البسط

 

“Wala usiufanye mkono wako kama uliofungwa shingoni mwako, wala usiukunjue ovyo ovyo (utakuwa ni mwenye kulaumiwa ukifanya hivyo)…” (Al-Israa: 29)

 

Na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) akasema:

 

دينار أنفقته في سبيل الله , ودينار أنفقته في رقبة ,  ودينار تصدّقت به على مسكين , ودينار أنفقته على أهلك , أعظمها أجرا الذي أنفقته على أهلك

 

“Dinari utakayoitoa katika njia ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), na dinari utakayoitoa katika kumkomboa mtumwa, na dinari utakayompa sadaka masikini, na dinari utakayoitoa kwa mke wako, bora ya dinari yenye malipo makubwa (katika hayo) ni ile utakayotoa kwa ajili ya mke wako.” (Muslim)

 

Na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  akasema: “Atakapotoa mtu matumizi kwa mkewe, matumizi yaliyo katika hesabu itakuwa ni sadaka yake.” (Al-Bukhaariy na Muslim)

 

Kitu muhimu kinachoangaliwa na Uislamu katika kutafuta riziki ni kuwa riziki yako ni halali na chanzo chake  ni halali ambayo haina uovu, shaka wala shubha ndani yake. Hili ni kwa hali yoyote ilivyo ya kimaisha na ugumu wake utakavyokuwa kwa kuingiliwa na mipenyo ya sheitani.

 

Hapa hatuna budi kumnong’oneza mke mnong’onezo ambao tunaufupisha katika haya: mume anaweza kupatwa na ufakiri hivyo ni juu yake awe na subira, kwani wewe ndie uliyemchagua kwa uhuru wako mwenyewe. Kisha elewa kuwa maisha ya kiuchumi ni yenye kubadilika, siku moja ipo pamoja nawe yaani maisha ya kiuchumi ni mazuri, lakini kumbuka vile vile kuwa siku nyingine maisha ya kiuchumi yanaweza kuwa magumu.

 

Ni uzuri ulioje mtu kutokufanya maisha yake kuwa makuu. Ajitahidi ayafanye mepesi yanayowezekana kuendeshwa bila matatizo yoyote na hivyi kumwezesha kuhifadhi kinachobakia. Ubadhirifu ni utazaa majuto, taabu na ubakhili. Bora ya mambo ni yale ya kati kwa kati. Tumuombe Allaah Atuondoshee kujiona, kujifakharisha na israafu. Aamiyn

 

 

Share