060-Asbaabun-Nuzuwl: Al Mumtahinah Aayah 01: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لاَ تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ أَوْلِيَاءَ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

060-Al-Mumtahinah Aayah 1

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ أَوْلِيَاءَ تُلْقُونَ إِلَيْهِم بِالْمَوَدَّةِ وَقَدْ كَفَرُوا بِمَا جَاءَكُم مِّنَ الْحَقِّ يُخْرِجُونَ الرَّسُولَ وَإِيَّاكُمْ ۙ أَن تُؤْمِنُوا بِاللَّـهِ رَبِّكُمْ إِن كُنتُمْ خَرَجْتُمْ جِهَادًا فِي سَبِيلِي وَابْتِغَاءَ مَرْضَاتِي ۚ تُسِرُّونَ إِلَيْهِم بِالْمَوَدَّةِ وَأَنَا أَعْلَمُ بِمَا أَخْفَيْتُمْ وَمَا أَعْلَنتُمْ ۚ وَمَن يَفْعَلْهُ مِنكُمْ فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ﴿١﴾

1. Enyi walioamini! Msifanye adui Wangu na adui wenu kuwa marafiki wandani mkiwapa mapenzi, na hali wamekwishakufuru yaliyokujieni ya haki; wanamfukuza Rasuli pamoja nanyi kwa sababu mmemuamini Allaah Rabb wenu; Mnapotoka kwa ajili ya jihaad katika njia Yangu na kutafuta radhi Zangu mnawapa siri kwa mapenzi, na hali Mimi Najua zaidi yale mnayoyaficha na yale mnayoyadhihirisha. Na yeyote atakayefanya hivyo miongoni mwenu, basi kwa yakini amepotea njia ya sawa.

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

حَدَّثَنَا قُتَيْبَةُ، حَدَّثَنَا سُفْيَانُ، عَنْ عَمْرِو بْنِ دِينَارٍ، قَالَ أَخْبَرَنِي الْحَسَنُ بْنُ مُحَمَّدٍ، أَنَّهُ سَمِعَ عُبَيْدَ اللَّهِ بْنَ أَبِي رَافِعٍ، يَقُولُ سَمِعْتُ عَلِيًّا ـ رضى الله عنه ـ يَقُولُ بَعَثَنِي رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنَا وَالزُّبَيْرَ وَالْمِقْدَادَ فَقَالَ ‏"‏انْطَلِقُوا حَتَّى تَأْتُوا رَوْضَةَ خَاخٍ، فَإِنَّ بِهَا ظَعِينَةً مَعَهَا كِتَابٌ، فَخُذُوا مِنْهَا‏"‏‏.‏ قَالَ فَانْطَلَقْنَا تَعَادَى بِنَا خَيْلُنَا حَتَّى أَتَيْنَا الرَّوْضَةَ، فَإِذَا نَحْنُ بِالظَّعِينَةِ قُلْنَا لَهَا أَخْرِجِي الْكِتَابَ‏.‏ قَالَتْ مَا مَعِي كِتَابٌ‏.‏ فَقُلْنَا لَتُخْرِجِنَّ الْكِتَابَ أَوْ لَنُلْقِيَنَّ الثِّيَابَ، قَالَ فَأَخْرَجَتْهُ مِنْ عِقَاصِهَا، فَأَتَيْنَا بِهِ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَإِذَا فِيهِ مِنْ حَاطِبِ بْنِ أَبِي بَلْتَعَةَ إِلَى نَاسٍ بِمَكَّةَ مِنَ الْمُشْرِكِينَ، يُخْبِرُهُمْ بِبَعْضِ أَمْرِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ يَا حَاطِبُ مَا هَذَا ‏"‏‏.‏ قَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ لاَ تَعْجَلْ عَلَىَّ، إِنِّي كُنْتُ امْرَأً مُلْصَقًا فِي قُرَيْشٍ ـ يَقُولُ كُنْتُ حَلِيفًا وَلَمْ أَكُنْ مِنْ أَنْفُسِهَا ـ وَكَانَ مَنْ مَعَكَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ مَنْ لَهُمْ قَرَابَاتٌ، يَحْمُونَ أَهْلِيهِمْ وَأَمْوَالَهُمْ، فَأَحْبَبْتُ إِذْ فَاتَنِي ذَلِكَ مِنَ النَّسَبِ فِيهِمْ أَنْ أَتَّخِذَ عِنْدَهُمْ يَدًا يَحْمُونَ قَرَابَتِي، وَلَمْ أَفْعَلْهُ ارْتِدَادًا عَنْ دِينِي، وَلاَ رِضًا بِالْكُفْرِ بَعْدَ الإِسْلاَمِ‏.‏ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ أَمَا إِنَّهُ قَدْ صَدَقَكُمْ ‏"‏‏.‏ فَقَالَ عُمَرُ يَا رَسُولَ اللَّهِ دَعْنِي أَضْرِبْ عُنُقَ هَذَا الْمُنَافِقِ‏.‏ فَقَالَ ‏"‏ إِنَّهُ قَدْ شَهِدَ بَدْرًا، وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّ اللَّهَ اطَّلَعَ عَلَى مَنْ شَهِدَ بَدْرًا قَالَ اعْمَلُوا مَا شِئْتُمْ فَقَدْ غَفَرْتُ لَكُمْ ‏"‏‏.‏ فَأَنْزَلَ اللَّهُ السُّورَةَ: ‏((‏يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لاَ تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ أَوْلِيَاءَ تُلْقُونَ إِلَيْهِمْ بِالْمَوَدَّةِ‏))‏ إِلَى قَوْلِهِ: ((‏فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ))‏

Ametuhadithia Qutaybah, ametuhadithia Sufyaan toka kwa ‘Amri bin Diynaar amesema, amenieleza Al-Hasan bin Muhammad ya kuwa amemsikia ‘Ubaydullaah bin Abiy Raafiy’ akisema: “Nimemsikia ‘Aliy (رضي الله عنه) akisema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alinituma mimi pamoja na Az-Zubayr na Al-Miqdaad akituambia: ((Nendeni haraka hadi mfike Rawdhwat Khaaakh (eneo kati ya Makkah na Madiynah), kwani hapo yupo mwanamke ana barua, ichukueni toka kwake)). Akasema: Tukaondoka mbio na farasi wetu mpaka tukafika Ar-Rawdhwah na tukamkuta mwanamke huyo. Tukamwambia atoe barua hiyo, naye akasema sina barua. Tukamwambia: Lazima utaitoa barua au sisi tutakuvua nguo zako (tukupekue). Akasema: Akaitoa ndani ya kuruni la nywele zake na tukaja nayo kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Tukashtuka kukuta ndani yake ujumbe toka kwa Haatwib bin Abiy Balta'h kwenda kwa washirikina wa Makkah akiwaeleza baadhi ya mambo ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).  Hapo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ee Haatwib! Nini hii?)) Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Usinihukumie haraka. Hakika mimi nilikuwa mtu niliyeshikana sana na Maquraysh – anasema nilikuwa rafiki niliyeungana nao lakini si urafiki wa kidhati – na Muhaajiriyn walio pamoja nawe, walikuwa na jamaa zao, wanalinda watu wao na mali zao. Nikapenda, kwa kuwa sina nasaba yoyote kwao, nitengeneze kinga kutoka kwao ya kunilindia jamaa zangu. Nami sikufanya hilo kwa kuwa ati nimeritadi na dini yangu, au nimeridhia ukafiri baada ya Uislamu. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ama huyu hakika amewaambieni ukweli.)) ‘Umar akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Niruhusu nifyeke shingo ya mnafiki huyu. Akasema: ((Hakika yeye ameshiriki (vita vya) Badr. Na nini kitakujuza, huenda Allaah Alisimama mbele ya walioshiriki Badr Akawaambia: Fanyeni mtakalo, Mimi Nishawaghufirieni)) Hapo Allaah Akateremsha Suwrah:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ أَوْلِيَاءَ تُلْقُونَ إِلَيْهِم بِالْمَوَدَّةِ  

 

Enyi walioamini! Msifanye adui Wangu na adui wenu kuwa marafiki wandani mkiwapa mapenzi,  

 

Mpaka kauli Yake:

فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ

basi kwa yakini amepotea njia ya sawa.

 

[Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Share