09-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Kapewa Majina Kadhaa Ya Kusifiwa Na Allaah

Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

09-Kapewa Majina Kadhaa Ya Kusifiwa Na Allaah

www.alhidaaya.com

 

 

عن جبير بن مطعم رضي الله عنه أن رسول اللهصلى الله عليه وسلم قال: ((إنَّ لِيْ أَسْمَاءً، أَنَا مُحَمَّدٌ، وَأَنَا أَحْمَدُ، وَأَنَا المَاحِي الَّذِي يَمْحُو الله بِيَ الكُفْرَ، وَأَنَا الحَاشِرُ الَّذِي يُحْشَرُ النَّاسُ عَلَى قَدَمَيَّ، وَأَنَا العَاقِبُ الَّذِي لَيْسَ بَعْدَهُ أَحَدٌ))

 

 وفي لفظ  ((وَنَبِيُّ التَّوبَةِ، وَنَبِيُّ الرَّحْمَةِ)) . متفق عليه.

 

Imepokelewa kutoka kwa Jubayr bin Mutw’im (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mimi nina majina kadhaa: Mimi ni Muhammad na mimi ni Ahmad, na mimi ni Al-Maahiy (mfutaji) ambaye Allaah Hufuta kufru kupitia kwangu, na mimi ni Al-Haashir (mkusanyaji) ambaye watu watakusanywa mbele ya miguu yangu (Siku ya Qiyaamah), na mimi ni Al-‘Aaqib (Wa mwisho) ambaye hakuna baada yake mtu (Nabiy))   [Muslim]

 

Na katika lafdhi nyengine:  ((Na Nabiy wa Tawbah na Nabiy wa Rahmah)) [Muslim]

 

 

 

  

Share