48-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

 

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

48-Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ يَوْمًا فَصَلَّى عَلَى أَهْلِ أُحُدٍ صَلاَتَهُ عَلَى الْمَيِّتِ، ثُمَّ انْصَرَفَ إِلَى الْمِنْبَرِ فَقَالَ ‏ "‏ إِنِّي فَرَطٌ لَكُمْ، وَأَنَا شَهِيدٌ عَلَيْكُمْ، وَإِنِّي وَاللَّهِ لأَنْظُرُ إِلَى حَوْضِي الآنَ، وَإِنِّي أُعْطِيتُ مَفَاتِيحَ خَزَائِنِ الأَرْضِ ـ أَوْ مَفَاتِيحَ الأَرْضِ ـ وَإِنِّي وَاللَّهِ مَا أَخَافُ عَلَيْكُمْ أَنْ تُشْرِكُوا بَعْدِي، وَلَكِنْ أَخَافُ عَلَيْكُمْ أَنْ تَنَافَسُوا فِيهَا ‏"‏‏.‏

 

Kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) amesema: Siku moja Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikwenda nje na akaongoza Swalaah za maiti; Mashuhadaa wa Uhd, kisha akapanda katika Minbar akasema: “Mimi nitaandaa njia kwa ajili yenu kama muasisi na nitakuwa Shahidi kwa ajili yenu. Na wa-Allaahi, ninaiona Al-Hawdhw (chemchemi ya Al-Kawthar) sasa hivi na nimepewa funguo za hazina zote za ardhi (au funguo za ardhi). Na Wa-Allaahi, hakika mimi sikhofu kuwa mtamshirikisha Allaah baada ya kufa kwangu, lakini nakhofu kuwa mtagombana baina yenu kwa ajili ya vitu vya kidunia.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Kupewa Hazina Za Ulimwengu: Ni kuongezeka na kupanuka Uislamu, na kujaaliwa ushindi mkubwa na mateka ya mali, kwa sababu unapopatikana ushindi wa nchi ni sawa na kumiliki mali na hazina zake.

 

 

Share