36-Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Mwanamke Anayetokwa Majimaji Anafaa Kusoma Qur-aan Na Kuswali Swalaah Za Sunnah?

 

 

Fataawaa Mas-ala 60 Kuhusu Hedhi Na Nifaas

 

36-Mwanamke Anayetokwa Majimaji Anafaa Kusoma Qur-aan

Na Kuswali Swalaah Za Sunnah?

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Mwanamke akitawadha ambae hutokwa na majimaji haya kwa ajili ya Swalaah ya faradhi je ni sahihi kwake aswali anachotaka kwa ajili ya Sunnah na kusoma Qur-aan  kwa wudhu wa faradhi ile kwa ajili ya faradhi  nyingine?

 

 

 

JIBU:

 

 

Akitawadha kwa ajili ya Swalaah ya faradhi kwa  wakati wake wa mwanzo  basi ni juu  yake  kuswali faradhi, Sunnah au kusoma Qur-aan hadi wakati mwingine wa Swalaah nyingine.

 

Share