Sharh Asmaa Allaah Al-Husnaa Wa Swifaatihi (من) تيسير الكريم الرحمن في تفسير كلام المنان

 

Sharh Asmaa Allaah Al-Husnaa Wa Swifaatihi

 

(Maelezo Ya Majina Mazuri Ya Allaah Na Swiffah Zake)

 

 

Yamechukuliwa Kutoka:

 

تيسير الكريم الرحمن في تفسير كلام المنان

العلامة الشيخ عبد الرحمن بن ناصر السعدي

 

Taysiyr Al-Kariym Ar-Rahmaan Fiy Tafsiyr

Kalaam Al-Mannaan

 

 

Al-‘Allaamah Ash-Shaykh

‘Abdirrahmaan Bin Naaswir As-Sa’diy (1307-1376)

 

 

Imetafsiriwa Kwa Lugha Ya Kiingereza Na Abu Rumaysah

 

Imetarjumiwa Na Kuhaririwa Na Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Yaliyomo

 

 

1- Orodha Ya Majina Ya Allaah عز وجل Na Maana Zake Ki Mukhtasari

 

 

2-Dibaji Ya Mfasiri Wa Kitabu Cha Kiingereza Kutoka Kiarabu

 

 

3-Baadhi Ya Sifa Za Allaah Zilizotajwa Katika Qur-aan

 

 

4-Onyo Dhidi Ya Tafsiri Ya Majina Na Sifa Za Allaah Kwa Namna Ya Kitamathali

 

 

5-Wasifu Wa ‘Allaamah Abu ‘Abdirrahmaan Naaswir As-Sa’diy  

 

 

6-Sharh Ya Majina Mazuri Na Kamilifu Ya Allaah (Na Swiffah Zake)

 

 

 

 

01-Orodha Ya Majina Ya Allaah  عز وجل Na Maana Zake Ki Mukhtasari

 

Jina/

Swiffah

 

Tamshi

Maana

 

الرّب

 

Ar-Rabb

 

Rabb Wa Kila Kitu, Mola, Bwana, Muumbaji, Msimamizi, Mneemeshaji, Mfalme, Mwenye Kuruzuku, Mwendeshaji wa Mambo, Mlezi.

 

 

الله

Allaah

 

Mwenye Uluwhiyyah, Mwenye ‘Ubuwdiyyah

 

 

الملك

Al-Malik

 

Mfalme

 

 

المالك

Al-Maalik

 

Mwenye Kumiliki

 

 

الّذي له الملك

Alladhiy Lahul-Mulk

 

Ambaye Ufalme ni Wake

 

الواحد

Al-Waahid

 

Mmoja Pekee Asiye Na Mfano

 

 

الأحد

Al-Ahad

 

Mpweke Asiye Na Mshirika

 

الصّمد

Asw-Swamad

 

Mwenye Kukusudiwa Kwa Haja Zote

 

العليم

Al-‘Aliym

 

Mjuzi Wa Yote Daima

الخبير

Al-Khabiyr

 

Mjuzi Wa Undani Na Kina Cha Mambo, Mwenye Ujuzi Wa Ya Dhahiri Na Ya Siri

 

الحكيم

Al-Hakiym

 

Mwenye Hikmah Wa Yote Daima

 

الرّحمن

Ar-Rahmaan

 

Mwingi Wa Rehma

الرّحيم

Ar-Rahiym

 

Mwenye Kurehemu 

البرّ

Al-Barr

 

Mwingi Wa Ihsani

الكريم

Al-Kariym

 

Karimu, Mtukufu

الجوّاد

Al-Jawwaad:

 

Mwingi wa Ukarimu

الرّؤف

Ar-Rauwf

 

Mwenye Huruma Mno

الواهَاب

Al-Wahhaab

 

Mwingi Wa Kutunuku, Mpaji Wa Yote

 

السّميع

As-Samiy’i

 

Mwenye Kusikia Yote Daima

 

البصير

Al-Baswiyr

 

Mwenye Kuona Yote Daima

 

الحميد

Al-Hamiyd

 

Mwenye Kustahiki Kuhimidiwa

 

المجيد

Al-Majiyd

 

Mwingi Mno Wa Vipawa Na Ukarimu

 

الكبير

Al-Kabiyr

 

Mkubwa Wa Dhati, Vitendo Na Sifa

 

العظيم

Al-‘Adhwiym

 

Adhimu, Mwenye Taadhima

 

الجليل

Al-Jaliyl

 

Jalali, Mwenye Ujalali, Mtukuka Daima, Mwenye Hadhi

 

العفوّ

Al-‘Afuww

 

Mwingi Wa Kusamehe

الغفور

Al-Ghafuwr

 

Mwingi Wa Kughufiria, Kusitiri

 

الغفّار

Al-Ghaffaar

 

Mwingi Wa Kughufuria, Kusitiri Mara Kwa Mara

 

التواب

At-Tawwaab

 

Mwingi Wa Kupokea Toba Baada Ya Toba

 

القدّوس

Al-Qudduws

 

Mtakatifu, Ametakasika Na Sifa Zote Hasi

 

السّلام

As-Salaam

 

Mwenye Amani, Mwenye Kusalimika Na Kasoro Zote

 

العلي

Al-‘Aliyy

 

Yuko Juu Ya Vyote, Mwenye Uluwa

 

الأعلى

Al-A’laa

 

Mwenye Uluwa Na Taadhima Kuliko Vyote

 

العزيز

Al-‘Aziyz

 

Mwenye Nguvu, Mshindi Asiyeshindika Daima

 

القوي

Al-Qawiyy

 

Mwenye Nguvu

المتين

Al-Matiyn

 

Mwenye Nguvu Na Shadidi, Madhubuti

 

الجبّار

Al-Jabbaar

 

Jabari, Mwenye Kulazimisha, Mwenye Kuunga

 

المتكبّر

Al-Mutakabbir

 

Mwenye Kustahiki Kutakabari, Yuko Juu Ya Viumbe

 

الخالق

Al-Khaaliq

 

Muumbaji

البارء

Al-Baariu

Muumbaji Wa Viumbe Kwa Maumbile Yanayonasibiana Na Mazingira Ya Maisha Yao

 

المصوّر

Al-Muswawwir

 

Muundaji Sura Na Umbo

المؤمن

Al-Muumin

 

Mwenye Kusadikisha Ahadi, Mwenye Kuaminisha

 

المهيمن

Al-Muhaymin

 

Mwenye Kutawalia Na Kuendesha

 

القدير

Al-Qadiyr

 

Muweza Wa Yote Daima

اللّطيف

Al-Latwiyf

 

Latifu, Mwenye Kudabiri Mambo Kwa Utuvu, Mjuzi Wa Ya Dhihiri Na Ya Siri

 

الحسيب

Al-Hasiyb

 

Mwenye Kuhesabu, Kutosheleza

 

الرقيب

Ar-Raqiyb

 

Mwenye Kuchunga

الحفيظ

Al-Hafiydhw

 

Mwenye Kuhifadhi, Kulinda

 

المحيط

Al-Muhiytw

Mwenye Kuzunguka Vyote

 

القهّار

Al-Qahhaar

 

Mwenye Kuteza Nguvu Asiyepingika

 

القاهر

Al-Qaahir

 

Mwenye Kuteza Nguvu, Asiyepingika

المقيت

Al-Muqiyt

 

Mwenye Kuruzuku Chakula

 

الوكيل

Al-Wakiyl

 

Mtegemewa Kwa Yote, Msimamizi

 

ذو الجلال والإكرام

Dhul-Jalal Wal-Ikraam

 

Mwenye Ujalali Na Ukarimu,Mwenye Utukufu wa Juu Kabisa, Ukarimu Na Hadhi

 

الودود

Al-Waduwd

 

Mwenye Mapenzi Tele Halisi

الفتّاح

Al-Fattaah

 

Mwingi Wa Kufungua, Kuhukumu

 

الرّزاق

Ar-Razzaaq

 

Mwingi Wa Kuwaruzuku Viumbe Vyote

 

الحكم

Al-Hakam

 

Hakimu Mwadilifu Wa Haki Zaidi Kuliko Wote

 

العدل

Al-‘Adl

 

Mwadilifu Kuliko Wote

جامع الناس

Jaami’un-Naas

 

Mwenye Kuwakusanya Watu

 

الحيّ

Al-Hayyu

 

Aliye Hai Daima

القيّوم

Al-Qayyuwm

 

Msimamizi Wa Kila Jambo Milele

 

النور

An-Nuwr

 

Mwenye Nuru, Mwanga

بديع السماوات والأرض

Badiy’us-Samaawaat Wal-Ardhw

Mwanzishaji wa Mbingu na Ardhi

 

القابض

Al-Qaabidhw

 

Mwenye Kuchukua

الباسط

Al-Baasitw

 

Mwenye Kukunjua

المعطي

Al-Mu’twiy

 

Mpaji

المانع

Al-Maani’u

 

Mwenye Kuzuia

الشهيد

Ash-Shahiyd

Shahidi Mwenye Kujua Vyema Yenye Kuonekana Na Yasiyoonekana, Mwenye Kushuhudia

 

المبدء

Al-Mubdiu

 

Mwanzishaji

المعيد

Al-Mu’iyd

 

Mrejeshaji

الفعّال لما يريد

Al-Fa-‘aalu Limaa Yuriyd

 

Mwenye kufanya Atakacho

الغني

Al-Ghaniyy

 

Mkwasi Amejitosheleza, Hahitaji Lolote

المغني

Al-Mughniy

 

Al-Mughniy

 Mkwasi,

Amejitajirisha

 

الحليم

Al-Haliym

 

Mpole Wa Kuwavumilia Waja

الشّاكر

Ash-Shaakir

 

Mwenye Kupokea Shukurani

الشكور

Ash-Shakuwr

 

Mwingi Wa Shukrani, Mwingi Wa Kukubali Kidogo Kwa Thawabu Tele

 

القريب

Al-Qariyb

 

Aliye Karibu

المجيب

Al-Mujiyb

 

Mwenye Kuitikia

 

الكافي

Al-Kaafiy

 

Aliyejitosheleza

الأوّل

Al-Awwal

 

Wa Kwanza Bila Mwanzo

الآخر

Al-Aakhir

 

Wa Mwisho, Hapana Kitu Baada Yake

الظّاهر

Adhw-Dhwaahir

 

Dhahiri Kwa Vitendo Vyake

الباطن

Al-Baatwin

 

Asiyeonekana Na Viumbe

الواسع

Al-Waasi’u

 

Aliyeenea

الهادي

Al-Haadiy

 

Mwenye Kuongoza

الرّشيد

Ar-Rashiyd

 

Mwenye Kuelekeza, Kuongoza

الحق

Al-Haqq

Wa Haki, Wa Kweli

 

 

 

Majina Mengineyo Ambayo Hayakutajwa Hapo Juu

 

Jina/

Swiffah

 

Tamshi

Maana

العالم

Al-‘Aalim

 

Mjuzi wa Yote Daima

الحفي

Al-Hafiyy

 

Mwenye Kutoa Utukufu

الأكرم

Al-Akram

 

Mkarimu Kuliko Wote

الإله

Al-Ilaah

 

Ilaah - Mwabudiwa Wa Haki

الخلاّق

Al-Khallaaq

 

Muumbaji Wa Kila Namna Kwa Wingi 

المليك

Al-Maliyk

 

Mfalme Mwenye Nguvu Daima

المبين

Al-Mubiyn

 

Mwenye Kubainisha

المولى

Al-Mawlaa

 

Maula, Bwana Mlezi, Msaidizi, Msimamizi 

المقتدر

Al-Muqtadir

 

Mwenye Uwezo Wa Juu Kabisa

المتعّال

Al-Muta’aal

 

Mwenye Uluwa Na Taadhima

القادر

Al-Qaadir

 

Mwenye Uwezo

الوارث

Al-Waarith

Mrithi Kwa Kuondosha Viumbe Wote Na Kubaki Yeye Tu

 

الولي

Al-Waliyyu

 

Walii, Aliye Karibu

النصير

An-Naswiyr

Mwenye Kunusuru, Msaidizi

 

 

02- Dibaji Ya Mfasiri Wa Kitabu Cha Kiingereza Kutoka Kiarabu

 

 

 

Himdi na shukurani zote ni kwa Allaah. Tunamhimidi, tunamwomba msaada na maghfirah. Anayeongozwa na Allaah hakuna wa kumpotosha na ambaye Allaah Anamwacha apotee, hakuna wa kumwongoza. Nashuhudia kwamba hapana apasaye  kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah Peke Yake, hana mshirika na nashuhudia kwamba  Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ni Mja na Rasuli Wake.

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٨٠﴾

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanamili katika kukadhibisha Majina Yake, watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda. [Al-A’raaf (7): 180]

 

 

Kutoka katika vituo vitukufu na vya juu zaidi vya utambuzi ni kumjua Allaah (سبحانه وتعالى), kupitia uzuri Wake. Hii ndiyo elimu waliyo nayo wasomi wa uumbwaji huu. Wote wanamjua kupitia miongoni mwa Sifa Zake lakini wenye utambuzi kamilifu zaidi ni wanomjua kupitia ukamilifu Wake, Utaadhima (Utukufu) Wake na Uzuri Wake. Hakuna chenye kufanana Naye katika Sifa Yake yoyote ile, na kama utachukulia kuwa uumbaji Wake ulikuwa katika namna bora sana, na ukataka kujaribu na kulinganisha jumla ya uzuri Wake wake wa ndani na wa nje na uzuri wa Allaah (سبحانه وتعالى), ulinganisho huo utakuwa hafifu kuliko tochi yenye mwangaza hafifu kuwashwa mkabala na  kisahani kinachowaka cha jua.

 

Inatosha kujua uzuri Wake kwamba kama kizuizi Chake kingeondolewa, kila kitukufu cha Dhati Yake kinawafikia viumbe Wake kingefutika kabisa. Inatosha kujua kuwa uzuri wote, wa nje na ndani, unaopatikana ulimwenguni humu na Aakhirah, ni matokeo ya athari ya kazi Yake, hivyo, ni nini basi anachoweza mtu kuhisi kuhusu uzuri wa Ambaye uzuri huu umetoka Kwake? Inatosha kujua uzuri Wake kuwa, Kwake ndipo ilipomiliki taadhima yote kikamilifu, nguvu na uwezo wote kikamilifu, ukarimu wote, upaji wote, elimu yote na Rahmah yote.

 

 

Kutoka katika Nuru ya Dhati Yake kiza chote hutiwa nuru, kama Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alivyosema pindi alipoomba du’aa huko Twaaif:

 

أَعُوذُ بِنُورِ وَجْهِكَ الَّذِي أَشْرَقَتْ لَهُ الظُّلُمَات وَصَلَحَ عَلَيْهِ أَمْر الدُّنيْا وَالآخِرَة

 

Najikinga kwa Nuru ya Wajihi Wako inayotia Nuru kiza na juu yake mambo ya duniani na Aakhirah hupangiliwa.[1]

 

 

‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه) amesema: “Hapana usiku na mchana pamoja kwa Rabb Wako, Nuru ya mbingu na ardhi huja kutokana na Nuru ya Dhati yake.”[2] Kwa hivyo, Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Nuru ya mbingu na ardhi na katika Siku ya Hukmu, pindi Atakapohukumu watu, Nuru Yake itaiangaza dunia.

 

 

Mojawapo katika Majina Yake ni Al-Jamiyl (Mzuri), Imesimuliwa kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa amesema:

 

الله جَمِيلُ يُحِبُّ الْجَمال

((Allaah ni Jamiyl (Mzuri) na Anapenda uzuri))” [Muslim]

 

 

Uzuri Wake ni hatua nne, uzuri wa Dhati Yake, uzuri wa Sifa Zake, uzuri wa Vitendo Vyake na uzuri wa Majina Yake.

 

 

Majina Yake yote ni mazuri, Sifa Zake zote ni kamilifu, matendo Yake yote yameegemea katika hikma safi kabisa, ni zenye manufaa, za haki na pia ni Rahmah.

 

 

Hivyo, ni juu ya mja kujua kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki ghairi Yake Allaah (سبحانه وتعالى), ni juu yake kumpenda Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) kwasababu Yeye ni Yeye na kwa sababu ya ukamilifu Wake. Pia ni juu ya mja kujua kuwa kwa ukweli hakuna anayemfadhili mmojawapo kwa kila namna ya baraka za nje na ndani isipokuwa Yeye Allaah (عز وجل) na kwa hivyo anapaswa ampende Yeye kwa hili pia, na amsifu Yeye. Hivyo, mja anapaswa ampende Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) kwa sababu ya mambo yote haya mawili. [Ibn Al-Qayyim, Al-Fawaaid (uk 258)]

 

 

Katika kushikamana na mahimizo ya hapo juu, tasnifu hii imedondolewa kutoka katika maneno ya ufunguzi ya Imaam Naaswir As-Sa’diy (رحمه الله) katika Tafsiyr yake ya Qur-aan, Tafsiyr Al-Kariym Ar-Rahman, ambamo kwa ufupi na kwa vizuri ameeleza Majina hayo ya Allaah yanayojitokeza katika Qur-aan. Baada ya kila maelezo, mwandishi ameongeza baadhi ya Aayah za Qur-aan kuonesha matumizi ya Jina fulani mahsusi. Inapaswa itambulike kuwa mwandishi  (رحمه الله)  ametaja tu Majina yanayojitokeza katika Qur-aan na idadi yake kwa ujumla inafikia themanini na tisa kwa mtazamo wake. Majina ya ziada yaliyotajwa katika Qur-aan yameongezwa kutokana na kazi ya Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (رحمه الله) katika Qawaaidul-Muthlaa fiy SwifaatiLLaah wa Asmaaihil-Husnaa na kuleta jumla ya mia moja na tatu.

 

 

Kabla ya kuendelea na makala au kitabu hiki, itakuwa ni jambo la manufaa kuleta baadhi ya kanuni za ujumla kuhusu Majina ya Allaah (عز وجل)[3]

 

 

i-Majina Yote Ya Allaah Ni Mazuri Na Makamilifu

 

 

Hii ni kwa sababu yanaunda maelezo kamilifu na Sifa zisozo na ila hata kidogo, wala hazina japo uwezekano wa kuwa na kasoro. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa. [Al-A’raaf (7): 180]

 

 

 

ii-Majina Ya Allaah Ni Halisi Na Maelezo Halisi

 

 

Ni Majina halisi kulingana na kukuwa yanamaanisha Dhati ya Allaah (عز وجل) na maelezo kulingana na maana zake; Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٨﴾

Naye Ndiye Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Ahqaaf (46):8]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَرَبُّكَ الْغَفُورُ ذُو الرَّحْمَةِ ۖ

Na Rabb wako ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye Rahmah. [Al-Kahf (18):58]

 

 

Hivyo Aayah ya pili inathibitisha kuwa Mwenye Rahmah ni Ambaye Ana Sifa hiyo na ameelezwa kwa Rahmah. Hapo pia kuna muwafaka wa wanaisimu kuwa neno

 

عليم

‘Mjuzi’

 

Hupewa mwenye ujuzi tu.

 

Na neno la

سميع

‘Mwenye kusikia’

 

 

Hupewa mwenye kusikia tu, na kuendelea.

 

 

 

iii-Ikiwa Jina La Allaah Linajulisha Maelezo Elekezi

 

 

Ni muhimu kuthibitisha mambo matatu:

 

1-Jina hilo hasa

 

2-Sifa inayojulishwa na Jina hilo

 

3-Hukmu na matumizi ya lazima yaliyomo (katika kutajwa kwa Jina hilo)

 

 

Hii ndiyo sababu ‘Ulamaa wameeleza kuwa adhabu iliyowekwa kwa waporaji wa njiani imeondolewa ikiwa watatubu, kwa mujibu wa kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن قَبْلِ أَن تَقْدِرُوا عَلَيْهِمْ ۖ فَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣٤﴾

Isipokuwa wale waliotubia kabla ya kuwashinda nguvu basi jueni kwamba hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Maa-idah (5): 34]

 

 

Hii ni kwasababu, kidokezo muhimu kwa Majina haya mawili, ni kuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Amewaghufuria dhambi zao na Amewaonyesha Rahmah kwa kuwaondolea kutumika adhabu waliyowekewa.

 

 

Halikadhalika, neno la

 

السميع

‘Mwenye kusikia yote daima’

 

 

Linashurutisha kuwa unathibitisha Jina hili, Sifa ya Kusikia na kidokezo cha lazima kuwa Anasikia yote, ya siri na dhahiri.

 

 

Ikiwa jina si elekezi, basi ni muhimu tu kuthibitisha mambo ya mawili ya mwanzo yaliyotajwa hapo juu. Kwa mfano, Jina

 

الحيّ

 

‘Aliye Hai daima’

 

 

Ni muhinu kuthibitisha Jina hili na Sifa inazohusiana nayo ya uhai.

 

 

 

iv- Jina La Allaah Linaweza Kujulikana Kwa Kupitia Wahy Tu

 

 

 

Hii ni kwasababu hakuna njia ya kiakili tu ya kuyajua. Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾

Na wala usifuatilie usiyo na elimu nayo. Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitaulizwa. [Al-Israa (17) :36]

 

 

 

v-Majina Ya Allaah Hayajafungika Kwa Idadi Yoyote

 

  

Hii inatokana na Hadiyth Swahiyh ya Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiomba:

 

للَّهُمَّ إِنِّي عَبْدُكَ، وَابْنُ عَبْدِكَ، وَابْنُ أَمَتِكَ، نَاصِيَتِي بِيَدِكَ، مَاضٍ فِيَّ حُكْمُكَ، عَدْلٌ فِيَّ قَضَاؤُكَ، أَسْأَلُكَ بِكُلِّ اسْمٍ هُوَ لَكَ سَمَّيْتَ بِهِ نَفْسَكَ، أَوْ عَلَّمْتَهُ أَحَدًا مِنْ خَلْقِكَ، أَوْ أَنْزَلْتَهُ فِي كِتَابِكَ، أَوْ اسْتَأْثَرْتَ بِهِ فِي عِلْمِ الْغَيْبِ عِنْدَكَ، أَنْ تَجْعَلَ الْقُرْآنَ رَبِيعَ قَلْبِي، وَنُورَ صَدْرِي، وَجَلَاءَ حُزْنِي، وَذَهَابَ هَمِّي

Ee Allaah hakika mimi ni mja Wako, mtoto wa mja Wako, mtoto wa kijakazi Chako, utosi wangu uko Mikononi Mwako, yaliyopita kwangu yako katika hukumu Yako, ni usawa kwangu kunihukumu Kwako, nakuomba kwa kila Jina ambalo ni Lako Ulilojiita  Mwenyewe au Uliloliteremsha katika Kitabu Chako, au Ulilomfundisha yeyote yule kati ya viumbe Vyako, au Ulilolihifadhi Wewe Mwenyewe (na kujihusisha kulijua) katika ’ilmu ya ghayb Kwako, nakuomba Ujaalie Qur-aan kuwa ni rabiy' (uhuisho, raha, furaha na ustawisho) wa moyo wangu na nuru ya kifua changu, na ufumbuzi wa  huzuni yangu, na sababu ya kuondoka wahka wangu kujifunza.” [Ameipokea Ahmad (1/391) [452], Al-Haakim (1/509) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika As-Silsilah Asw-Swahiyhah (199) na Al-Kalimi Atw-Twayyib (124)]

 

Haiwezekani kuyafungia Majina hayo ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) Ameyahifadhi Kwake katika ghaibu kwa kuweka idadi au kuyaenea. Kuhusu Hadiyth inayotaja Majina tisini na tisa, maana yake ni kuwa, mwenye kuyahifadhi, kuyaelewa na kuyatumia katika maisha yake ya kila siku, idadi hii ya majina, ataingia Jannah (Peponi).

 

 

 

 

3-Baadhi Ya Sifa Za Allaah (عز وجل) Zilizotajwa Katika Qur-aan

 

 

 

 

أَحْكَمُ الْحَاكِمِينَ

Mwadilifu Zaidi Wa Wanaohukumu Kuliko Mahakimu Wote.

 

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَنَادَىٰ نُوحٌ رَّبَّهُ فَقَالَ رَبِّ إِنَّ ابْنِي مِنْ أَهْلِي وَإِنَّ وَعْدَكَ الْحَقُّ وَأَنتَ أَحْكَمُ الْحَاكِمِينَ﴿٤٥﴾

Na Nuwh akamwita Rabb wake, akasema: Rabb wangu! Hakika mwanangu ni katika ahli zangu, na hakika ahadi Yako ni ya kweli, Nawe ni Mwadilifu zaidi wa wanaohukumu kuliko mahakimu wote.  [Huwd (11): 45]

 

 

 

أَهْلُ الْمَغْفِرَةِ

Mstahiki Wa Kughufuria (Madhambi)

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ ۚ هُوَ أَهْلُ التَّقْوَىٰ وَأَهْلُ الْمَغْفِرَةِ﴿٥٦﴾

Na hawatowaidhika isipokuwa Akitaka Allaah; Yeye Ndiye Mstahiki wa kuogopwa, na Mstahiki wa kughufuria (madhambi).  [Al-Muddath-thir (74): 56]

 

 

 

 

عالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ

Mjuzi Wa Ghayb Na Dhahiri

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَهُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ ۖ وَيَوْمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُ ۚ قَوْلُهُ الْحَقُّ ۚ وَلَهُ الْمُلْكُ يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ ۚ عالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ ۚ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ ﴿٧٣﴾

Naye Ndiye Ambaye Ameumba mbingu na ardhi kwa haki. Na Siku Atakaposema: Kun! basi (jambo) huwa! Kauli Yake ni haki.  Naye Atakuwa na ufalme Siku itakapopulizwa baragumu. Mjuzi wa ghayb na dhahiri. Naye ni Mwenye hikmah wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika.  [Al-An-‘Aam (6): 73]

 

 

 

عَلَّامُ الْغُيُوبِ

Mjuzi Wa Ghayb

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَوْمَ يَجْمَعُ اللَّـهُ الرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَا أُجِبْتُمْ ۖ قَالُوا لَا عِلْمَ لَنَا ۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ ﴿١٠٩﴾

Siku Allaah Atakayowakusanya Rusuli na Kuwaambia: Mlijibiwa nini? Watasema: Hatuna ujuzi nalo; hakika Wewe Ndiye Mjuzi wa ghayb. [Al-Maa-idah (5): 109]

 

 

 

أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ

Mbora Zaidi Wa Kurehemu

Kuliko Wengine Wote Wenye Kurehemu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ رَبِّ اغْفِرْ لِي وَلِأَخِي وَأَدْخِلْنَا فِي رَحْمَتِكَ ۖ وَأَنتَ أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ ﴿١٥١﴾

 (Muwsaa) Akasema: Rabb wangu! Nighufurie na kaka yangu, na Utuingize katika rahmah Yako. Nawe ni Mbora zaidi wa kurehemu kuliko wengine wote wenye kurehemu. [Al-A’raaf (7) 151]

 

 

 

 

أَسْرَعُ الْحَاسِبِينَ

Mwepesi Zaidi Kuliko Wote Wanaohisabu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ثُمَّ رُدُّوا إِلَى اللَّـهِ مَوْلَاهُمُ الْحَقِّ ۚ أَلَا لَهُ الْحُكْمُ وَهُوَ أَسْرَعُ الْحَاسِبِينَ ﴿٦٢﴾

Kisha hurudishwa kwa Allaah Rabb wao wa haki. Tanabahi! Hukumu ni Yake Pekee; Naye ni Mwepesi zaidi kuliko wote wanaohisabu. [Al-An’Aam (6): 62]

 

 

 

 

ذُو الْعَرْشِ

Mwenye ‘Arsh

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

رَفِيعُ الدَّرَجَاتِ ذُو الْعَرْشِ يُلْقِي الرُّوحَ مِنْ أَمْرِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ لِيُنذِرَ يَوْمَ التَّلَاقِ﴿١٥﴾

 (Allaah) Mwenye uluwa juu ya vyeo na daraja. Mwenye ‘Arsh, Anapelekea Ar-Ruwh (Wahy) kwa amri Yake kwa Amtakaye miongoni mwa waja Wake, ili aonye Siku ya kukutana. [Ghaafir (40): 15]

 

 

 

 

ذُو فَضْلٍ

Mwenye Fadhila

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ خَرَجُوا مِن دِيَارِهِمْ وَهُمْ أُلُوفٌ حَذَرَ الْمَوْتِ فَقَالَ لَهُمُ اللَّـهُ مُوتُوا ثُمَّ أَحْيَاهُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ لَذُو فَضْلٍ عَلَى النَّاسِ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَشْكُرُونَ ﴿٢٤٣﴾

Je, hukuwaona wale walitoka majumbani mwao nao wakiwa ni maelfu wakikhofu mauti, Allaah Akawaambia: Kufeni kisha Akawahuisha? Hakika Allaah ni Mwenye fadhila juu ya watu lakini watu wengi hawashukuru.  [[Al-Baqarah (2): 243]

 

 

 

ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ

Mwenye Fadhila Adhimu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَخْتَصُّ بِرَحْمَتِهِ مَن يَشَاءُ ۗ وَاللَّـهُ ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ ﴿٧٤﴾

Humchagua kwa rahmah Yake Amtakaye; na Allaah ni Mwenye fadhila adhimu. [Aali ‘Imraan (3): 74]

 

 

 

 

 

ذُو انتِقَامٍ

Mwenye Kulipiza

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْتُلُوا الصَّيْدَ وَأَنتُمْ حُرُمٌ ۚ وَمَن قَتَلَهُ مِنكُم مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاءٌ مِّثْلُ مَا قَتَلَ مِنَ النَّعَمِ يَحْكُمُ بِهِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ هَدْيًا بَالِغَ الْكَعْبَةِ أَوْ كَفَّارَةٌ طَعَامُ مَسَاكِينَ أَوْ عَدْلُ ذَٰلِكَ صِيَامًا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمْرِهِ ۗ عَفَا اللَّـهُ عَمَّا سَلَفَ ۚ وَمَنْ عَادَ فَيَنتَقِمُ اللَّـهُ مِنْهُ ۗ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ ﴿٩٥﴾

Enyi walioamini! Msiue mawindo na hali mko katika ihraam. Na atakayemuua (mnyama) miongoni mwenu kwa kusudi, basi malipo yake itakuwa ni kilicho sawa na alichokiua katika wanyama wa mifugo. Kama wanavyohukumu wawili wenye uadilifu miongoni mwenu. Mnyama huyo afikishwe Ka’bah, au kafara ya kulisha maskini, au badala ya hayo, kufunga swiyaam ili aonje matokeo maovu ya jambo lake. Allaah Ameshasamehe yaliyopita; na yeyote atakayerudia tena, basi Allaah Atamlipiza (kumuadhibu). Na Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kulipiza.  [Al-Maa-idah (5): 95]

 

 

 

ذُو عِقَابٍ أَلِيمٍ

Mwenye Adhabu Iumizayo.

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّا يُقَالُ لَكَ إِلَّا مَا قَدْ قِيلَ لِلرُّسُلِ مِن قَبْلِكَ ۚ إِنَّ رَبَّكَ لَذُو مَغْفِرَةٍ وَذُو عِقَابٍ أَلِيمٍ﴿٤٣﴾

Huambiwi (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) isipokuwa yale yale waliyokwisha ambiwa Rusuli kabla yako. Hakika Rabb wako ni Mwenye maghfirah na Mwenye adhabu iumizayo. [Fusswilat (41: 43]

 

ذو المعارج

Mwenye Kumiliki Njia Za Kupandia

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

سَأَلَ سَائِلٌ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ﴿١﴾ لِّلْكَافِرِينَ لَيْسَ لَهُ دَافِعٌ﴿٢﴾ مِّنَ اللَّـهِ ذِي الْمَعَارِجِ﴿٣﴾

 

Muulizaji ameuliza kuhusu adhabu itakayotokea. Kwa makafiri, ambayo hakuna wa kuikinga. Kutoka kwa Allaah Mwenye kumiliki njia za kupandia.   [Al-Ma’aarij (70: 1 - 3]

 

 

 

ذُو مَغْفِرَةٍ

Mwenye Maghfira

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَيَسْتَعْجِلُونَكَ بِالسَّيِّئَةِ قَبْلَ الْحَسَنَةِ وَقَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِمُ الْمَثُلَاتُ ۗ وَإِنَّ رَبَّكَ لَذُو مَغْفِرَةٍ لِّلنَّاسِ عَلَىٰ ظُلْمِهِمْ ۖ وَإِنَّ رَبَّكَ لَشَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٦﴾

  Na wanakuhimiza kwa maovu kabla ya mazuri, na hali imekwishapita kabla yao mifano ya adhabu. Na hakika Rabb wako ni Mwenye maghfirah kwa watu juu ya dhulma zao, na hakika Rabb wako ni Mkali wa kuakibu. [Ar-Ra’d (13): 6]

 

 

 

 

ذُو الْقُوَّةِ

Mwenye Nguvu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ ﴿٥٨﴾

Hakika Allaah Ndiye Mwingi wa kuruzuku, Mwenye nguvu Madhubuti.  [Adh-Dhaariyyaat (51): 58]

 

 

 

 

ذُو الرَّحْمَةِ ۚ

Mwenye Rahmah

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَرَبُّكَ الْغَنِيُّ ذُو الرَّحْمَةِ ۚ إِن يَشَأْ يُذْهِبْكُمْ وَيَسْتَخْلِفْ مِن بَعْدِكُم مَّا يَشَاءُ كَمَا أَنشَأَكُم مِّن ذُرِّيَّةِ قَوْمٍ آخَرِينَ ﴿١٣٣﴾

Na Rabb wako ni Mkwasi Mwenye rahmah. Akitaka Atakuondosheni na Aweke wengine watakaofuatia baada yenu kwa Atakao, kama vile Alivyokuzalisheni kutokana na vizazi vya watu wengine.  [Al-An’aam (6): 147]

 

 

 

ذُو الطَّوْلِ

Mwenye Wingi Wa Ukarimu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

غَافِرِ الذَّنبِ وَقَابِلِ التَّوْبِ شَدِيدِ الْعِقَابِ ذِي الطَّوْلِ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ إِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Mwenye kughufuria dhambi, Anayepokea tawbah, Mkali wa kuakibu, Mwenye wingi wa Ukarimu, hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake ndio mahali pa kuishia.  [Ghaafir (40): 3]

 

 

 

 

 

فَالِقُ الْحَبِّ وَالنَّوَىٰ

Mpasuaji Wa Mbegu Na Kokwa

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ فَالِقُ الْحَبِّ وَالنَّوَىٰ ۖ يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَمُخْرِجُ الْمَيِّتِ مِنَ الْحَيِّ ۚ ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ ۖ فَأَنَّىٰ تُؤْفَكُونَ ﴿٩٥﴾

Hakika Allaah ni Mpasuaji wa mbegu na kokwa (zikawa miche). Anatoa kilicho hai kutokana na kilicho mfu na Mtoaji kilicho mfu kutokana na kilicho hai. Huyo Ndiye kwenu Allaah. Basi vipi mnaghilibiwa?   [Al-An’aam (6): 95]

 

 

 

 

 

فَاطِرُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ

Muanzilishi Wa Mbingu Na Ardhi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

قُلْ أَغَيْرَ اللَّـهِ أَتَّخِذُ وَلِيًّا فَاطِرِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَهُوَ يُطْعِمُ وَلَا يُطْعَمُ ۗ قُلْ إِنِّي أُمِرْتُ أَنْ أَكُونَ أَوَّلَ مَنْ أَسْلَمَ ۖ وَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْمُشْرِكِينَ ﴿١٤﴾

Sema: Je, nimfanye mlinzi asiyekuwa Allaah; Muanzilishi wa mbingu na ardhi, Naye Ndiye Anayelisha na wala halishwi? Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Hakika mimi nimeamrishwa niwe wa kwanza katika wenye kusilimu. Na wala usijekuwa kabisa miongoni mwa washirikina.  [Al-An’aam (6):14]

 

 

غَافِرُ الذَّنبِ

Mwenye Kughufuria Dhambi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

غَافِرِ الذَّنبِ وَقَابِلِ التَّوْبِ شَدِيدِ الْعِقَابِ ذِي الطَّوْلِ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ إِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Mwenye kughufuria dhambi, Anayepokea tawbah, Mkali wa kuakibu, Mwenye wingi wa Ukarimu, hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake ndio mahali pa kuishia.  [Ghaafir (40): 3]

 

 

 

 

إِلَـٰهِ النَّاسِ

Muabudiwa Wa Haki Wa Watu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

إِلَـٰهِ النَّاسِ ﴿٣﴾

Muabudiwa wa haki wa watu.  [An-Naas (114): 3]

 

 

 

 

خَيْرُ الْفَاصِلِينَ

Mbora Wa Wenye Kuamua Hukumu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ إِنِّي عَلَىٰ بَيِّنَةٍ مِّن رَّبِّي وَكَذَّبْتُم بِهِ ۚ مَا عِندِي مَا تَسْتَعْجِلُونَ بِهِ ۚ إِنِ الْحُكْمُ إِلَّا لِلَّـهِ ۖ يَقُصُّ الْحَقَّ ۖ وَهُوَ خَيْرُ الْفَاصِلِينَ ﴿٥٧﴾

Sema: Hakika mimi niko juu ya hoja bayana kutoka kwa Rabb wangu nanyi mumeikadhibisha. Sina yale mnayoyahimiza. Hakuna hukumu isipokuwa ya Allaah Pekee. Anasimulia ya haki; Naye ni Mbora wa wenye kuamua hukumu. [Al-An’aam (6): 57]

 

 

 

خَيْرُ الْفَاتِحِينَ

Mbora Wa Wenye Kuhukumu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَدِ افْتَرَيْنَا عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا إِنْ عُدْنَا فِي مِلَّتِكُم بَعْدَ إِذْ نَجَّانَا اللَّـهُ مِنْهَا ۚ وَمَا يَكُونُ لَنَا أَن نَّعُودَ فِيهَا إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ رَبُّنَا ۚ وَسِعَ رَبُّنَا كُلَّ شَيْءٍ عِلْمًا ۚ عَلَى اللَّـهِ تَوَكَّلْنَا ۚ رَبَّنَا افْتَحْ بَيْنَنَا وَبَيْنَ قَوْمِنَا بِالْحَقِّ وَأَنتَ خَيْرُ الْفَاتِحِينَ ﴿٨٩﴾

Kwa yakini itakuwa tumemtungia Allaah uongo ikiwa tutarudi katika millah yenu baada ya Allaah kutuokoa nayo. Na haiwi kwetu kurejea humo isipokuwa Akitaka Allaah Rabb wetu. Rabb wetu Amekienea kila kitu kwa ujuzi. Kwa Allaah tunatawakali. Rabb wetu! Hukumu baina yetu na baina ya kaumu yetu kwa haki, Nawe ni Mbora wa wenye kuhukumu. [Al-A’raaf (7): 89]

 

 

 

 

خَيْرُ الْغَافِرِينَ

Mbora Wa Wenye Kughufuria

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَاخْتَارَ مُوسَىٰ قَوْمَهُ سَبْعِينَ رَجُلًا لِّمِيقَاتِنَا ۖ فَلَمَّا أَخَذَتْهُمُ الرَّجْفَةُ قَالَ رَبِّ لَوْ شِئْتَ أَهْلَكْتَهُم مِّن قَبْلُ وَإِيَّايَ ۖ أَتُهْلِكُنَا بِمَا فَعَلَ السُّفَهَاءُ مِنَّا ۖ إِنْ هِيَ إِلَّا فِتْنَتُكَ تُضِلُّ بِهَا مَن تَشَاءُ وَتَهْدِي مَن تَشَاءُ ۖ أَنتَ وَلِيُّنَا فَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا ۖ وَأَنتَ خَيْرُ الْغَافِرِينَ ﴿١٥٥﴾

  Na Muwsaa akachagua wanaume sabini wa kaumu yake kwa ajili ya miadi Yetu kukutana kwa wakati na mahali. Kisha ilipowachukua tetemeko la ardhi; Muwsaa alisema: Rabb wangu! Ungelitaka Ungeliwaangamiza wao na mimi kabla. Je, Unatuangamiza kwa yale waliyoyafanya wapumbavu miongoni mwetu?  Haya si chochote isipokuwa ni majaribio Yako. Unampotoa kwayo Umtakaye, na Unamuongoa Umtakaye. Wewe ni Mlinzi wetu, basi Tughufurie na Turehemu; Nawe ni Mbora wa wenye kughufuria. [Al-A’raaf (7): 55]

 

 

 

 

خَيْرٌ حَافِظًا

Mbora Wa Wenye Kuhifadhi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ هَلْ آمَنُكُمْ عَلَيْهِ إِلَّا كَمَا أَمِنتُكُمْ عَلَىٰ أَخِيهِ مِن قَبْلُ ۖ فَاللَّـهُ خَيْرٌ حَافِظًا ۖ وَهُوَ أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ ﴿٦٤﴾

 Akasema: Je, nimwaminishe kwenu ila kama nilivyokuaminini juu ya kaka yake kabla? Basi Allaah ni Mbora wa wenye kuhifadhi. Naye ni Mbora zaidi wa kurehemu kuliko wengine wote wenye kurehemu. [Yusuf (2): 64]

 

 

خَيْرُ الْحَاكِمِينَ

Mbora Wa Wenye Kuhukumu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِن كَانَ طَائِفَةٌ مِّنكُمْ آمَنُوا بِالَّذِي أُرْسِلْتُ بِهِ وَطَائِفَةٌ لَّمْ يُؤْمِنُوا فَاصْبِرُوا حَتَّىٰ يَحْكُمَ اللَّـهُ بَيْنَنَا ۚ وَهُوَ خَيْرُ الْحَاكِمِينَ ﴿٨٧﴾

Na kama liko kundi miongoni mwenu limeamini kwa yale niliyotumwa nayo na kundi halikuamini; basi subirini mpaka Allaah Ahukumu baina yetu. Naye ni Mbora wa wenye kuhukumu. [Al-A’raaf (7): 87]

 

 

 

 

خَيْرُ الْمَاكِرِينَ

Mbora Wa Wenye Kupanga Makri (Njama)

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذْ يَمْكُرُ بِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِيُثْبِتُوكَ أَوْ يَقْتُلُوكَ أَوْ يُخْرِجُوكَ ۚ وَيَمْكُرُونَ وَيَمْكُرُ اللَّـهُ ۖ وَاللَّـهُ خَيْرُ الْمَاكِرِينَ﴿٣٠﴾

Na pindi (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) walipokupangia makri wale waliokufuru ili wakufunge, au wakuue, au wakutoe (Makkah). Na wanapanga makri, na Allaah Anapanga makri (kupindua njama zao), na Allaah ni Mbora wa wenye kupanga makri. [Al-Anfaal (8): 30]

 

 

 

 

خَيْرُ الْمُنزِلِينَ

Mbora Wa Wenye Kuteremsha (Ardhini)

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقُل رَّبِّ أَنزِلْنِي مُنزَلًا مُّبَارَكًا وَأَنتَ خَيْرُ الْمُنزِلِينَ ﴿٢٩﴾

Na sema: Rabb wangu! Niteremshe mteremko wa baraka, Nawe ni Mbora wa wenye kuteremsha. [Al-Mu-uminuwn (23): 29]

 

 

 

 

خَيْرُ النَّاصِرِينَ

Mbora Kabisa Wa Wenye Kunusuru

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

بَلِ اللَّـهُ مَوْلَاكُمْ ۖ وَهُوَ خَيْرُ النَّاصِرِينَ ﴿١٥٠﴾

Bali Allaah ndio Mlinzi na Msaidizi wenu. Naye ni Mbora kabisa wa wenye kunusuru. [Aali ‘Imraan (3): 150]

 

 

 

خَيْرُ الرَّاحِمِينَ

Mbora Wa Wenye Kurehemu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّهُ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْ عِبَادِي يَقُولُونَ رَبَّنَا آمَنَّا فَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الرَّاحِمِينَ ﴿١٠٩﴾

Hakika lilikuwa kundi miongoni mwa waja Wangu, wakisema: Rabb wetu! Tumeamini, basi Tughufurie na Uturehemu, Nawe ni Mbora wa wenye kurehemu. [Al-Mu-uminuwn (23): 109]

 

 

 

 

خَيْرُ الرَّازِقِينَ

Mbora Wa Wenye Kuruzuku

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ اللَّـهُمَّ رَبَّنَا أَنزِلْ عَلَيْنَا مَائِدَةً مِّنَ السَّمَاءِ تَكُونُ لَنَا عِيدًا لِّأَوَّلِنَا وَآخِرِنَا وَآيَةً مِّنكَ ۖ وَارْزُقْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الرَّازِقِينَ ﴿١١٤﴾

Akasema ‘Iysaa mwana wa Maryam: Ee Allaah, Rabb wetu, Tuteremshie meza iliyotandazwa chakula kutoka mbinguni ili iwe kwetu ni sikukuu kwa wa mwanzo wetu na wa mwisho wetu; na iwe Aayah (ishara, hoja) itokayo Kwako; basi Turuzuku; kwani Wewe ni Mbora wa wenye kuruzuku.  [Al-Maa-idah (5): 114]

 

 

خَيْرُ الْوَارِثِينَ

Mbora Wa Wenye Kurithi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَزَكَرِيَّا إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ رَبِّ لَا تَذَرْنِي فَرْدًا وَأَنتَ خَيْرُ الْوَارِثِينَ ﴿٨٩﴾

Na Zakariyyaa alipomwita Rabb wake: Rabb wangu! Usiniache pekee; Nawe Ndiye Mbora wa wenye kurithi.  [Al-Anbiyaa (21): 89]

 

 

 

 

الْمَلِكُ الْحَقُّ

Mfalme Wa Haki

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَتَعَالَى اللَّـهُ الْمَلِكُ الْحَقُّ ۗ وَلَا تَعْجَلْ بِالْقُرْآنِ مِن قَبْلِ أَن يُقْضَىٰ إِلَيْكَ وَحْيُهُ ۖ وَقُل رَّبِّ زِدْنِي عِلْمًا ﴿١١٤﴾

 Basi Ametukuka Allaah kwa ‘Uluwa, Mfalme wa haki. Na wala usiiharakize Qur-aan (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kabla haikumalizwa kufunuliwa Wahy kwako. Na sema: Rabb wangu! Nizidishie elimu. [Twaa Haa (20): 114]

 

 

 

 

مَالِكُ الْمُلْكِ

Mfalme Anayemiliki Ufalme Wote

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَاءُ ۖ بِيَدِكَ الْخَيْرُ ۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢٦﴾

Sema: Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, Unampa ufalme Umtakaye, na Unamuondoshea ufalme Umtakaye, na Unamtukuza Umtakaye, na Unamdhalilisha Umtakaye, khayr imo Mkononi Mwako.  Hakika Wewe juu ya kila kitu ni Muweza. [Aali ‘Imraan (3): 26]

 

 

مَلِكِ النَّاسِ

Mfalme Wa Watu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَلِكِ النَّاسِ ﴿٢﴾

Mfalme wa watu. [An-Naas (114): 2]

 

 

 

 

مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ

Mfalme Wa Siku Ya Malipo

 

 

 

 Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ ﴿٤﴾

Mfalme wa siku ya malipo. [Al-Faatihah (1): 4]

 

 

 

 

نُورُ السَّمَاوَاتِ

Nuru Ya Mbingu Na Ardhi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اللَّـهُ نُورُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَاةٍ فِيهَا مِصْبَاحٌ ۖ الْمِصْبَاحُ فِي زُجَاجَةٍ ۖ الزُّجَاجَةُ كَأَنَّهَا كَوْكَبٌ دُرِّيٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ مُّبَارَكَةٍ زَيْتُونَةٍ لَّا شَرْقِيَّةٍ وَلَا غَرْبِيَّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِيءُ وَلَوْ لَمْ تَمْسَسْهُ نَارٌ ۚ نُّورٌ عَلَىٰ نُورٍ ۗ يَهْدِي اللَّـهُ لِنُورِهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَيَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣٥﴾

Allaah ni Nuru ya mbingu na ardhi. Mfano wa Nuru Yake kama shubaka ndani yake mna taa yenye mwanga mkali. Taa hiyo yenye mwanga mkali iko katika (tungi la) gilasi. Gilasi hiyo ni kama kwamba nyota inayong’aa na kumeremeta, inawashwa kutokana na mti wa baraka wa zaytuni, hauko Mashariki wala Magharibi. Yanakaribia mafuta yake yang’ae japokuwa moto haujayagusa; Nuru juu ya Nuru. Allaah Anamwongoza kwa Nuru Yake Amtakaye. Na Allaah Anapiga mifano kwa watu. Na Allaah kwa kila kitu ni Mjuzi.  [An-Nuwr (24): 35]

 

 

 

 

قَابِلِ التَّوْبِ

Anayepokea Tawbah

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

غَافِرِ الذَّنبِ وَقَابِلِ التَّوْبِ شَدِيدِ الْعِقَابِ ذِي الطَّوْلِ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ إِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Mwenye kughufuria dhambi, Anayepokea tawbah, Mkali wa kuakibu, Mwenye wingi wa Ukarimu, hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake ndio mahali pa kuishia. [Ghaafir (40): 3]

 

 

 

 

رَبُّ الْعَالَمِينَ

Rabb Wa Walimwengu.

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِذْ قَالَ لَهُ رَبُّهُ أَسْلِمْ ۖ قَالَ أَسْلَمْتُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٣١﴾

Rabb wake Alipomwambia: Jisalimishe na utii (Ibraahiym) Akasema: Nimejisalimisha na kutii kwa Rabb wa walimwengu. [Al-Baqarah (2): 131]

 

 

 

رَبُّ الْعَرْشِ

Rabb Wa ‘Arsh

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِن تَوَلَّوْا فَقُلْ حَسْبِيَ اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ ۖ وَهُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ﴿١٢٩﴾

Na wakikengeuka, basi sema: Amenitosheleza Allaah; Hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye. Kwake nimetawakali. Naye ni Rabb wa ‘Arsh adhimu. [At-Tawbah (9): 129]

 

 

رَبُّ الْفَلَقِ

Rabb Wa Mapambazuko

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾

Sema: Najikinga na Rabb wa mapambazuko. [Al-Falaq (113): 1]

 

 

 

رَبّ هَـٰذَا الْبَيْتِ

Rabb Wa Nyumba Hii (Al-Ka’bah)

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَلْيَعْبُدُوا رَبَّ هَـٰذَا الْبَيْتِ ﴿٣﴾

Basi wamuabudu Rabb wa nyumba hii (Ka’bah).  [Quraysh (106): 3]

 

 

 

 

رَبُّ كُلِّ شَيْءٍ ۚ

Rabb Wa Kila Kitu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ أَغَيْرَ اللَّـهِ أَبْغِي رَبًّا وَهُوَ رَبُّ كُلِّ شَيْءٍ ۚ وَلَا تَكْسِبُ كُلُّ نَفْسٍ إِلَّا عَلَيْهَا ۚ وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ ۚ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُم مَّرْجِعُكُمْ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ فِيهِ تَخْتَلِفُونَ ﴿١٦٤﴾

Sema Je, nitake ghairi ya Allaah kuwa ni Rabb na hali Yeye ni Rabb wa kila kitu? Na wala nafsi yoyote haitochuma (khayr au shari) ila ni juu yake. Na wala habebi mbebaji, mzigo (wa dhambi) wa mwengine. Kisha kwa Rabb wenu ndio marejeo yenu, Atakujulisheni kwa yale mliyokuwa mkikhitilafiana nayo.  [Al-An’aam (6): 164]

 

 

 

 

رَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ

Rabb Wa Magharibi Mbili

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ ﴿١٧﴾

Rabb wa Mashariki mbili na Rabb wa Magharibi mbili. [Ar-Rahman (55): 17]

 

 

 

رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ

Rabb Wa Mashariki Mbili

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ ﴿١٧﴾

Rabb wa Mashariki mbili na Rabb wa Magharibi mbili. [Ar-Rahman (55): 17]

 

 

 

 

رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ

Rabb Wa Mashariki Na Magharibi

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ ﴿٢٨﴾

 (Muwsaa) Akasema: Rabb wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, mkiwa nyinyi ni wenye kutia akilini. [Ash-Shu’araa (26): 28]

 

 

 

 

رَبُّ النَّاسِ

Rabb Wa Watu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ﴿١﴾

Sema: Najikinga na Rabb wa watu.  [An-Naas (114): 1]

 

 

 

 

رَبُّ الْعِزَّةِ

Rabb Mtukufu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ ﴿١٨٠﴾

Subhaana Rabbika! Utakasifu ni wa Rabb wako, Rabb Mtukufu kutokana na yale wanayoyavumisha. [Asw-Swaffaat (37): 180]

 

 

 

 

رَّبُّ السَّمَاوَاتِ السَّبْعِ

Rabb Wa Mbingu Saba

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ السَّبْعِ وَرَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ ﴿٨٦﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Nani Rabb wa mbingu saba, na Rabb wa ‘Arsh adhimu[Al-Mu-umin (23): 86]

 

 

 

 

رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ

Rabb Wa Mbingu Na Ardhi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ ۚ قُلْ أَفَاتَّخَذْتُم مِّن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ لَا يَمْلِكُونَ لِأَنفُسِهِمْ نَفْعًا وَلَا ضَرًّا ۚ قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الْأَعْمَىٰ وَالْبَصِيرُ أَمْ هَلْ تَسْتَوِي الظُّلُمَاتُ وَالنُّورُ ۗ أَمْ جَعَلُوا لِلَّـهِ شُرَكَاءَ خَلَقُوا كَخَلْقِهِ فَتَشَابَهَ الْخَلْقُ عَلَيْهِمْ ۚ قُلِ اللَّـهُ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ وَهُوَ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿١٦﴾

Sema: Ni nani Rabb wa mbingu na ardhi? Sema: Ni Allaah. Sema: Je, mnawafanya wengineo badala Yake kuwa walinzi na hali hawamiliki kwa ajili ya nafsi zao manufaa wala dhara? Sema: Je, kipofu analingana sawa na mwenye kuona, au je, viza vinalingana sawa na nuru? Au wamemfanyia Allaah washirika walioumba kama uumbaji Wake, kisha yakafanana maumbile kwao?  Sema: Allaah ni Muumbaji wa kila kitu, Naye ni Mmoja Pekee, Asiyepingika. [Ar-Ra’d (13): 16]

 

 

 

 

رَبُّ الشِّعْرَىٰ

Rabb Wa Nyota Ya Ash-Shi’-raa

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأَنَّهُ هُوَ رَبُّ الشِّعْرَىٰ ﴿٤٩﴾

Na kwamba Yeye ndiye Rabb wa nyota ya Ash-Shi’-raa (inayoabudiwa). [An-NAjm (53): 49]

 

 

 

 

رَفِيعُ الدَّرَجَاتِ

Mwenye Uluwa Juu Ya Vyeo Na Daraja

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

رَفِيعُ الدَّرَجَاتِ ذُو الْعَرْشِ يُلْقِي الرُّوحَ مِنْ أَمْرِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ لِيُنذِرَ يَوْمَ التَّلَاقِ﴿١٥﴾

 (Allaah) Mwenye uluwa juu ya vyeo na daraja. Mwenye ‘Arsh, Anapelekea Ar-Ruwh (Wahy) kwa amri Yake kwa Amtakaye miongoni mwa waja Wake, ili aonye Siku ya kukutana. [Ghaafir (40): 15]

 

 

 

 

سَرِيعُ الْحِسَابِ

Mwepesi Wa Kuhesabu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّ الدِّينَ عِندَ اللَّـهِ الْإِسْلَامُ ۗ وَمَا اخْتَلَفَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْعِلْمُ بَغْيًا بَيْنَهُمْ ۗ وَمَن يَكْفُرْ بِآيَاتِ اللَّـهِ فَإِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴿١٩﴾

Hakika Dini mbele ya Allaah ni Uislamu. Na hawakukhitilafiana wale waliopewa Kitabu ila baada ya kuwajia elimu kwa kufanyiana baghi na uhusuda baina yao. Na atakayekanusha Aayaat za Allaah basi hakika Allaah ni Mwepesi wa kuhesabu. [Aali ‘Imraan (3): 19]

 

 

 

شَدِيدُ الْعَذَابِ

Mkali Wa Kuadhibu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ۖ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ ۗ وَلَوْ يَرَى الَّذِينَ ظَلَمُوا إِذْ يَرَوْنَ الْعَذَابَ أَنَّ الْقُوَّةَ لِلَّـهِ جَمِيعًا وَأَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعَذَابِ ﴿١٦٥﴾

Na miongoni mwa watu wako wenye kuchukua asiyekuwa Allaah na kuwafanya kuwa ni wanaolingana (na Allaah) wanawapenda kama kumpenda Allaah. Na wale walioamini wana mapenzi zaidi kwa Allaah. Na lau wangelitambua wale waliodhulumu watakapoona adhabu kwamba nguvu zote ni za Allaah; na kwamba hakika Allaah ni Mkali wa kuadhibu.  [Al-Baqarah (2): 165]

 

 

شَدِيدُ الْعِقَابِ

Mkali Wa Kuakibu (Kuadhibu)

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

غَافِرِ الذَّنبِ وَقَابِلِ التَّوْبِ شَدِيدِ الْعِقَابِ ذِي الطَّوْلِ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ إِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Mwenye kughufuria dhambi, Anayepokea tawbah, Mkali wa kuakibu, Mwenye wingi wa Ukarimu, hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake ndio mahali pa kuishia. [Ghaafir (40): 3]

 

 

 

 

سَرِيعُ الْعِقَابِ

Mwepesi wa kuakibu (kuadhibu)

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَهُوَ الَّذِي جَعَلَكُمْ خَلَائِفَ الْأَرْضِ وَرَفَعَ بَعْضَكُمْ فَوْقَ بَعْضٍ دَرَجَاتٍ لِّيَبْلُوَكُمْ فِي مَا آتَاكُمْ ۗ إِنَّ رَبَّكَ سَرِيعُ الْعِقَابِ وَإِنَّهُ لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٦٥﴾

Naye (Allaah) Ndiye Aliyekufanyeni makhalifa wa duniani na Akanyanyua baadhi yenu juu ya wengine daraja mbali mbali ili Akujaribuni katika yale Aliyokupeni. Hakika Rabb wako ni Mwepesi wa kuakibu, na hakika Yeye bila shaka ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.  [Al-An’aam (6): 165]

 

 

 

شَدِيدُ الْمِحَالِ

Mkali Na Mwenye Nguvu Za Kuhujumu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَيُسَبِّحُ الرَّعْدُ بِحَمْدِهِ وَالْمَلَائِكَةُ مِنْ خِيفَتِهِ وَيُرْسِلُ الصَّوَاعِقَ فَيُصِيبُ بِهَا مَن يَشَاءُ وَهُمْ يُجَادِلُونَ فِي اللَّـهِ وَهُوَ شَدِيدُ الْمِحَالِ ﴿١٣﴾

Na radi inamsabihi (Allaah) kwa Himidi Zake na Malaika pia kwa kumkhofu, na Anatuma mingurumo ya radi, humsibu kwayo Amtakaye nao huku (makafiri) wakiwa wanabishana kuhusu Allaah Naye ni Mkali na Mwenye nguvu za kuhujumu. [Ar-Ra’d (13): 13]

 

 

 

سَمِيعُ الدُّعَاء

Mwenye Kusikia Du’aa

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُ ۖ قَالَ رَبِّ هَبْ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةً طَيِّبَةً ۖ إِنَّكَ سَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٨﴾

Hapo hapo Zakariyyaa akamwomba Rabb wake, akasema: Rabb wangu Nitunukie kutoka Kwako kizazi chema hakika Wewe ni Mwenye kusikia du’aa yangu.  [Aali ‘Imraan (3): 38]

 

 

 

وَاسِعُ الْمَغْفِرَةِ

Mkunjufu Wa Kughufuria

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَائِرَ الْإِثْمِ وَالْفَوَاحِشَ إِلَّا اللَّمَمَ ۚ إِنَّ رَبَّكَ وَاسِعُ الْمَغْفِرَةِ ۚ هُوَ أَعْلَمُ بِكُمْ إِذْ أَنشَأَكُم مِّنَ الْأَرْضِ وَإِذْ أَنتُمْ أَجِنَّةٌ فِي بُطُونِ أُمَّهَاتِكُمْ ۖ فَلَا تُزَكُّوا أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اتَّقَىٰ ﴿٣٢﴾

Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. Hakika Rabb wako ni Mkunjufu wa kughufuria. Yeye Anakujueni vyema, tangu Alipokuanzisheni kutoka katika ardhi, na pale mlipokuwa mimba changa matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa. [An-Najm (53): 32]

 

 

 

 

مُحْيِي الْمَوْتَى

Mwenye Kuhuisha Wafu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَانظُرْ إِلَىٰ آثَارِ رَحْمَتِ اللَّـهِ كَيْفَ يُحْيِي الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا ۚ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمُحْيِي الْمَوْتَىٰ ۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٥٠﴾

Basi tazama athari za rahmah ya Allaah vipi Anaihuisha ardhi baada ya kufa kwake. Hakika (Afanyayo) hayo, Ndiye bila shaka Mwenye Kuhuisha wafu, Naye juu ya kila kitu ni Muweza.  [Rum (30): 50]

 

 

 

 

4-Onyo Dhidi Ya Tafsiri Ya Majina Na Sifa Za Allaah Kwa Namna Ya Kitamathali

 

 

Imaam ‘Aliy bin Al-Murtadhwaa Al-Yamaaniy amesema: n

 

“… Jambo la pili ni kuilaumu Dini kuwa ina ila kwa kukataa vitabu na kueleza Sifa nje nje (dhwawaahir), na kuziondoa mbali na maana zake uhakika na halisi na kuzifanya kitamathili pasi na ushahidi wa wazi na  wa kauli moja ambao ungeonyesha ulazima wa taawiyl (taawili: kuipa maana ndogo, kugeuza maana halisi)). Katika hili, wanaofanya haya wanafuata Ahlul-Kalaam (watu wa balagha na kimantiki) kibubusa tu katika kanuni ambazo wao wenyewe hawajaafikiana. Baya kabisa katika haya ni madh-hab ya Qaraamitwah, Baatwiniyyah, katika taawiyl ya Majina Mazuri ya Allaah na ukanushaji wao chini ya kisingizio cha kumwepusha Allaah dhidi ya za Sifa za zinazowahusu wanaadamu tu na hivyo kuishadidisha au kuithibitsha tawhiyd machoni mwao, kwa madai ya kuyatumia Majina hayo kwa Allaah kuwa ni tashbiyh (kushabihi na wanaadamu). Haya yalifikia hatua ya kusema kuwa Yeye Hayupo, Hapatikani na Hana Sifa ya kutokuwepo au kukosekana…”

 

 

Kutokana na masuala muhimu ya Dini hii ni kuchukua Majina Mazuri ya Allaah yaliyotajwa katika Kitabu Chake kwa njia ya kumtukuza na kumsifu Yeye. Huoni kwa mfano, Ar-Rahmaan na Ar-Rahiym, husomwa katika kila Swalaah na kutajwa katika kila mjumuiko wa Kiislamu, wote wakiwa wameafikiana kuwa Majina haya mawili ni katika namna bora zaidi za kumsifu Allaah (عز وجل), na kujiweka karibu Naye kwa njia ya kumtukuza kwa majina hayo…?

 

 

Hivyo ni nini cha kuzuia kuthibitisha Sifa ya Rahmah na mfano wake zilizothibitishwa na Allaah na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) katika namna ile ile, ikiambatanishwa na kukanusha mapungufu yaliyohusiana na sifa za viumbe? Kuna kitu gani chenye kuweza kuzuia kufanywa namna kama hiyo kwa kila sifa ya Rabb ambayo pia viumbe wanayo? Yeye (سبحانه وتعالى) Amesifika nazo katika hali ya ukamilifu mkubwa zaidi, zimeondolewa namna yoyote ya ila, ilhali mja anasifika nazo huku kukiwa na ila na udhaifu. Ni katika hali hii ndipo Ahlus-Sunnah wameelewa ukanushaji wa tashbiyh, si kwa kukanusha Sifa kama wafanyavyo wenye kukanusha Sifa Zake (Mu‘atwilah).

 

 

Kutoka katika masuala yanayoashiria kutokuwa na maana taawiyl (taawili: kuipa maana ndogo, kugeuza maana halisi)), ni kuwa Mu’tazilah hawapendi ta’wiyl ambazo kundi la  Ash‘ariy wanazotoa za Mwenye Hikma wa Yote Daima (Al-Hakiym). Kundi la Ash‘ariy hawapendi ta’wiyl ambazo baadhi ya Mu’tazilah hutoa za Mwenye Kusikia Yote Daima (As-Sami’) na Mwenye Kuona Yote Daima (Al-Baswiyr). Ahlus-Sunnah hawapendi taawiyl kuwa makundi yote mawili hufanya Ar-Rahmaan, Ar-Rahiym na mfano wao. Makundi yote haya hayapendi taawiyl zilizotolewa na Qaraamitwah. Hivyo ni wajibu kukazia Alichokithibitisha Allaah (عز وجل) kwa Nafsi Yake Tukufu pasi na taawiyl (kuipa maana ndogo, kugeuza maana halisi) na ta’twiyl (kuzipinga, kukanusha uwezekano).

 

 

Rai kuwa kuthibitisha maana halisi ya Majina haya ni kufuru na upotovu, kuwa Swahaba na Salaf wema hawakufahamu maana zake, au kuwa walifahamu lakini hawakubeba jukumu la kuwashauri watu juu ya maana zake halisi, haiwezekani kwa sababu ya mambo mawili:

 

 

i-Hoja muhimu na ya kauli moja kuwa asili ya mwanadamu inaeleza kuwa kila jambo la aina hii kama lingekuwa na tahadhari dhidi yake kutokea kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na Swahaba wake, na lingekuwa lenye kujirudiarudia na kubwa sana kuliko tahadhari dhidi ya mwongo Dajjaal. Hilo haliwezekani kwasababu ya akili zao timamu na Dini kamilifu kuwa vipi waweze kuwaacha vizazi vyao, wake zao na jamii kwa ujumla wasikilize jambo lililohusika na Allaah ambalo maana yake halisi ni kufuru, na wakalinyamazia? Kama wangeacha tahadhari hii, kwa hakika wao wangeacha tahadhari dhidi ya Dajjaal, kwa ajili ya kutangua ubwana wake ni jambo kubwa na kalifu zaidi kiakili.

 

 

Huoni kuwa pale wale waliopewa Balagha ya Kimadhehebu (Mutakallimiyn) walipoamini mgongano wa maana halisi ya maandiko haya, tahadhari zao dhidi yake zilikuja kuwa mara nyingi kama zilivyofanya taawiyl zao kwa ajili yake? Waliandika majalada mengi kuhusu hili, waliamsha uzembe wao, walifundisha ujinga, walitangaza kufuru ya waliowapinga, na walilieneza hilo baina ya Waislamu, bali ulimwengu mzima. Hata hivyo, hili lingekuwa na haki zaidi kwa (صلى الله عليه وآله وسلم) ambaye ni Sayyid wa Manabii, Mtangulizi wa Salaf na wasaidizi wa Dini, kama madai yao kweli yalikuwa sahihi.

 

 

ii-Imethibitika kuwa nyongeza yoyote katika Dini imeharamishwa, hivyo si sahihi kuwa Shariy’ah iwe kimya kuhusu jambo linalotakiwa kutoka katika andiko linalotokana na misingi ya Dini. Uislamu unapaswa ufuatwe, sio uwe wa kubuni na hii ndiyo sababu unatangaza kuwa yeyote anayekana nguzo za Dini kuwa ni kafiri kwa sababu zinajulikana kwa umuhimu. Kwa hivyo, inastahiki na kufaa zaidi kuwa Shairy’ah haikuleta jambo lenye kurudiwarudiwa, kusomwa kijuujuu kuwa ni batili, lakini bila kututahadharisha nalo, hususan pindi liliposikika kuwa ni batili na linajulikana katika Vitabu vya Allaah (سبحانه وتعالى). Kwa kuhitimisha, hakuna kitukiacho kinachoweza kupingana na maana halisi ya maandiko kwa njia ya Shariy’ah au akili na hivyo kulazimika taawiyl.

 

 

Ar-Raaziy alithibitisha katika kitabu chake, Al-Arba‘iyn, naye ni alikuwa katika wapinzani wakubwa wa Ahlus-Sunnah,  kuwa Vitabu vyote vya Kimbinguni vimekuja na utajo wa Sifa za Allaah, na Allaah Hakutaja andiko hata moja kuwa  inatakiwa Yeye Aondolewe na Sifa ya Rahmah, Kuvumilia, Hikma na mfano wake. Hivyo suala hili liko dhahiri ingawa anaweza kukataa.[4]

 

 

 

5-Wasifu Wa ‘Allaamah Abu ‘Abdirrahmaan Naaswir As-Sa’diy (رحمه الله)

 

 

Jina lake ni Abu ‘Abdillaah ‘Abdurrahman bin Naaswir bin ‘Abdillaah bin Naaswir ‘Aliy As-Sa’diy wa kabila la Tamiymiy. Alizaliwa katika jiji la ‘Unayzah, Qasiym mnamo tarehe 12 Muharram, 1307 H. Mama yake alifariki wakati yeye alipokuwa na umri wa miaka mine na baba yake alifariki dunia wakati yeye alipofikisha miaka saba. Hivyo, alikua kama yatima lakini licha ya haya alikuwa na makuzi mema.

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) alikuwa na akili sana na alihifadhi Qur-aan alipokuwa na umri wa miaka kumi na mmoja na baada ya hapo alitumia muda mwingi akisoma kwa ‘Ulamaa wa nchini mwake. Alijibidiisha masomoni mwake mpaka akafanya vyema katika aina mbalimbali za sayansi ya Kiislamu na alipofikisha umri wa miaka ishirini na mitatu alikuwa tayari akifundisha. Alijitolea kwa hali zote kwa kujifunza na kufundisha mpaka akawa na mamlaka inayoongoza nchini mwake, akiwa pamoja na wanafunzi waliojazana kwake kutoka maeneo yote.

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) alisoma chini ya ‘Ulamaa waliokuwa wakiongoza katika wakati wake, miongoni mwao alikuwa Shaykh Ibraahiym bin Hamad bin Jaasir; ambaye  Imaam As-Sa’dy alimsifu kuhusu uwezo wake wa juu ya kuhifadhi Hadiyth, taqwa yake na mapenzi yake kwa masikini. Mara nyingi alishuhudia masikini akija kwa Shaykh Ibraahiym naye Shaykh akitoa nguo na kumpa, licha ya yeye mwenyewe kuwa na haja nacho na akiwa masikini hasa.

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله)  alisoma pia chini ya Shaykh Muhammad bin ‘Abdilkariym ash-Shibl, Shaykh Swaalih bin ‘Uthmaan, Hakimu wa ‘Unayzah, Shaykh bin Sa’b Al-Quwayjiriy, Muhammad Al-Amiyn Ash-Shanqiytwiy na wengine.

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) alijulikana kwa taqwa yake wake, maadili mema na unyenyekevu kwa wadogo, wakubwa, matajiri na masikini. Kila mara alikuwa akipitisha sehemu ya muda wake kukutana na wale waliotaka wakutane naye na alikuwa mkarimu kwa masikini, mayatima na wageni, akiwasaidia kwa kadiri ya uwezo wake.

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) alibobea katika Fiqhi na Uswuw Al-Fiqhi, hatimaye akawa katika madhehebu ya Hanbal kama walivyokuwa walimu wake wote. 

 

 

Kazi yake ya kwanza katika Fiqhi iliandikwa kwa mtindo wa kimashairi juu ya madhehebu ya Hanbal ambayo ndiyo pia ilikuwa rai yake. Alisoma kazi ya Ibn Taymiyyah na Ibn Al-Qayyim kwa undani na akanufaika kutokana nao. Alipoendelea na masomo yake hakujifunga sana na madhehebu ya Hanbal bali alifuata njia aliyoamini kuwa ilihakikishiwa ushahidi uliokuwa na nguvu zaidi. Hata hivo, kamwe hakuweza kuwalaumu au kuwadharau wale waliofuata madhehebu fulani. Kadhalika alikuwa bingwa katika Tafsiyr, akiwa amesoma kazi nyingi za Tafsiyr na akiwa ameisoma chini ya walimu wake na kwa kweli alihariri Tafsiyr yeye mwenyewe. Wote waliomsikia akikisherehi Kitabu cha Allaah walitamani aendelee kutokana na uzungumzaji wake wa namna ya kushajiisha na faida nyingi alizozipata kutoka katika Aayah za Qur-aan.

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) alihariri kazi nyingi na miongoni mwake ni zifuatazo:

 

·        تفسير السعدي = تيسير الكريم الرحمن في تفسير كلام المنان

 

·        إرشاد أولى البصائر والألباب لنيل الفقة بأقرب الطرق وأيسر الأسباب

 

·        الدرة البهية شرح القصيدة التائية في حل المشكلة القدرية

 

·        القول السديد شرح كتاب التوحيد 

 

·        التوضيح والبيان لشجرة الإيمان

 

·        القواعد الحسان لتفسير القرآن

 

·        الوسائل المفيدة للحياة السعيدة

 

·        التنبيهات اللطيفة على ما احتوت عليه العقيدة الواسطية من المباحث المنيفة

 

·        رسالة لطيفة جامعة في أصول الفقه المهمة

 

·        بهجة قلوب الأبرار وقرة عيون الأخيار

 

·        تفسير أسماء الله الحسنى

 

·        منهج السالكين وتوضيح الفقة في الدين

 

·        الفواكه الشهية في الخطب المنبرية والخطب المنبرية على المناسبات

 

·        تيسير اللطيف المنان في خلاصة تفسير القرآن

 

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) alifariki hapo ‘Unayzah mnamo mwaka 1376 H Allaah Amrehemu na Amjaalie makazi ya Jannatul-Firdaws. Aamiyn.

 

 

 

 

6-Sharh Ya Majina Mazuri Na Kamilifu Ya Allaah Na Swiffah Zake

 

 

Idadi kubwa ya Majina Mazuri na Kamilifu ya Allaah (عز وجل)  yamerudiwarudiwa mara kadhaa katika Qur-aan kama matukio yalivyohitaji, na kuna ulazima wa kuelezea maana zake kwa ufupi na ya kufahamika. Hivyo tunasema:

 

 

 

 

الرّب

Ar-Rabb:

 

Rabb Wa Kila Kitu, Mlezi, Mola, Bwana, Muumbaji, Msimamizi, Mneemeshaji, Mfalme, Mwenye Kuruzuku, Mwendeshaji wa Mambo

 

 

 

Jina hili limerudiwarudiwa katika Aayah nyingi.

 

Allaah (سبحانه وتعالى) – Ni Ar-Rabb Ambaye Anayelea na kukimu waja Wake kwa kuendesha na kusimamia mambo yao yote na kuwapa namna zote za fadhila na baraka. Hususan kabisa, Yeye Ndiye Anayelea na kukimu marafiki wa waja wanyoofu kwa kusahihisha na kutakasa nyoyo, roho na maadili yao. Kwa ajili hii, du’aa zao mara kwa mara huombwa kwa Jina hili tukufu kwasababu wanatafuta malezi haya hasa.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَرَبُّكَ الْغَفُورُ ذُو الرَّحْمَةِ ۖ لَوْ يُؤَاخِذُهُم بِمَا كَسَبُوا لَعَجَّلَ لَهُمُ الْعَذَابَ ۚ بَل لَّهُم مَّوْعِدٌ لَّن يَجِدُوا مِن دُونِهِ مَوْئِلًا ﴿٥٨﴾

Na Rabb wako ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye Rahmah. Kama Angeliwachukulia kwa yale waliyoyachuma, Angeliwaharakizia adhabu. Bali wao wana miadi, hawatopata pasi Naye kimbilio la kuepukana nayo. [Al-Kahf (18): 58]

 

 

 

 

الله

Allaah

Mwenye Uluwhiyyah, Mwenye ‘Ubuwdiyyah

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Ilaah Mmoja Pekee Ambaye Ndiye Anayeabudiwa na Ndiye mwenye haki ya kuabudiwa na viumbe wake wote. Hayo ni kwasababu ya sifa nzuri na kamilifu za Ki Ilaah Alizo Nazo Yeye:

 

 Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ ۚ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۖ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا ۚ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٢٥٥﴾

Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, Aliyehai daima, Msimamia kila kitu. Haumchukui usingizi wala kulala. Ni Vyake pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Nani huyu ambaye anashufai mbele Yake bila ya idhini Yake. Anajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Wala hawawezi kufikia kuelewa chochote kuhusu ujuzi Wake isipokuwa kwa Alitakalo. Imeenea Kursiyy Yake mbingu na ardhi. Wala hakumchoshi kuvihifadhi viwili hivyo. Naye ni Mwenye Uluwa; Ametukuka, Adhimu; Mkuu kabisa. [Al-Baqarah (2): 255]

 

 

 

الْمَلِكُ

Al-Malik

Mfalme

 

 

 

الْمَالِكُ

Al-Maalik

Mwenye Kumiliki

 

 

 

الَّذِي لَهُ الْمُلْكُ

Alladhi Lahul-Mulk

Ambaye Ufalme Ni Wake

 

 

 

Allaah (عز وجل) Amesifika Sifa ya kuwa ni Mfalme, Mmiliki. Hizi ni Sifa zinazoeleza Utukufu, ‘Uluwa Zake na Usimamizi Wake na utaratibu wa mambo. Allaah (سبحانه وتعالى) Yeye Ndiye Pekee Anayeelekeza mambo yote ya uumbaji, amri na jaza. Ni Wake Yeye uumbaji wote, viumbe wote ni watiifu Kwake. Anaumiliki uumbaji nao unaendelea na utaendelea kuwa na haja Kwake.

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَتَعَالَى اللَّـهُ الْمَلِكُ الْحَقُّ ۗ وَلَا تَعْجَلْ بِالْقُرْآنِ مِن قَبْلِ أَن يُقْضَىٰ إِلَيْكَ وَحْيُهُ ۖ وَقُل رَّبِّ زِدْنِي عِلْمًا ﴿١١٤﴾

Basi Ametukuka Allaah kwa ‘Uluwa, Mfalme wa haki. Na wala usiiharakize Qur-aan (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kabla haikumalizwa kufunuliwa Wahy kwako. Na sema: Rabb wangu! Nizidishie elimu. [Twahaa (20):114)]

 

 

Na Anasema pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَاءُ ۖ بِيَدِكَ الْخَيْرُ ۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢٦﴾

Sema: Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, Unampa ufalme Umtakaye, na Unamuondoshea ufalme Umtakaye, na Unamtukuza Umtakaye, na Unamdhalilisha Umtakaye, khayr imo Mkononi Mwako.  Hakika Wewe juu ya kila kitu ni Muweza.

 

 تُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَتُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ ۖ وَتُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَتُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ ۖ وَتَرْزُقُ مَن تَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿٢٧﴾

Unauingiza usiku katika mchana na Unauingiza mchana katika usiku; na Unatoa kilicho hai kutokana na kilicho mfu na Unatoa kilicho mfu kutokana na kilicho hai na Unamruzuku Umtakaye bila ya hesabu. [Aal-‘Imraan  (3): 26, 27]

 

Na Anasema pia (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِۚ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ ﴿٩﴾

Ambaye Pekee Ana ufalme wa mbingu na ardhi; na Allaah juu ya kila kitu ni Shahidi. [Al-Buruwj (85): 9]

 

 

 

 

الْواحِدُ

Al-Waahid

Mmoja Pekee Asiye Na Mfano

 

 

 

الأَحَدُ

Al-Ahad

Mpweke Asiye Na Mshirika

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Yeye Ndiye Mmoja wa Pekee katika vipengele vyote vya ukamilifu kiasi kwamba hakuna chochote chenye kushirikiana Naye katika hayo. Ni jambo la lazima kwa waja kumpwekesha Yeye Peke Yake katika iymaan, maneno na matendo kwa kutambua ukamilifu Wake usio na mipaka, Tawhiyd Yake na kumpwekesha katika namna zote za ‘ibaadah.

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu Nabiy Yuwsuf aliposema:

 

يَا صَاحِبَيِ السِّجْنِ أَأَرْبَابٌ مُّتَفَرِّقُونَ خَيْرٌ أَمِ اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ﴿٣٩﴾

Enyi masahibu wangu wawili wa jela. Je, miola wengi wanaofarakana ni bora au Allaah Mmoja Pekee, Asiyepingika? [Yuwsuf (12): 39]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾

Sema: Yeye ni Allaah Mmoja Pekee[Al-Ikhlaas (112): 1]

 

 

 

 

الصَّمَدُ

As-Swamad:

Mwenye Kukusudiwa Kwa Haja Zote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Yeye Ndiye Pekee Ambaye viumbe wote wanamtegemea kwa mahitaji yao yote; dhiki zao, mtihani, balaa na mashaka yao, na mahitaji yao yote mengineyo. Haya ni kutokana na ukamilifu Wake usio na mipaka wa Nafsi, Majina, Sifa na Matendo Yake.

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾

Sema: Yeye ni Allaah Mmoja Pekee. 

 

اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾

Allaah ni Aliyekamilika sifa za utukufu Wake, Mkusudiwa haja zote.  [Al-Ikhlaasw (112): 1-2)]

 

 

الْعَلِيمُ

Al-‘Aliym

Mjuzi Wa Yote Daima

 

 

الْخَبِيرُ

Al-Khabiyr

Mjuzi Wa Undani Na Kina Cha Mambo,

Mwenye Ujuzi Wa Ya Dhahiri Na Ya Siri

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Yeye Ndiye Ambaye elimu Yake inazunguka mambo yote ya dhahiri na yaliyojificha, ya wazi na ya siri, mambo yote yanayolazimika kutukia, mambo yasiyowezekana kutukia na mambo ambayo huenda yakatukia. Anayajua mambo ya viumbe wote, yaliyopita, ya sasa na ya baadaye. Kwa hakika, hakuna kilichofichikana dhidi Yake.

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ عِندَهُ عِلْمُ السَّاعَةِ وَيُنَزِّلُ الْغَيْثَ وَيَعْلَمُ مَا فِي الْأَرْحَامِ ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤﴾

Hakika Allaah Ana elimu ya Saa (Qiyaamah), na Anateremsha mvua na Anajua yale yaliyomo katika tumbo la uzazi, na nafsi yoyote haijui nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haijui itafia katika ardhi gani, hakika Allaah ni Mjuzi wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Luqman (31):34]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ﴿١٣﴾

Enyi watu! Hakika Sisi Tumekuumbeni kutokana namwanamme na mwanamke, na Tukakujaalieni  mataifa na makabila ili mtambuane. Hakika aliye na hadhi zaidi miongoni mwenu mbele ya Allaah ni mwenye taqwa zaidi kati yenu. Hakika Allaah ni Mjuzi wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-Hujuraat (49): 13]

 

 

 

الْحَكِيمُ

Al-Hakiym

Mwenye Hikma Wa Yote Daima

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Yeye Ndiye Mwenye Hikma ya juu kabisa kuliko wote, Ambaye Ndiye Mwenye Hikma yote katika uumbaji Wake na kuamuru Kwake, Ambaye Alikifanya vyema kila Alichokiumba.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّـهِ حُكْمًا لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ ﴿٥٠﴾

Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu kwa watu wenye yakini. [Al-Maa-idah (5): 50]

 

Kwa hivyo, Allaah (سبحانه وتعالى) Hakuumba kitu chochote kwa upuuzi tu na Hakutunga Shariy’ah yoyote bure tu au isiyokuwa ya maana na manufaa kwa viumbe Wake na uumbaji Wake.

 

  

Allaah (سبحانه وتعالى), Yeye Ndiye Pekee Mwenye kuhukumu mwanzoni na mwishoni. Ana sehemu tatu za kutawala ambazo hakuna kingine chochote chenye fungu humo. Anawatawala waja Wake kwa Shariy’ah Yake, Qadar Yake na jazaa Yake.

 

 

Maana ya hikma ni kukiweka kitu mahali pake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لِلَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ مَثَلُ السَّوْءِ ۖ وَلِلَّـهِ الْمَثَلُ الْأَعْلَىٰ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٦٠﴾

Kwa wale wasioamini Aakhirah wana mfano mbaya (ya upungufu); na Allaah Ana Sifa kamilifu tukufu kabisa. Naye ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [An-Nahl (16): 60]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَهُوَ الَّذِي فِي السَّمَاءِ إِلَـٰهٌ وَفِي الْأَرْضِ إِلَـٰهٌ ۚ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ﴿٨٤﴾

Na Yeye Ndiye Muabudiwa wa haki mbinguni na ardhini pia (Ndiye Huyo Huyo) Ilaah. Naye Ndiye Mwenye hikmah wa yote, Mjuzi wa yote. [Az-Zukhruf [(43):84]

 

 

 

الرَّحْمنُ

Ar-Rahmaan

Mwingi Wa Rahmah

 

 

 

الرَّحِيمُ

Ar-Rahiym

Mwenye Kurehemu

 

 

الْبَرُّ

Al Barr

Mwingi Wa Ihsani

 

 

 

الْكَرِيمُ

Al-Kariym

Karimu

 

 

الْجَوَّادُ

Al-Jawwaad

Mwingi wa Ukarimu

 

 

 

الرَّؤُوفُ

Al-Rauwf:

Mwenye Huruma Mno

 

 

 

الْوَاهَّابُ

Al Wahhaab

Mwingi Wa Kutunuku, Mpaji Wa Yote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Majina yote haya yana maana yaliyokaribiana, na yote yanaelekeza katika kueleza sifa za Ar-Rabb kuwa na Rahmah na ukarimu. Zinaelekeza katika eneo kubwa la Rahmah yake na hadiya, tunuku inayokizunguka kila kilichopo, wanazopewa kwa mujibu wa amri za Yake. Waumini wamechaguliwa makhususi kwa ajili ya hili na wanapewa fungu zuri lililo bora katika haya, ni sawa na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ فَسَأَكْتُبُهَا لِلَّذِينَ يَتَّقُونَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَالَّذِينَ هُم بِآيَاتِنَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٥٦﴾

Na Tuandikie katika dunia hii mazuri na katika Aakhirah. Hakika sisi Na rahmah Yangu imeenea kila kitu. Basi Nitawaandikia wale wenye taqwa na wanaotoa Zakaah na ambao wao wanaziamini Aayaat (ishara, dalili) Zetu. [Al-A’raaf (7):156]

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Baraka zote na namna mbali mbali za ukarimu zinatokana na athari ya Rahmah Yake na ukarimu kama ukarimu humu duniani na Aakhirah zinatokana na athari ya Rahmah Yake.

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الرَّحْمَـٰنُ ﴿١﴾

Ar-Rahmaan.

 

عَلَّمَ الْقُرْآنَ ﴿٢﴾

Amefundisha Qur-aan.

 

خَلَقَ الْإِنسَانَ ﴿٣﴾

Ameumba insani.

 

عَلَّمَهُ الْبَيَانَ ﴿٤﴾

Amemfunza ufasaha. 

 

[Ar-Rahmaan (55): 1 - 4]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

=

إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ﴿٢٨﴾

Hakika sisi tulikuwa kabla Tunamuomba Yeye Pekee, hakika yeye Ndiye Mwingi huruma na fadhila, Mwenye kurehemu. [At-Tuwr (52):28]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ ﴿٦﴾

Ee mwana Aadam! Nini kilichokughuri kuhusu Rabb wako Mkarimu? [Al-Infitwaar (82): 6]

 

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ وَأَنَّ اللَّـهَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٠﴾

Na lau si fadhila ya Allaah juu yenu na rahmah Yake, na kwamba Allaah ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu. [An-Nuwr (24): 20]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

رَبَّنَا لَا تُزِغْ قُلُوبَنَا بَعْدَ إِذْ هَدَيْتَنَا وَهَبْ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحْمَةً ۚ إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ ﴿٨﴾

 (Husema): Rabb wetu, Usizipotoe nyoyo zetu baada ya kuwa Umetuhidi na Tutunukie kutoka kwako rahmah. Hakika Wewe ni Mwingi wa kutunuku na kuneemesha.  [Aali ‘Imraan (3):8]

 

 

السَّمِيعُ

As-Samiy’i

Mwenye Kusikia Yote Daima

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Anayesikia sauti zote, katika lugha zake tofauti tofauti na zote katika wingi wake na haja mbalimbali.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِنْ آمَنُوا بِمِثْلِ مَا آمَنتُم بِهِ فَقَدِ اهْتَدَوا ۖ وَّإِن تَوَلَّوْا فَإِنَّمَا هُمْ فِي شِقَاقٍ ۖ فَسَيَكْفِيكَهُمُ اللَّـهُ ۚ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿١٣٧﴾

Watakapoamini kama vile mlivyoamini nyinyi, basi kwa yakini watakuwa wameongoka; na wakikengeuka basi hakika wao wamo katika upinzani, na Allaah Atakutosheleza nao, Naye ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote. [Al-Baqarah (2):137]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَاللَّـهُ يَقْضِي بِالْحَقِّ ۖ وَالَّذِينَ يَدْعُونَ مِن دُونِهِ لَا يَقْضُونَ بِشَيْءٍ ۗ إِنَّ اللَّـهَ هُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ﴿٢٠﴾

Na Allaah Anahukumu kwa haki. Na wale wanaowaomba badala Yake hawawezi kuhukumu kwa chochote. Hakika Allaah Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ghaafir (40): 20]

 

 

الْبَصِيرُ

Al-Baswiyr

Mwenye Kuona Yote Daima

 

 

 

Allaah (عز وجل), Anayeona vitu vyote hata visivyo muhimu na vidogo sana. Yeye (سبحانه وتعالى) Anamwona sisimizi mweusi juu ya jiwe jeusi katika usiku wa giza. Anakiona kilicho chini ya ardhi ya saba na kilicho juu ya mbingu ya saba. Pia Anawasikia na Anawaona wale wenye kustahiki jazaa, kwa mujibu wa amri na Hikma Yake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ أَؤُنَبِّئُكُم بِخَيْرٍ مِّن ذَٰلِكُمْ ۚ لِلَّذِينَ اتَّقَوْا عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَأَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ وَرِضْوَانٌ مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِالْعِبَادِ ﴿١٥﴾

Sema: Je, nikujulisheni yaliyo bora kuliko hayo? Kwa wale waliokuwa na taqwa kwa Rabb wao watapata Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo na wake waliotakasika na radhi kutoka kwa Allaah. Na Allaah ni Mwenye kuwaona waja. [Aali ‘Imraan (3): 15]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَن تَنفَعَكُمْ أَرْحَامُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ ۚ يَوْمَ الْقِيَامَةِ يَفْصِلُ بَيْنَكُمْ ۚ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ﴿٣﴾

Hawatokufaeni jamaa zenu wa uhusiano wa damu, na wala watoto wenu Siku ya Qiyaamah (Allaah) Atapambanua baina yenu; na Allaah kwa yale myatendayo ni Mwenye kuona. [Al-Mumtahinah (60): 3]

 

 

الْحَمِيدُ

Al-Hamiyd

Mwenye Kustahiki Kuhimidiwa

 

 

 

Allaah (عز وجل), Katika Nafsi Yake, Majina Yake, Sifa Zake na Matendo Yake. Ana Majina bora kuliko wote, na Ana Sifa kamilifu zaidi kuliko wote zikiambatana na matendo bora na timilifu kuliko wote.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الر ۚ كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ لِتُخْرِجَ النَّاسَ مِنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ بِإِذْنِ رَبِّهِمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿١﴾

Alif Laam Raa. Kitabu Tumekiteremsha kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) ili uwatoe watu kutoka kwenye viza kuwaingiza katika nuru kwa idhini ya Rabb wao, waelekee katika njia ya Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Ibraahiym (14): 1]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ آتَيْنَا لُقْمَانَ الْحِكْمَةَ أَنِ اشْكُرْ لِلَّـهِ ۚ وَمَن يَشْكُرْ فَإِنَّمَا يَشْكُرُ لِنَفْسِهِ ۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ حَمِيدٌ ﴿١٢﴾

Kwa yakini Tulimpa Luqmaan hikmah kwamba: Mshukuru Allaah. Na anayeshukuru, basi hakika anashukuru kwa manufaa ya nafsi yake. Na anayekufuru, basi hakika Allaah ni Mkwasi, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Luqmaan (31): 12]

 

 

الْمَجِيدُ

Al-Majiyd

Mwingi Mno Wa Vipawa Na Ukarimu

 

 

الْكَبِيرُ

Al-Kabiyr

Mkubwa Wa Dhati, Vitendo Na Sifa

 

 

الْعَظِيمُ

Al-‘Adhwiym

Adhimu, Mwenye Taadhima

 

 

الْجَلِيلُ

Al-Jaliyl

Jalali, Mwenye Ujalali, Mtukuka Daima, Mwenye Hadhi

 

 

 

Allaah (عز وجل), Yeye Ana Aifa ya ‘Uluwa, Utukufu na Ukubwa. Yeye Ndiye mkubwa kuliko wote, Mtukuka zaidi na mkubwa kuliko kitu chochote. Yeye Huadhimishwa na kufanywa mkubwa nyonyoni mwa marafiki zake na walio karibu Naye, nyoyo zao zinatiririkiwa na ukubwa Wake na taadhima Yake, kujisalimisha mbele Yake na unyenyekevu mbele ya utukufu Yake.

 

Anasema Allaah (عز وجل):

ذُو الْعَرْشِ الْمَجِيدُ ﴿١٥﴾

Mwenye ‘Arsh; Mwenye utukufu kamili, enzi, wingi wa vipawa, fadhila na ukarimu. [Al-Buruwj (85):15]

 

Na Anasema pia Allaah (عز وجل):

عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْكَبِيرُ الْمُتَعَالِ ﴿٩﴾

Mjuzi wa ghayb na dhahiri, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa, Mwenye Uluwa Aliyejitukuza kabisa. [Ar-Ra’d (13): 9]

 

Na pia Anasema Allaah (عز وجل):

 

فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ ﴿٧٤﴾

Basi sabbih kwa Jina la Rabb wako Adhimu Mkuu kabisa. [Al-Waaqi’ah (56): 74]

 

الْعَفُوُّ

Al-‘Afuww

Mwingi Wa Kusamehe

 

 

الْغَفُورُ

Al-Ghafuur

Mwingi Wa Kughufiria, Kusitiri

 

 

الْغَفَّارُ

Al-Ghaffaar

Mwingi Wa Kughufuria, Kusitiri Mara Kwa Mara

 

 

 

Allaah (عز وجل) ni Pekee Ambaye Alikuwa na hata sasa ni Mwenye Sifa ya kusamehe. Allaah (عز وجل) Ndiye Aliyekuwa, na hata sasa Anaonyesha msamaha na huruma kwa waja Wake. Kila mmoja yuko katika haja kubwa sana ya maghfirah Yake kama walivyo na haja kubwa ya Rahmah Yake na ukarimu. Allaah (سبحانه وتعالى) Ameahidi maghfirah na msamaha kwa mwenye kutimiza masharti yake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِنِّي لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا ثُمَّ اهْتَدَىٰ ﴿٨٢﴾

Na hakika Mimi bila shaka ni Mwingi mno wa kughufuria kwa anayetubia na akaamini na akatenda mema kisha akaendelea kuongoka.   [Twahaa (20): 82]

 

Na pia Anasema Allaah (عز وجل):

 

دَرَجَاتٍ مِّنْهُ وَمَغْفِرَةً وَرَحْمَةً ۚ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٩٦﴾

Ni daraja za vyeo (vya juu) kutoka Kwake na maghfirah na rahmah. Na Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa (4):  96]

 

Na pia Anasema Allaah (عز وجل):

 

أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ ۖ قُلْ إِنِ افْتَرَيْتُهُ فَلَا تَمْلِكُونَ لِي مِنَ اللَّـهِ شَيْئًا ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَا تُفِيضُونَ فِيهِ ۖ كَفَىٰ بِهِ شَهِيدًا بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ ۖ وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٨﴾

Je, wanasema ameitunga?  Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Ikiwa nimeitunga, basi hamna uwezo wa kunifaa chochote mbele ya Allaah. Yeye Anajua zaidi yale mnayoyaropokwa. Ananitosheleza kuwa Shahidi baina yangu na baina yenu; Naye Ndiye Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Ahqaaf (46): 8]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى) :

إِن تُبْدُوا خَيْرًا أَوْ تُخْفُوهُ أَوْ تَعْفُوا عَن سُوءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَفُوًّا قَدِيرًا ﴿١٤٩﴾

Mkidhihirisha khayr au mkiificha au mkisamehe uovu; basi hakika Allaah daima ni Mwingi wa kusamehe, Muweza wa yote. [An-Nisaa (4): 149]

 

 

التَّوَّابُ

At-Tawwaab

Mwingi Wa Kupokea Toba Baada Ya Toba

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Ambaye Anaendelea kuwageukia kwa maghfirah na msamaha wale wanaogeukia Kwake kwa tawbah, na Anayesamehe makosa ya mwenye kutubu. Wote wanaogeukia kwa Allaah (عز وجل) kwa dhati, Allaah (عز وجل) Anawageukia kwa kuanza kuwapa uwezo wa kutubu na kuelekeza nyoyo zao upande Wake, kisha baada ya hili Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) huwageukia kwa kupokea tawbah zao na kuwasamehe makosa yao.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ هُوَ يَقْبَلُ التَّوْبَةَ عَنْ عِبَادِهِ وَيَأْخُذُ الصَّدَقَاتِ وَأَنَّ اللَّـهَ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ﴿١٠٤﴾

Je, hawajui kwamba Allaah Ndiye Anayepokea tawbah ya waja Wake, na Anapokea Swadaqah na kwamba Allaah Ndiye Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [At-Tawbah (9):104]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ﴿١٢﴾

Enyi walioamini!  Jieupusheni sana na dhana kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi, na wala wasisengenyane baadhi yenu wengineo. Je, anapenda mmoja wenu kwamba ale nyama ya nduguye aliyekufa? Basi mmelichukia hilo! Na mcheni Allaah! Hakika Allaah ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [Al-Hujuraat (49): 12]

 

 

الْقُدُّوسُ

Al-Qudduus

Mtakatifu Ametakasika Na Sifa Zote Hasi

 

 

السَّلاَمُ

As-Salaam

Mwenye Amani, Mwenye Kusalimika Na Kasoro Zote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Aliye Mkubwa na Ameepukana mbali na namna yoyote ya ila, kasoro, au kufanana na kiumbe Chake chochote. Hivyo, Ameepukana mbali na namna yoyote ya upungufu kama Alivyoepukana na Sifa ya kushabihiana Naye au kukaribia hilo katika Sifa Yake yoyote ya ukamilifu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

  لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ﴿١١﴾

Hakuna chochote kinachofanana Naye, Naye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ash-Shuwraa (42): 11]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ ﴿٤﴾

Na wala haiwi Awe na yeyote anayefanana na kulingana Naye. [Al-Ikhlaasw (112): 4]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَاعْبُدْهُ وَاصْطَبِرْ لِعِبَادَتِهِ ۚ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا ﴿٦٥﴾

Rabb wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake; basi mwabudu Yeye tu na dumisha subira katika ‘ibaadah Yake. Je, unamjua yeyote anayefanana Naye (Allaah)?  [Maryam (19): 65]

 

Na Ameonya Allaah (سبحانه وتعالى):

فَلَا تَجْعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا

Basi msimfanyie Allaah waliolingana naye [Al-Baqarah (2):22]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يُسَبِّحُ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ الْمَلِكِ الْقُدُّوسِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ﴿١﴾

 Vinamsabbih Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi, Mfalme, Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Jumu’ah (62): 1]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha na Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi na kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mwenye ukubwa na uadhama, Subhaana Allaah! Utakasifu ni wa Allaah kutokana na ambayo wanamshirikisha. [Al-Hashr (59):23]

 

 

الْعَلِيُّ

Al‘Aliyy

Yuko Juu Ya Vyote, Mwenye ‘Uluwa

 

 

الأَعْلى

Al-A’laa

Mwenye ‘Uluwa Na Taadhima Kuliko Vyote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى), Kwake Yeye ndipo kwenye ‘Uluwa katika vipengele Vyake vyote. ‘Uluwa wa Nafsi Yake, ‘Uluwa wa Sifa Zake na enzi, ‘Uluwa wa nguvu na nguvu. Allaah (عز وجل), Yeye Ndiye Pekee aliye katika Kiti Chake cha Enzi na Ndiye Aliyekizunguka kwa mamlaka. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Pekee ambaye ziko Kwake Sifa za ukubwa, utukufu, ukuu na uzuri unapata ukamilifu na utimilifu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ﴿٤﴾

Ni Vyake vilivyomo mbinguni na ardhini, Naye ni (Mwenye ‘Uluwa, Ametukuka,  Mwenye Taadhima, Mkuu kabisa. [Ash-Shuwraa (42): 4]

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى ﴿١﴾

Sabbih Jina la Rabb wako Mwenye ‘Uluwa Ametukuka kabisa kuliko vyote. [Al-A’laa [(87): 1]

 

 

الْعَزِيزُ

Al-‘Aziyz

Mwenye Nguvu, Mshindi Asiyeshindika Daima

 

 

 

Allaah (عز وجل) ni Pekee Aambaye Kwake ndiko kwenye nguvu na taadhima katika ukamilifu Wake, nguvu na taadhima ya nguvu, ya ushindi na ya kuzuia. Amewazuia viumbe Wake wote dhidi ya kumzunguka na kumkamata. Allaah (عز وجل), Yeye ni Mweza  juu ya kila kitu kilichopo, viumbe wote ni watawaliwa na wanawajibika Kwake, wamesalimu amri mbele ya Utukufu Wake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَهُ الْكِبْرِيَاءُ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٣٧﴾

Na Ukubwa, Uadhama, Ujalali ni Wake Pekee mbinguni na ardhini; Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [AL-Jaathiyah (45): 37]

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿١﴾

Amebarikika Ambaye Mkononi Mwake umo ufalme Naye juu ya kila kitu ni Muweza.

 

الَّذِي خَلَقَ الْمَوْتَ وَالْحَيَاةَ لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلًا ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْغَفُورُ﴿٢﴾

Ambaye Ameumba mauti na uhai ili Akujaribuni ni nani kati yenu mwenye ‘amali nzuri zaidi. Naye ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwingi wa kughufuria. [Al-Mulk (67): 1-2]

 

 

 

الْقَوِيُّ

Al-Qawiyy

Mwenye Nguvu

 

 

الْمَتِينُ

Al-Matiyn:

Mwenye Nguvu Na Shadidi, Madhubuti

 

 

 

Majina haya yanaingia katika maana ya Al’Aziyz.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ أُخْرِجُوا مِن دِيَارِهِم بِغَيْرِ حَقٍّ إِلَّا أَن يَقُولُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ۗ وَلَوْلَا دَفْعُ اللَّـهِ النَّاسَ بَعْضَهُم بِبَعْضٍ لَّهُدِّمَتْ صَوَامِعُ وَبِيَعٌ وَصَلَوَاتٌ وَمَسَاجِدُ يُذْكَرُ فِيهَا اسْمُ اللَّـهِ كَثِيرًا ۗ وَلَيَنصُرَنَّ اللَّـهُ مَن يَنصُرُهُ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَقَوِيٌّ عَزِيزٌ ﴿٤٠﴾

Ambao wametolewa majumbani mwao bila ya haki isipokuwa kwa kuwa wanasema: Rabb wetu ni Allaah. Na lau ingelikuwa Allaah Hawakingi watu baadhi yao kwa wengine, bila shaka yangelivunjwa mahekalu na makanisa, na masinagogi na Misikiti inayotajwa humo Jina la Allaah kwa wingi. Na bila shaka Allaah Atamnusuru yeyote yule anayenusuru Dini Yake. Hakika Allaah bila shaka ni Mwenye nguvu zote, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika. [Al-Hajj (22): 40]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ ﴿٥٨﴾

Hakika Allaah Ndiye Mwingi wa kuruzuku, Mwenye nguvu Madhubuti. [Adh-Dhaariyaat (51): 58]

 

 

 

الْجَبَّارُ

Al-Jabbaar

Jabari, Mwenye Kulazimisha, Mwenye Kuunga

 

 

 

 

Jina hili la Allaah (سبحانه وتعالى)  linajumuisha maana ya Al-‘Aliy na Al-A’laa, maana ya Al-Qahhaar na maana ya Ar-Rauwf.

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayezifanyia ukarimu na kuziponya roho. Allaahz ni Pekee Anayewapa nguvu wanyonge na walio dhaifu, Allaah (عز وجل) ni Pekee Anayewalinda na kuwapa hifadhi wale wanaokimbilia Kwake na kuomba hifadhi Kwake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha na Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi na kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mwenye ukubwa na uadhama, Subhaana Allaah! Utakasifu ni wa Allaah kutokana na ambayo wanamshirikisha. [Al-Hashr (59): 23]

 

 

الْمُتَكَبِّرُ

Al-Mutakabbir

Mwenye Kustahiki Kutakabari, Yuko Juu Ya Viumbe

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee mwenye kustahiki kutakabari, Aliye juu ya lolote ovu, lenye ila na upungufu kutokana na ukubwa Wake na utukufu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha na Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi na kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mwenye ukubwa na uadhama, Subhaana Allaah! Utakasifu ni wa Allaah kutokana na ambayo wanamshirikisha. [Al-Hashr (59): 23]

 

 

الْخَالِقُ

Al-Khaaliq

Muumbaji

 

 

الْبَارِئُ

Al-Baariu

Muumbaji Viumbe Kwa Maumbile

Yanayonasibiana Na Mazingira Ya Maisha Yao

 

 

 

الْمُصَوِّرُ

Al-Muswawwir

Muundaji Sura Na Maumbile

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Aliyeumba vyote vilivyopo na Alivianzisha, Aliyekifanya kila kitu sawa na katika mahali pake kwa mujibu wa amri na Hikmah Yake. Aliyekitia umbo kila kitu Hikma Yake. Allaah (سبحانه وتعالى) Anaendelea kufanya hivyo.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ۚ يُسَبِّحُ لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٢٤﴾

Yeye Ndiye Allaah, Muumbaji, Mwanzishi viumbe bila kasoro, Muundaji sura na umbile, Ana Majina Mazuri kabisa, kinamsabihi Pekee kila kilichokuweko katika mbingu na ardhi, Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Hashr (59): 24]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 هُوَ الَّذِي يُصَوِّرُكُمْ فِي الْأَرْحَامِ كَيْفَ يَشَاءُ ۚ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٦﴾

Yeye Ndiye Aliyekusawirini umbo katika matumbo ya uzazi vile Atakavyo. Hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Aal-‘Imraan: (3): 6]

 

 

الْمُؤمِنُ

Al-Muumin

Mwenye Kusadikisha Ahadi, Mwenye Kuaminisha

 

 

 

Allaah (عز وجل) ni Pekee Aliyejisifia Mwenyewe kwa Sifa kamilifu na kwa ukamilifu wa utukufu na uzuri. Allaah (عز وجل) ni Pekee Aliyewapeleka Rusuli Wake na Akateremsha Vitabu Vyake pamoja na dalili na ushahidi dhahiri. Allaah (عز وجل) ni Pekee Anayeshuhudia ukweli wa Rusuli Wake kwa kuwapa kila dalili na ushahidi wa kuthibitisha ukweli wa kile walichokuja nacho.

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha na Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi na kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mwenye ukubwa na uadhama, Subhaana Allaah! Utakasifu ni wa Allaah kutokana na ambayo wanamshirikisha. [Al-Hashr (59): 23]

 

 

 

الْمُهَيْمِنُ

Al-Muhaymin

Mwenye Kutawalia Na Kuendesha

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayeona mambo yaliyofichikana, yote ambayo nyoyo hutunza kiuficho. Allaah (سبحانه وتعالى) Ambaye elimu Yake inakizingira kila kitu.

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha na Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi na kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mwenye ukubwa na uadhama, Subhaana Allaah! Utakasifu ni wa Allaah kutokana na ambayo wanamshirikisha. [Al-Hashr (59): 23]

 

 

 

الْقَدِيرُ

Al-Qadiyr

Muweza Wa Yote Daima

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Mwenye nguvu timilifu na kamilifu na uwezo. Kwa nguvu Zake Amefanya kila kitu kiwepo. Kwa nguvu hiyo Yeye hupanga kila kitu. Kwa nguvu hiyo, Ameumba na kukamilisha uumbaji. Kwa nguvu hiyo, Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) Huhuisha na kufisha. Kwa nguvu hiyo Atafufua waja kwa ajili ya jazaa yao;  kuwapa malipo waliofanya mema na kuwaingiza Motoni kwa waliotenda uovu. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye, Anapotaka jambo liwe huliambia tu:

كُن فَيَكُونُ

 

Kun! basi (jambo) huwa!

 

Kwa nguvu Zake Allaah (سبحانه وتعالى) na uwezo, hugeuza nyoyo na kuzielekeza kwa yeyote Amtakaye.

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلِكُلٍّ وِجْهَةٌ هُوَ مُوَلِّيهَا ۖ فَاسْتَبِقُوا الْخَيْرَاتِ ۚ أَيْنَ مَا تَكُونُوا يَأْتِ بِكُمُ اللَّـهُ جَمِيعًا ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٤٨﴾

Na kila mmoja ana upande wa kuuelekea. Basi shindaneni kwenye mambo ya khayr. Popote mtakapokuwa Allaah Atakuleteni nyote pamoja (Qiyaamah). Hakika Allaah juu ya kila kitu ni Muweza. [Al-Baqarah (2): 148]

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَوَلَمَّا أَصَابَتْكُم مُّصِيبَةٌ قَدْ أَصَبْتُم مِّثْلَيْهَا قُلْتُمْ أَنَّىٰ هَـٰذَا ۖ قُلْ هُوَ مِنْ عِندِ أَنفُسِكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٦٥﴾

Ulipokusibuni msiba ingawa mliwasibu (maadui) mara mbili yake mlisema: Umetoka wapi huu? Sema: Huo ni kutoka kwenu wenyewe. Hakika Allaah juu ya kila kitu ni Muweza. [Aali ‘Imraan (3): 165]

 

 

اللَّطِيف

Al-Latwiyf

Latifu, Mwenye Kudabiri Mambo Kwa Utuvu,

Mjuzi Wa Ya Dhihiri Na Ya Siri

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye elimu Yake inakizingira siri zote na mambo yalifichikana, Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye Anayekijua vyema yote yaliyofichikana katika kina cha mbingu na ardhi na Anakijua kila kitu hadi chini mpaka utondoti mdogo wa chini kabisa.  Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Aliye mwema kwa waja Wake Waumini, Akiwaongoza kuelekea kwenye lililo na faida kwao na kuwasaidia kupitia njia wasizozijua, haya ni kwa Ukarimu na Ukarimu Wake. Jina hili linabeba pia maana za Al-Kabiyr na Ar-Rauwf.

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ ۖ وَهُوَ اللَّطِيفُ الْخَبِيرُ ﴿١٠٣﴾

Macho hayamzunguki bali Yeye Anayazunguka macho yote; Naye ni Mwenye kudabiri mambo kwa ulatifu, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika [Al-An’aam (6): 103]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَتُصْبِحُ الْأَرْضُ مُخْضَرَّةً ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ ﴿٦٣﴾

Je, huoni kwamba Allaah Ameteremsha kutoka mbinguni maji kisha ardhi ikawa chanikiwiti. Hakika Allaah bila shaka ni Mwenye kudabiri mambo kwa ulatifu, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-Hajj (22): 63]

 

 

الْحَسِيبُ

Al-Hasiyb

Mwenye Kuhesabu, Kutosheleza

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ajuaye yote ya waja Wake na kuwatosheleza wanaomtegemea. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewalipa waja Wake ima wema au ubaya kwa hikma na elimu juu ya utondoti mdogo kabisa wa amali zao.

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا ﴿٨٦﴾

Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo. Hakika Allaah daima ni Mwenye kuhesabu kila kitu. [An-Nisaa (4): 86]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ يُبَلِّغُونَ رِسَالَاتِ اللَّـهِ وَيَخْشَوْنَهُ وَلَا يَخْشَوْنَ أَحَدًا إِلَّا اللَّـهَ ۗ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ حَسِيبًا ﴿٣٩﴾

Wale wanaobalighisha ujumbe wa Allaah na wanamkhofu Yeye na wala hawamkhofu yeyote isipokuwa Allaah. Na Allaah Anatosheleza kuwa Mwenye kuhesabu. [Al-Ahzaab (33): 39]

 

 

 

الرَّقِيبُ

Ar-Raqiyb

Mwenye Kuchunga

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye huona kilichofichikana nyoyoni. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayeihukumu kila roho kwa ilichochokichuma. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayekifadhi kila kilichoumbwa na kuviendesha kwa usimamizi bora kabisa na kwa mpango timamu na kamilifu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ 

Enyi watu! Mcheni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume na wanawake wengi. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. Hakika Allaah ni Mwenye kuwachunga daima. [An-Nisaa (4):1]

 

الْحَافِظُ

Al-Haafidhw

Mwenye Kuhifadhi, Kulinda

 

 

الْحَفِيظُ

Al-Hafiydhw:

Mwenye Kuhifadhi, Kulinda

 

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayehifadhi na kutunza Alivyoviumba na Ambaye elimu Yake inavizunguka vyote Alivyovifanya viwepo. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewahifadhi marafiki Zake dhidi ya kuangukia katika madhambi na mambo ya hilaki. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Aliye Mkarimu kwao katika nyakati za harakati na mapumziko. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayehesabu amali za waja na malipo yao.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ صَدَّقَ عَلَيْهِمْ إِبْلِيسُ ظَنَّهُ فَاتَّبَعُوهُ إِلَّا فَرِيقًا مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢٠﴾

Na kwa yakini Ibliys alisadikisha dhana yake juu yao, basi walimfuata isipokuwa kundi miongoni mwa Waumini.

 

 

وَمَا كَانَ لَهُ عَلَيْهِم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا لِنَعْلَمَ مَن يُؤْمِنُ بِالْآخِرَةِ مِمَّنْ هُوَ مِنْهَا فِي شَكٍّ ۗ وَرَبُّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَفِيظٌ ﴿٢١﴾

Na yeye (Ibliys) hakuwa ana madaraka yoyote juu yao isipokuwa ili Tujue ni nani yule anayeamini Aakhirah na nani yule anayeitilia shaka. Na Rabb wako ni Mwenye kuhifadhi kila kitu. [Sabaa (34): 20-21]

 

Na pia Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى) :

 

قَالَ هَلْ آمَنُكُمْ عَلَيْهِ إِلَّا كَمَا أَمِنتُكُمْ عَلَىٰ أَخِيهِ مِن قَبْلُ ۖ فَاللَّـهُ خَيْرٌ حَافِظًا ۖ وَهُوَ أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ ﴿٦٤﴾

Akasema: Je, nimwaminishe kwenu ila kama nilivyokuaminini juu ya kaka yake kabla? Basi Allaah ni Mbora wa wenye kuhifadhi. Naye ni Mbora zaidi wa kurehemu kuliko wengine wote wenye kurehemu. [Yuwsuf (12): 64]

 

 

 

الْمُحِيطُ

Al-Muhiytw

Mwenye Kuzunguka Vyote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Mwenye elimu ya kila kitu, Rahmah Yake inakizunguka kila kitu, Naye ni Mwenye kutamalaki na kutawala  kila kitu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِن تَمْسَسْكُمْ حَسَنَةٌ تَسُؤْهُمْ وَإِن تُصِبْكُمْ سَيِّئَةٌ يَفْرَحُوا بِهَا ۖ وَإِن تَصْبِرُوا وَتَتَّقُوا لَا يَضُرُّكُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا ۗ إِنَّ اللَّـهَ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطٌ ﴿١٢٠﴾

Ikikuguseni hasanah (nusura, ushindi) inawachukiza, na likikusibuni baya hulifurahia; na mkisubiri na mkawa na taqwa haitokudhuruni chochote katika hila zao. Hakika Allaah ni Mwenye kuyazunguka wayatendayo.  [Aali ‘Imraan (3): 120]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ خَرَجُوا مِن دِيَارِهِم بَطَرًا وَرِئَاءَ النَّاسِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ ۚ وَاللَّـهُ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطٌ﴿٤٧﴾

Na wala msiwe kama wale waliotoka majumbani mwao kwa majivuno na kujionyesha kwa watu, na wanazuia njia ya Allaah. Na Allaah ni Mwenye kuyazunguka yote wanayoyatenda. [Al-Anfaal (8): 47]

 

 

الْقَهَّارُ

Al Qahhaar

Mwenye Kuteza Nguvu Asiyepingika

 

 

الْقَاهِرُ

Al-Qaahir

Mwenye Kuteza Nguvu Asiyepingika

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Aliyekitiisha kila kitu. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye mbele Yake uumbaji wote umetii na kunyenyekea mbele ya utukufu na nguvu kamilifu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَهُوَ الْقَاهِرُ فَوْقَ عِبَادِهِ ۖ وَيُرْسِلُ عَلَيْكُمْ حَفَظَةً حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ تَوَفَّتْهُ رُسُلُنَا وَهُمْ لَا يُفَرِّطُونَ ﴿٦١﴾

Naye ni Asiyepingika, Aliye Mkuu kabisa juu ya waja Wake, na Anakutumieni Malaika wanaohifadhi hata yanapomfikia mmoja wenu mauti, Wajumbe Wetu humfisha, nao hawafanyi taksiri. [Al-An’aam (6): 61]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَلَا تَحْسَبَنَّ اللَّـهَ مُخْلِفَ وَعْدِهِ رُسُلَهُ ۗ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ ﴿٤٧﴾

Basi usidhanie kwamba Allaah ni Mwenye kukhalifu ahadi Yake kwa Rusuli Wake. Hakika Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kulipiza.

 

يَوْمَ تُبَدَّلُ الْأَرْضُ غَيْرَ الْأَرْضِ وَالسَّمَاوَاتُ ۖ وَبَرَزُوا لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ﴿٤٨﴾

Siku ardhi itakapobadilishwa kuwa ardhi nyingine na mbingu pia na (viumbe wote) watahudhuria kwa Allaah Mmoja Pekee, Asiyepingika. [Ibraahiym (14): 47-48]

 

 

 

الْمُقِيتُ

Al-Muqiyt

Mwenye Kuruzuku Chakula

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye hukipa riziki kila kiumbe kilichopo kwa kitu cha kukitia nguvu, Anayekipa chakula na kukiongoza kwa vyovyote Atakavyo kulingana na hikma na sifa Yake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّن يَشْفَعْ شَفَاعَةً حَسَنَةً يَكُن لَّهُ نَصِيبٌ مِّنْهَا ۖ وَمَن يَشْفَعْ شَفَاعَةً سَيِّئَةً يَكُن لَّهُ كِفْلٌ مِّنْهَا ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقِيتًا ﴿٨٥﴾

Atakayeombea uombezi mzuri atapata fungu lake katika hayo. Na atakayeombea uombezi mbaya atapata sehemu yake katika hayo. Na Allaah daima ni Mwenye kudhibiti na Mwangalizi wa kila kitu[An-Nisaa (4): 85]

 

 

 

الْوَكِيلُ

Al-Wakiyl

Mtegemewa Kwa Yote, Msimamizi

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Mwenye jukumu la kupanga mambo ya viumbe kulingana na Elimu Yake, nguvu kamili na kila Hikmah inayozunguka. Allaah (عز وجل) ni Pekee Anayewatazama marafiki Wake na kuwarahisishia mambo, kuwahifadhi dhidi ya uovu na kuwatoshelezea mambo yao yote. Hivyo, mwenye kumtegemea, Yeye humtosheleza.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 اللَّـهُ وَلِيُّ الَّذِينَ آمَنُوا يُخْرِجُهُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ ۖ  

Allaah ni Mlinzi Msaidizi wa wale walioamini, Anawatoa kutoka katika viza na kuwaingiza katika nuru. [Al-Baqarah (2): 257]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ فَاعْبُدُوهُ ۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ وَكِيلٌ ﴿١٠٢﴾

Huyo kwenu Ndiye Allaah, Rabb wenu. Hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye Muumbaji wa kila kitu, basi mwabuduni Yeye Pekee. Naye juu ya kila kitu ni Mdhamini Anayetegemewa kwa yote. [Al-An’aam (6): 102]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿٣﴾

Na tawakali kwa Allaah, na Anatosheleza Allaah kuwa ni Mdhamini. [Al-Ahzaab (33): 3]

 

 

 

ذُو الْجَلاَلِ وَالإِكْرامِ

Mwenye Ujalali Na Ukarimu,

Mwenye Utukufu wa Juu Kabisa, Ukarimu Na Hadhi

 

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee  Mwenye ukuu, utukufu, Rahmah na ukarimu. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Mwenye kuonyesha ukarimu katika nyanja zote mbili, jumla na mahsusi. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewapandisha hadhi marafiki Wake na walio karibu Naye.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ ﴿٢٦﴾

Kila aliyekuwa juu yake (ardhi) ni mwenye kutoweka.

 

وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ ﴿٢٧﴾

Na utabakia Wajihi wa Rabb wako Mwenye Ujalali na Taadhima. [Ar-Rahmaan (55): 26-27]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ ﴿٧٨﴾

Tabaarak, Limebarikika Jina la Rabb wako Mwenye Ujalali na Ukarimu. [Ar-Rahmaan (55): 78]

 

 

 

الْوَدُودُ

Al-Waduwd

Mwenye Mapenzi Tele Halisi

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewapenda Manabii na Rusuli Wake na wafuasi wao, nao pia wanampenda. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni mpendwa wao zaidi kuliko kingine chochote. Nyoyo zao zimejazwa na mapenzi Kwake, ndimi zao mara huendelea kuwa na rutuba kwa kumhimidi Yeye na nyoyo zao mara zote zimevutwa Kwake kwa mapenzi, unyoofu na tawbah.

 

Kauli Yake Allaah (عز وجل):

 

وَاسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي رَحِيمٌ وَدُودٌ﴿٩٠﴾

Na ombeni maghfirah kwa Rabb wenu, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu ni Mwenye kurehemu, Mwenye upendo halisi. [Huwd (11): 90]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

وَهُوَ الْغَفُورُ الْوَدُودُ ﴿١٤﴾

Naye ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye upendo halisi. [Al-Buruwj (85): 14]

 

 

 

الْفَتَّاحُ

Al-Fattaah

Mwingi Wa Kufungua, Kuhukumu

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Atakayewahukumu waja Wake kwa taratibu Zake za Shariy’ah. Taratibu Zake za amri na za jazaa. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewafumbua macho wale walio wakweli na niya safi kupitia ukarimu Wake. Allaah (عز وجل) ni Pekee Anayewafungua nyoyo zao ili waweze kumjua Yeye, wampende na watubu Kwake. Yeye hufungua milango ya Rahmah na rizki kwa waja Wake na Anawapa njia za kupata vyote viwili, mema ya humu duniani na Aakhirah.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّا يَفْتَحِ اللَّـهُ لِلنَّاسِ مِن رَّحْمَةٍ فَلَا مُمْسِكَ لَهَا ۖ وَمَا يُمْسِكْ فَلَا مُرْسِلَ لَهُ مِن بَعْدِهِ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٢﴾

Rahmah yoyote Anayoifungua Allaah kwa watu, basi hakuna wa kuizuia, na Anayoizuia, basi hakuna wa kuipeleka baada Yake, Naye ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Faatwir (35): 2]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ يَجْمَعُ بَيْنَنَا رَبُّنَا ثُمَّ يَفْتَحُ بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَهُوَ الْفَتَّاحُ الْعَلِيمُ ﴿٢٦﴾

Sema: Rabb wetu Atatukusanya, kisha Atahukumu baina yetu kwa haki, Naye Ndiye Hakimu, Mjuzi wa yote. [Sabaa (34): 26]

 

Na pia Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ ﴿١١٧﴾

Akasema: Rabb wangu! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.

 

فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١١٨﴾

Basi Hukumu baina yangu na baina yao hukumu (Yako), na Uniokoe mimi na wale walio pamoja nami miongoni mwa Waumini. [Ash-Shu’araa (26):  117-118]

 

 

 

الرَّزَّاقُ

Ar-Razzaaq

Mwingi Wa Kuwaruzuku Viumbe Vyote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewaruzuku waja Wake wote, hakuna kiumbe duniani isipokuwa Allaah (سبحانه وتعالى) hukipa rizki. Rizki Yake kwa waja Wake ni ya namna mbili:

 

 

i-Rizki ya ujumla ambayo hukunjuka kwa waja wema na watenda dhambi, wa kwanza mpaka wa mwisho. Hii ni rizki inayohitajika mwilini.

 

 

ii-Rizki mahususi. Hii hutolewa kwenye nyoyo, zinastawishwa kwa ‘ilmu na iymaan. Pia rizki ya halaal iliyoteuliwa kwa manufaa ya Dini, na hii ni mahsusi kwa Waumini na hugawanywa kulingana na daraja zao mbalimbali na kile inachokiamuru Hikmah na Rahmah Yake.

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۖ وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم مِّنْ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكُمْ وَإِيَّاهُمْ ۖ وَلَا تَقْرَبُوا الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ ۖ وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿١٥١﴾

Sema: Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote, na muwafanyie ihsaan wazazi wawili, na wala msiwaue watoto wenu kutokana na umasikini. Sisi Tunakuruzukuni pamoja nao. Na wala msikaribie machafu yaliyo dhahiri na yaliyofichika. Na wala msiue nafsi ambayo Ameiharamisha Allaah (kuiua) isipokuwa kwa haki (ya shariy’ah). Hivyo ndivyo Alivyokuusieni kwayo mpate kutia akilini. [Al-An’aam (6): 151]

 

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴿٥٦﴾

Na Sikuumba majini na wana Aadam isipokuwa waniabudu.

 

مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ ﴿٥٧﴾

Sitaki kutoka kwao riziki yoyote, na wala Sitaki wanilishe.

 

إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ ﴿٥٨﴾

Hakika Allaah Ndiye Mwingi wa kuruzuku, Mwenye nguvu Madhubuti.

[Adh-Dhaariyyat (51): 56-58]

 

 

الْحَكَمُ

Al-Hakam

Hakimu Mwadilifu Wa Haki Zaidi Kuliko Wote

 

 

 

الْعَدْلُ

Al-‘Adl

Mwadilifu Kuliko Wote

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewahukumu waja Wake humu duniani na Aakhirah kwa haki na uadilifu wake. Hatamdhulumu yeyote hata kwa uzito wa chembe ndogo kabisa ya hardali, na hakuna atakayebebeshwa mzigo wa mwingine. Hakuna mja atakayezidishiwa adhabu kuliko dhambi yake, atapewa anachostahiki tu. Hakuna haki ya mtu hata mmoja atakayonyimwa. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Mwadilifu katika Shariy’ah na amri Zake.

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنِّي تَوَكَّلْتُ عَلَى اللَّـهِ رَبِّي وَرَبِّكُم ۚ مَّا مِن دَابَّةٍ إِلَّا هُوَ آخِذٌ بِنَاصِيَتِهَا ۚ إِنَّ رَبِّي عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿٥٦﴾

Hakika mimi nimetawakali kwa Allaah, Rabb wangu na Rabb wenu. Hakuna kiumbe chochote kitembeacho isipokuwa Yeye (Allaah) Anamkamata kwa kipaji chake. Hakika Rabb wangu Yuko juu ya njia iliyonyooka. [Huwd (11): 56]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ إِنِّي عَلَىٰ بَيِّنَةٍ مِّن رَّبِّي وَكَذَّبْتُم بِهِ ۚ مَا عِندِي مَا تَسْتَعْجِلُونَ بِهِ ۚ إِنِ الْحُكْمُ إِلَّا لِلَّـهِ ۖ يَقُصُّ الْحَقَّ ۖ وَهُوَ خَيْرُ الْفَاصِلِينَ ﴿٥٧﴾

Sema: Hakika mimi niko juu ya hoja bayana kutoka kwa Rabb wangu nanyi mumeikadhibisha. Sina yale mnayoyahimiza. Hakuna hukumu isipokuwa ya Allaah Pekee. Anasimulia ya haki; Naye ni Mbora wa wenye kuamua hukumu. [Al-An’aam (6): 57]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

أَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَحْكَمِ الْحَاكِمِينَ ﴿٨﴾

Je, kwani Allaah Si Mwadilifu zaidi wa wanaohukumu kuliko mahakimu wote?   [At-Tiyn (95): 8]

 

 

 

 

جَامِعُ النَّاسُ

Jaami’un-Nas

Mwenye Kuwakusanya Watu

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Atakayewakusanya watu katika Siku isiyo na shaka. Atakusanya amali na malipo yao na Hataacha hata jambo moja, kubwa au dogo, bali Atalihesabu. Atayakusanya pamoja masalia ya waliofariki, wa mwanzo na wa baadaye kwa nguvu yake kamilifu na elimu izungukayo yote,  na kuwafufua.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

رَبَّنَا إِنَّكَ جَامِعُ النَّاسِ لِيَوْمٍ لَّا رَيْبَ فِيهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُخْلِفُ الْمِيعَادَ ﴿٩﴾ 

Rabb wetu! Hakika Wewe ni Mkusanyaji watu Siku isiyo na shaka ndani yake. Hakika Allaah Havunji miadi. [Aali ‘Imraan (3): 9]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ﴿١﴾

Naapa kwa siku ya Qiyaamah.

 

وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ﴿٢﴾

Na Naapa kwa nafsi inayojilaumu sana.

 

أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُ﴿٣﴾

Je, anadhani insani kwamba Hatutoikusanya mifupa yake?

 

 

بَلَىٰ قَادِرِينَ عَلَىٰ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُ﴿٤﴾

Ndio! Tuna uwezo wa  kusawazisha sawasawa ncha za vidole vyake .

 

 [Al-Qiyaamah (75): 1-4]

 

 

 

الْحَيُّ

Al-Hayyu

Aliye Hai Daima

 

 

الْقَيُّومُ

Al-Qayyuwm

Msimamizi Kila Jambo Milele

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Aliye na nguvu kamilifu, zipo za Kwake Mwenyewe na hamtegemei mwingine yoyote. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Mwenye kuruzuku wakazi wa mbinguni na ardhini, ni Pekee Anayedhibiti mambo yao na rizki zao. Jina Al-Hayyu linajumuisha Sifa zote za Nafsi Yake na Jina Al-Qayyuwm linajumuisha Sifa zote Matendo Yake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ ۚ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۖ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا ۚ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٢٥٥﴾

Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, Aliyehai daima, Msimamia kila kitu. Haumchukui usingizi wala kulala. Ni Vyake pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Nani huyu ambaye anashufai mbele Yake bila ya idhini Yake. Anajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Wala hawawezi kufikia kuelewa chochote kuhusu ujuzi Wake isipokuwa kwa Alitakalo. Imeenea Kursiyy Yake mbingu na ardhi. Wala hakumchoshi kuvihifadhi viwili hivyo. Naye ni Mwenye Uluwa; Ametukuka, Adhimu; Mkuu kabisa. [Al-Baqarah (2): 255]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

الم ﴿١﴾

Alif Laam Miym.

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ﴿٢﴾

Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, Aliye hai daima, Msimamia kila kitu.

 

 نَزَّلَ عَلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ وَأَنزَلَ التَّوْرَاةَ وَالْإِنجِيلَ ﴿٣﴾

Amekuteremshia Kitabu (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kwa haki kinachosadikisha yaliyo kabla yake na AkateremshaTawraat na Injiyl.

 

مِن قَبْلُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَأَنزَلَ الْفُرْقَانَ ۗ إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ اللَّـهِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ ۗ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ ﴿٤﴾

Kabla (ya kuteremshwa Qur-aan), iwe ni mwongozo kwa watu na Akateremsha pambanuo (la haki na batili). Hakika wale waliokufuru Aayaat za Allaah watapata adhabu kali. Na Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kuangamiza.

[Aali ‘Imraan (3): 1-4]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَعَنَتِ الْوُجُوهُ لِلْحَيِّ الْقَيُّومِ ۖ وَقَدْ خَابَ مَنْ حَمَلَ ظُلْمًا ﴿١١١﴾

Nyuso zitanyenyekea kwa Aliye Hai daima, Msimamizi wa kila kitu. Na kwa yakini ameharibikiwa abebaye dhulma. [Twaahaa (20): 111]

 

 

 

النُّورُ

An-Nuur

Mwenye Nuru, Mwanga

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Ana Nuru ya mbingu na dunia, ni Pekee Anayetia Nuru nyoyo za wanaomkhofu kwa ‘ilmu bila ya kumuona, bali wanamwamini na kutaraji mwongozo Wake. Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Aliyewasha angani na ardhini taa Alizoweka humo. Kizuizi Chake ni Nuru, na kama Angelikiondoa, basi Utukufu mkubwa na ubora wa Dhati Yake ingeunguza kila kiumbe ambacho uoni wake umekiangukia.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اللَّـهُ نُورُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَاةٍ فِيهَا مِصْبَاحٌ ۖ الْمِصْبَاحُ فِي زُجَاجَةٍ ۖ الزُّجَاجَةُ كَأَنَّهَا كَوْكَبٌ دُرِّيٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ مُّبَارَكَةٍ زَيْتُونَةٍ لَّا شَرْقِيَّةٍ وَلَا غَرْبِيَّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِيءُ وَلَوْ لَمْ تَمْسَسْهُ نَارٌ ۚ نُّورٌ عَلَىٰ نُورٍ ۗ يَهْدِي اللَّـهُ لِنُورِهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَيَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣٥﴾

Allaah ni Nuru ya mbingu na ardhi. Mfano wa Nuru Yake kama shubaka ndani yake mna taa yenye mwanga mkali. Taa hiyo yenye mwanga mkali iko katika (tungi la) gilasi. Gilasi hiyo ni kama kwamba nyota inayong’aa na kumeremeta, inawashwa kutokana na mti wa baraka wa zaytuni, hauko Mashariki wala Magharibi. Yanakaribia mafuta yake yang’ae japokuwa moto haujayagusa; Nuru juu ya Nuru. Allaah Anamwongoza kwa Nuru Yake Amtakaye. Na Allaah Anapiga mifano kwa watu. Na Allaah kwa kila kitu ni Mjuzi.   [An-Nuwr (24): 35]

 

 

 

بَدِيعُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ

Badiy’us-Samaawaat Wal-Ardhw

Mwanzishaji Wa Mbingu Na Ardhi

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni  Muumbaji na Mwanzilishi wa mbingu na ardhi. Amefanya hivyo katika namna bora kuliko zote na kwa maajabu zaidi ya uumbaji, yote katika namna ya ajabu na kamilifu zaidi, umbo na upatanifu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُ كُن فَيَكُونُ ﴿١١٧﴾

Mwanzilishi wa mbingu na ardhi. Anapokidhia jambo basi huliambia Kun! Basi nalo huwa. [Al-Baqarah (2): 117]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ أَنَّىٰ يَكُونُ لَهُ وَلَدٌ وَلَمْ تَكُن لَّهُ صَاحِبَةٌ ۖ وَخَلَقَ كُلَّ شَيْءٍ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿١٠١﴾

Mwanzilishi wa mbingu na ardhi. Inamkinikaje kuwa Yeye Ana mwana na hali hana mke! Naye Ameumba kila kitu, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi. [Al-An’aam (6): 101]

 

 

 

الْقَابِضُ

Al-Qaabidhw

Mwenye Kuchukua

 

 

الْبَاسِطُ

Al-Basitw

Mwenye Kukunjua

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayetoa rizki na roho. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayeruzuku burebure na anazipa uhai nyoyo. Yote haya ni kulingana na Hikmah na Rahmah Yake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّن ذَا الَّذِي يُقْرِضُ اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا فَيُضَاعِفَهُ لَهُ أَضْعَافًا كَثِيرَةً ۚ وَاللَّـهُ يَقْبِضُ وَيَبْسُطُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٢٤٥﴾

Ni nani atakayemkopesha Allaah mkopo mzuri kisha (Allaah) Amzidishie mzidisho mwingi. Na Allaah Anakunja na Anakunjua, na Kwake mtarejeshwa. [Al-Baqarah (2): 245]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا قَدَرُوا اللَّـهَ حَقَّ قَدْرِهِ وَالْأَرْضُ جَمِيعًا قَبْضَتُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَالسَّمَاوَاتُ مَطْوِيَّاتٌ بِيَمِينِهِ ۚ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَىٰ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٦٧﴾

Na hawakumkadiria Allaah kama inavyostahiki kumkadiria; na hali ardhi yote itatekwa Mkononi Mwake Siku ya Qiyaamah; na mbingu zitakunjwa Mkononi Mwake wa kulia. Subhaanahu wa Ta’aalaa (Utakasifu ni wa Allaah na Ametukuka kwa ‘Uluwa) kutokana na yale yote wanayomshirikisha. [Az-Zumar (39): 67]

 

 

 

الْمُعْطِي

Al-Mu’twiy

Mpaji

 

 

الْماَنِعُ

Al-Maani’u

Mwenye Kuzuia

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayetoa rizki na mahitaji ya waja Zake na Anayezuia. Hakuna wa kukizuia Anachokitoa na hakuna wa kikutoa Anachozuia. Kitu chochote chenye kuleta jema au manufaa hutafutwa na kutamaniwa kutoka Kwake. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye Anampa yeyote Amtakaye na kumzuia yeyote Amtakaye, yote haya kulingana na Hikmah na Rahmah yake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

كُلًّا نُّمِدُّ هَـٰؤُلَاءِ وَهَـٰؤُلَاءِ مِنْ عَطَاءِ رَبِّكَ ۚ وَمَا كَانَ عَطَاءُ رَبِّكَ مَحْظُورًا ﴿٢٠﴾

Wote hao Tunawakunjulia; hawa na hao katika hiba za Rabb wako. Na hazikuwa hiba za Rabb wako zenye kuzuiliwa. [Al-Israa (17): 20]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu Nabiy Sulaymaaan na du’a yake aliyoomba:

 

 

قَالَ رَبِّ اغْفِرْ لِي وَهَبْ لِي مُلْكًا لَّا يَنبَغِي لِأَحَدٍ مِّن بَعْدِي ۖ إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ ﴿٣٥﴾

Akasema: Rabb wangu! Nighufurie, na Nitunukie ufalme asiupate mtu yeyote baada yangu; hakika Wewe Ndiye Mwingi Wa kutunuku.

 

فَسَخَّرْنَا لَهُ الرِّيحَ تَجْرِي بِأَمْرِهِ رُخَاءً حَيْثُ أَصَابَ ﴿٣٦﴾

Basi Tukamtiishia upepo unaokwenda kwa amri yake pole pole popote anapotaka kufika.

 

وَالشَّيَاطِينَ كُلَّ بَنَّاءٍ وَغَوَّاصٍ ﴿٣٧﴾

Na mashaytwaan, kila ajengaye na mpiga mbizi.

 

وَآخَرِينَ مُقَرَّنِينَ فِي الْأَصْفَادِ ﴿٣٨﴾

Na wengineo, wafungwao minyororoni.

 

هَـٰذَا عَطَاؤُنَا فَامْنُنْ أَوْ أَمْسِكْ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿٣٩﴾

 (Tukasema) Hiki ni kipawa Chetu, basi toa au zuia bila ya hesabu. [Swaad (38): 35 - 39]

 

 

 

الشَّهِيدُ

Ash-Shahiyd

Shahidi Mwenye Kujua Vyema Yenye Kuonekana

Na Yasiyoonekana, Mwenye Kushuhudia

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayekijua kila kitu. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayesikia kila sauti kubwa na ya ukimya. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayeona kila kitu kisicho muhimu na kilicho muhimu, kidogo na kikubwa. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye ‘ilmu Yake inakizunguka kila kitu. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Atakayetoa ushahidi wa kutetea au dhidi ya waja Wake kwa yale waliyoyafanya.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ أَيُّ شَيْءٍ أَكْبَرُ شَهَادَةً ۖ قُلِ اللَّـهُ ۖ شَهِيدٌ بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ ۚ وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَـٰذَا الْقُرْآنُ لِأُنذِرَكُم بِهِ وَمَن بَلَغَ ۚ أَئِنَّكُمْ لَتَشْهَدُونَ أَنَّ مَعَ اللَّـهِ آلِهَةً أُخْرَىٰ ۚ قُل لَّا أَشْهَدُ ۚ قُلْ إِنَّمَا هُوَ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ وَإِنَّنِي بَرِيءٌ مِّمَّا تُشْرِكُونَ ﴿١٩﴾

Sema: Kitu gani ushahidi wake ndio mkubwa zaidi? Sema: Allaah; ni Mwenye kushuhudia yote baina yangu na baina yenu. Na nimefunuliwa Wahy hii Qur-aan ili nikuonyeni kwayo na kila itakayomfikia. Je, hivi nyinyi hakika mnashuhudia kwamba wako waabudiwa wengine pamoja na Allaah? Sema: Mimi sishuhudii (hayo). Sema: Hakika Yeye ni Mwabudiwa wa haki Mmoja (Pekee), na kwamba hakika mimi sihusiki na mnavyomfanyia shirki. [Al-An’aam (6): 19]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ كُلِّهِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا﴿٢٨﴾

Yeye Ndiye Aliyemtuma Rasuli Wake (Muhammad  (صلى الله عليه وآله وسلم kwa mwongozo na Dini ya haki ili Aishindishe juu ya dini zote. Na Allaah Anatosha kuwa ni Shahidi. [Al-Fath (48): 28]

 

 

الْمُبْدِئُ

Al-Mubdiu:

Mwanzishaji

 

 

 

الْمُعِيدُ

Al-Mu’iyd

Mrejeshaji

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye Ameanzisha uumbaji wa wana Aadam ili Awajaribu nani kati yao ni mwenye ‘amali njema kabisa, kisha Atawakusanya Siku ya Qiyaamah na kuwafanyia hesabu kwa kuwalipa jazaa zao wale waliotennda wema na kuwaadhibu wale waliotenda maovu. Pia ni Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee Ambaye Ameanzisha uumbaji wa ulimwengu na Akaumba kila kilichomo ndani ya dunia na Huendelea kuumba na kukariri uumbaji wa viumbe na vinginevyo.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِلَيْهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا ۖ وَعْدَ اللَّـهِ حَقًّا ۚ إِنَّهُ يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ لِيَجْزِيَ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ بِالْقِسْطِ ۚ وَالَّذِينَ كَفَرُوا لَهُمْ شَرَابٌ مِّنْ حَمِيمٍ وَعَذَابٌ أَلِيمٌ بِمَا كَانُوا يَكْفُرُونَ﴿٤﴾

Kwake ni marejeo yenu nyote. Ni ahadi ya Allaah ya kweli. Hakika Yeye Anaanzisha uumbaji, kisha Anaurejesha ili Awalipe kwa uadilifu wale walioamini na wakatenda mema. Na wale waliokufuru watapata kinywaji cha maji ya kuchemka, na adhabu iumizayo kwa yale waliyokuwa wakikufuru. [Yuwnus (10): 4]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَمَّن يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ وَمَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ ۗ أَإِلَـٰهٌ مَّعَ اللَّـهِ ۚ قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٦٤﴾

Au nani Anayeanzisha uumbaji, kisha Anaurejesha; na nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Je, yuko mwabudiwa pamoja na Allaah? Sema: Leteni ushahidi wenu wa wazi mkiwa ni wakweli. [An-Naml (27): 64]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

إِنَّهُ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ ﴿١٣﴾

Hakika Yeye Ndiye Anayeanzisha asili (ya uumbaji) na Atayerudisha. [Al-Buruwj (85): 13]

 

 

 

الْفَعَّالُ لِّمَا يُريدُ

Al-Fa’aalu Limaa Yuriyd

Mwenye Kufanya Atakacho

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Mwenye Kufanya Atakalo. Sifa hii ni kwasababu ya ukamilifu wa nguvu Yake na utekelezaji wa utashi na amri Yake kuwa kila kitu Anachotaka kukifanya, Anakifanya na kuwa hakuna wa kumzuia au kukataa. Hana msaidizi kwa kitu chochote Anachokifanya, bali Anapotaka jambo huliambia tu:

 

كُن فَيَكُونُ

Kun! basi (jambo) huwa!

 

Licha ya ukweli kuwa Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) hufanya Atakacho, utashi Wake unatenda kulingana na Hikmah Yake na Himdi. Amesifika kwa uwezo na nguvu kamili, na kwa utekelezaji wa utashi Wake na Ana Sifa ya kuwa na Hikmah kamili na yenye kukizunguka  kila kitu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَأَمَّا الَّذِينَ شَقُوا فَفِي النَّارِ لَهُمْ فِيهَا زَفِيرٌ وَشَهِيقٌ﴿١٠٦﴾

Basi ama wale walio mashakani, basi watakuwa motoni, lao humo ni upumuaji pumzi kwa mngurumo na uvutaji pumzi kwa mkoromo.

 

خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ ۚ إِنَّ رَبَّكَ فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ﴿١٠٧﴾

Ni wenye kudumu humo zitakavyodumu mbingu na ardhi isipokuwa Atakavyo Rabb wako. Hakika Rabb wako Anafanya Atakavyo.

 

وَأَمَّا الَّذِينَ سُعِدُوا فَفِي الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ ۖ عَطَاءً غَيْرَ مَجْذُوذٍ﴿١٠٨﴾

Na ama wale walio furahani, basi watakuwa katika Jannah, ni wenye kudumu humo zitakavyodumu mbingu na ardhi isipokuwa Atakavyo Rabb wako. Ni hiba isiyokatizwa. [Hud (11): 106-108]

 

 

 

الْغَنِيُّ

Al-Ghaniyy

Mkwasi Amejitosheleza, Hahitaji Lolote

 

 

 

الْمُغْنِي

Al-Mughniy

Mkwasi, Amejitajirisha

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Amejitosheleza kikamilifu pasi na kizuizi. Kushindwa kumeondolewa kwenye ukamilifu Wake na kwa Sifa Zake. Katu hana upungufu wa namna yoyote, haiwezekani kuwa Awe namna yoyote isipokuwa kujitosheleza, kwa sababu hali ya kujitosheleza inatokana na matokeo ya lazima ya Nafsi Yake. Kadhalika, ni muhali Kwake kuwa kitu kingine isipokuwa Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Muumbaji, Mwenye Nguvu Zote, Mpaji na Mwenye kuwakirimu waja wema. Allaah (سبحانه وتعالى) Hana haja ya kitu kwa yeyote. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Mwenye kujitosheleza Ambaye Mkononi Mwake ndipo kuna hazina za mbingu na ardhi, na hazina za duniani na Aakhirah. Amewatosheleza viumbe Wake wote na ni Mwenye kuwatosheleza Waumini katika viumbe Wake na katika hilo Anawatunikia nyoyoni mwao ‘ilmu ya kumjua Rabb wao na ukweli wa iymaan.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَوْلٌ مَّعْرُوفٌ وَمَغْفِرَةٌ خَيْرٌ مِّن صَدَقَةٍ يَتْبَعُهَا أَذًى ۗ وَاللَّـهُ غَنِيٌّ حَلِيمٌ ﴿٢٦٣﴾

Kauli njema na msamaha ni bora kuliko swadaqah inayoifuata udhia. Na Allaah ni Mkwasi, Mvumilivu. [Al-Baqarah (2): 263]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَرَبُّكَ الْغَنِيُّ ذُو الرَّحْمَةِ ۚ إِن يَشَأْ يُذْهِبْكُمْ وَيَسْتَخْلِفْ مِن بَعْدِكُم مَّا يَشَاءُ كَمَا أَنشَأَكُم مِّن ذُرِّيَّةِ قَوْمٍ آخَرِينَ ﴿١٣٣﴾

Na Rabb wako ni Mkwasi Mwenye rahmah. Akitaka Atakuondosheni na Aweke wengine watakaofuatia baada yenu kwa Atakao, kama vile Alivyokuzalisheni kutokana na vizazi vya watu wengine. [Al-An’aam (6): 133]

 

 

 

الْحَلِيمُ

Al-Haliym

Mpole Wa Kuwavumilia Waja

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewapa fadhila tele, za namna zote mbili, za nje na za ndani. Anawapa fadhila neema na rahmah viumbe Wake licha ya matendo yao mengi ya uasi na kuruka mipaka. Yeye Allaah (عز وجل) ni Mpole kwa wasiomtii, na Amewabainishia katika Kitabu Chake na Sunnah za Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) tahadharisho na kuwakanya   ili huenda wakatubu, na Anawapa  muda ili huenda wakawa wenye kurudi kutubia Kwake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي أَنفُسِكُمْ فَاحْذَرُوهُ ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿٢٣٥﴾

Na jueni kwamba Allaah Anajua yaliyomo katika nafsi zenu basi jihadharini Naye. Na jueni kwamba hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mvumilivu. [Al-Baqarah (2): 235]

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِن تُقْرِضُوا اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا يُضَاعِفْهُ لَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ۚ وَاللَّـهُ شَكُورٌ حَلِيمٌ﴿١٧﴾

Mkimkopesha Allaah karadhi nzuri, Atakuzidishieni maradufu, na Atakughufurieni. Na Allaah ni Mwenye kupokea shukurani, Mpole, Mvumilivu.  [At-Taghaabun (64): 17]

 

 

 

الشَّاكِرُ

Ash-Shaakir

Mwenye Kupokea Shukurani

 

 

الشَّكُورُ

Ash-Shakuwr

Mwingi Wa Shukrani,

Mwingi Wa Kukubali Kidogo Kwa Thawabu Tele

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayetambua na kutoa malipo kwa ajili ya amali ndogo na Ndiye Anayesamehe madhambi makubwa. Allaah (عز وجل) Ndiye Pekee Anayelipa maradufu waja Wake wanyoofu kwa kuwazidishia zaidi pasi na kipimo. Allaah (عز وجل) Ndiye Pekee Anayewatambua na kuwalipa wanaomshukuru na Anamkumbuka anayemdhukuru Yeye (عز وجل). Yeyote anayetafuta kuwa karibu Naye kwa kufanya amali njema, Allaah (عز وجل) Anasogea karibu yake kwa kiwango kikubwa.

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ ۖ فَمَنْ حَجَّ الْبَيْتَ أَوِ اعْتَمَرَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِ أَن يَطَّوَّفَ بِهِمَا ۚ وَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَإِنَّ اللَّـهَ شَاكِرٌ عَلِيمٌ ﴿١٥٨﴾

Hakika Asw-Swafaa na Al-Marwah ni katika alama za Allaah. Basi yeyote anayehiji kwenye Nyumba hiyo au akatekeleza ‘Umrah basi hakuna lawama kwake kutufu (vilima) viwili hivyo. Na atakayejitolea kufanya khayr basi hakika Allaah ni Mwenye kupokea shukurani, Mjuzi wa yote. [Al-Baqarah (2): 158]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّـهِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَّن تَبُورَ ﴿٢٩﴾

Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Allaah na wakasimamisha Swalaah, na wakatoa kutokana na yale Tuliyowaruzuku kwa siri na dhahiri wanataraji tijara isiyoteketea.

 

لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ ۚ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ ﴿٣٠﴾

Ili (Allaah) Awalipe ujira wao timilifu, na Awazidishie kutokana na fadhila Zake, hakika Yeye ni Mwingi wa kughufuria, Mwingi wa kupokea shukurani. [Faatwir (35): 29-30]

 

 

 

الْقَرِيبُ

Al-Qariyb

Aliye Karibu

 

 

الْمُجِيبُ

Al-Mujiyb

Mwenye Kuitikia

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Yuko karibu na kila mmoja, na ukaribu huo ni wa aina mbili:

 

 

i) Ukaribu wa kiujumla ambao unamaanisha kuwa Kwake karibu kwa kila mmoja kwa mujibu wa ‘ilmu Yake, utambuzi, kuona, kushuhudia na kuzunguka.

 

 

ii) Ukaribu mahsusi ambao ni maalumu kwa wanaomwabudu, wale wanaomwomba na wanaompenda. Ukweli wa aina hii ya ukaribu hauwezi kufahamika, bali tunachoweza kuona ni athari zake, ukarimu Wake kwa waja Wake, kuwasaidia Kwake na kule kuwafanya wawe imara katika Swiraatw Al-Mustaqiym (Njia iliyonyooka).

 

 

Kutokana na athari za ukaribu huu ni kuwapokelea maombi wale wanaomwomba, na kuwapa uwezo wa kuwa ni wenye kutubu. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Anayewaitikia, katika ufahamu wa ujumla, wanaomwomba, bila kujali ni akina nani, popote walipo na hali yoyote waliyonayo kama Alivyoahidi. Yeye Allaah (عز وجل) Ndiye Pekee Anawayewaitikia, katika ufahamu mahsusi, wale wanaompenda, wale wanaofuata Shariy‘ah. Pia Yeye Allaah (عز وجل) Ndiye anayeitikia katika haja kubwa na wale waliokata tamaa ya kuitikiwa na viumbe, na kwa hivyo muunganiko wao Kwake umetiwa nguvu kwa namna ya mapenzi, matumaini na khofu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu (kwa ujuzi); Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah (2): 186]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمْ صَالِحًا ۚ قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ ۖ هُوَ أَنشَأَكُم مِّنَ الْأَرْضِ وَاسْتَعْمَرَكُمْ فِيهَا فَاسْتَغْفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٌ مُّجِيبٌ﴿٦١﴾

Na kwa Thamuwd (Tulimpeleka) ndugu yao Swaalih. Akasema: Enyi kaumu yangu! Mwabuduni Allaah, hamna mwabudiwa wa haki ghairi Yake. Yeye Ndiye Aliyekuanzisheni katika ardhi, na Akakufanyieni makazi humo; basi mwombeni maghfirah, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu Yuko Karibu kwa ujuzi Wake, Mwenye kuitikia. [Huwd (11): 61]

 

 

 

 

الْكَافِي

Al-Kaafiy

Aliyejitosheleza

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayewatosheleza waja Wake katika kila kitu wanachokihitaji. Yeye Allaah (عز وجل) ni Pekee Anayewatosheleza, katika hali mahsusi, wanaomwamini Yeye na wanaomtegemea Yeye na wanahitaji mahitaji ya kidunia na ya kidini kutoka Kwake.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَرَدَّ اللَّـهُ الَّذِينَ كَفَرُوا بِغَيْظِهِمْ لَمْ يَنَالُوا خَيْرًا ۚ وَكَفَى اللَّـهُ الْمُؤْمِنِينَ الْقِتَالَ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ قَوِيًّا عَزِيزًا ﴿٢٥﴾

Na Allaah Akawarudisha nyuma wale waliokufuru kwa ghaidhi zao hawakupata kheri yoyote. Na Allaah Amewatosheleza Waumini vitani. Na Allaah daima ni Mwenye nguvu zote, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika. [Al-Ahzaab (33): 25]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَيْسَ اللَّـهُ بِكَافٍ عَبْدَهُ ۖ وَيُخَوِّفُونَكَ بِالَّذِينَ مِن دُونِهِ ۚ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَمَا لَهُ مِنْ هَادٍ﴿٣٦﴾

Je, kwani Allaah si Mwenye kumtosheleza mja Wake? Na wanakutisha na wale wasiokuwa Yeye? Na ambaye Allaah Amempotoa basi hana wa kumwongoa. [Az-Zumar (39): 36]

 

 

الأَوَّلُ

Al-Awwal

Wa Kwanza Bila Mwanzo

 

 

الآَخِرُ

Al-Aakhir

Wa Mwisho, Hapana Kitu Baada Yake

 

 

الظَّاهِرُ

Adhw-Dhwaahir

Dhahiri Kwa Vitendo Vyake

 

 

الْبَاطِنُ

Al-Baatwin 

Asiyeonekana Na Viumbe

 

 

 

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ameyaelezea Majina haya kwa maneno mafupi na dhahiri akisema:

 

 اللهُمَّ أَنْتَ الأَوَّلُ فَليْسَ قَبْلكَ شيء، وَأَنْتَ الآخِرُ فَليْسَ بَعْدَكَ شيء، وَأَنْتَ الظَّاهِرُ فَليْسَ فَوْقَكَ شيء، وَأَنْتَ البَاطِنُ فَليْسَ دُونَكَ شيء، اقْضِ عَنَّا الدَّيْنَ وَاغْنِنَا مِنَ الفَقْرِ

Ee Allaah, Wewe wa Awali hivyo basi hakuna kitu kabla Yako, Nawe ni wa Mwisho, basi hakuna kitu baada Yako, Nawe Uko juu kabisa hakuna kitu juu yako, Nawe uko karibu kabisa, hakuna kitu kilicho karibu kuliko Wewe, Nikidhie deni langu na nitosheleze kutokana na ufakiri. [Muslim]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣﴾

Yeye Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yake, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na Aliye juu kabisa hakuna kitu juu Yake, na Aliye karibu kabisa, hakuna kitu kilicho karibu kuliko Yeye, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi.  [Al-Hadiyd (57): 3]

 

 

الْواسِعُ

Al-Waasi’u

Aliyeenea

 

  

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Pekee Aliyeenea kwa mujibu wa Sifa Zake na ubora na yote yanayomhusu. Haya ni kwa mtazamo kuwa hakuna wa kuweza kutaja moja kwa moja sifa Zake kama Anavyostahiki, bali Yeye Allaah (عز وجل) Yuko sawa na Alivyojisia Yeye Mwenyewe. Allaah (عز وجل) Aliyeenea katika utukufu, na mamlaka, Aliyeenea katika kutoa Rahmah na mema, mkubwa katika utukufu.

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّثَلُ الَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ كَمَثَلِ حَبَّةٍ أَنبَتَتْ سَبْعَ سَنَابِلَ فِي كُلِّ سُنبُلَةٍ مِّائَةُ حَبَّةٍ ۗ وَاللَّـهُ يُضَاعِفُ لِمَن يَشَاءُ ۗ وَاللَّـهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ ﴿٢٦١﴾ 

Mfano wa wale wanaotoa mali zao katika njia ya Allaah ni kama mfano wa punje moja ya mbegu iliyotoa mashuke saba, katika kila shuke kuna punje mia. Na Allaah Humzidishia Amtakaye; na Allaah ni Mwenye wasaa, Mjuzi wa yote. [Al-Baqarah (2): 261]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَن يَرْتَدَّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ يَأْتِي اللَّـهُ بِقَوْمٍ يُحِبُّهُمْ وَيُحِبُّونَهُ أَذِلَّةٍ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ يُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَلَا يَخَافُونَ لَوْمَةَ لَائِمٍ ۚ ذَٰلِكَ فَضْلُ اللَّـهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَاللَّـهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ ﴿٥٤﴾

Enyi walioamini! Yeyote atakayeritadi miongoni mwenu kutoka Dini yake, basi Allaah Ataleta watu (badala yao) Atakaowapenda nao watampenda; wanyenyekevu kwa Waumini, washupavu juu ya makafiri; wanafanya jihaad katika njia ya Allaah na wala hawakhofu lawama za mwenye kulaumu. Hiyo ni fadhila ya Allaah Humpa Amtakaye. Na Allaah ni Mwenye wasaa, Mjuzi wa yote. [Al-Maaidah (5): 54]

 

 

الْهَادِي

Al-Haadiy

Mwenye Kuongoza

 

 

الرَّشِيدُ

Ar-Rashiyd

Mwenye Kuelekeza, Kuongoza

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Pekee Anayewaongoza na kuwaelekeza waja Wake kwenye yote ya manufaa na mbali na yenye kuwadhuru. Yeye Allaah (عز وجل) Ndiye Pekee Anayewafundisha kile wasichokijua hapo awali na Anawaongoza kwa mwongozo unaowahifadhi imara katika Swiraatw Al-Mustaqiym. (Njia iliyonyooka). Yeye Allaah (عز وجل) Ndiye Pekee Anayezitia msukumo nyoyo zao kwa taqwa na kuzifanya zitubie na kushikamana na amri Zake Allaah (عز وجل).

 

 

Jina la Ar-Rashiyd pia linabeba maana ya Al-Hakiym (Mwenye Hikmah). Yeye Allaah (عز وجل) ni Ar-Rashiyd katika Matendo Yake na Kauli Zake. Shariy’ah Zake zote ni nzuri, zimeongozwa vyema na zina Hikmah, pia uumbaji Wake una Hikmah.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَا لِكُلِّ نَبِيٍّ عَدُوًّا مِّنَ الْمُجْرِمِينَ ۗ وَكَفَىٰ بِرَبِّكَ هَادِيًا وَنَصِيرًا ﴿٣١﴾

Na hivyo ndivyo Tumemfanyia kila Nabiy adui miongoni mwa wakhalifu. Na Rabb wako Anatosheleza kuwa ni Mwenye kuongoza na Mwenye kunusuru. [Al-Furqaan (25): 31]

 

 

 

 

الْحَقُّ

Al-Haqq

Wa Haki, Wa Kweli

 

 

 

Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni wa Haki katika Nafsi Yake yote. Yeye Allaah (عز وجل) Ndiye muhimu kuliko vitu vyote. Yeye Ndiye anayehitajiwa na vitu. Allaah (عز وجل) Ana Sifa kamilifu. Yeye Ndiye Pekee hapo awali Aliyekuwa na sifa za utukufu, uzuri na ukamilifu mpaka sasa. Yeye Allaah (عز وجل) Ndiye Pekee aliyekuwa Mtukuka na hadi sasa.

 

 

Kauli Yake Allaah (عز وجل) ni kweli. Matendo Yake ni kweli, kukutana Naye ni kweli, Manabii Wake wake ni kweli, Vitabu vyake ni Kweli, Dini yake ni kweli, kumwabudu Yeye Peke Yake ni kweli, kila kinachomhusu Yeye ni kweli. Haya ni kwa sababu Allaah (عز وجل)  ndiye Kweli na vile wanavyoviomba ghairi Yake ni batili na kwasababu Allaah (عز وجل)  Ndiye wa juu kuliko wote, na Mkubwa Ametukuka kwa ‘Uluwa.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّـهَ هُوَ الْحَقُّ وَأَنَّهُ يُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَأَنَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٦﴾

Hivyo ni kwa kuwa Allaah Ndiye wa Haki, na kwamba Yeye Anahuisha wafu, na kwamba Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. [Al-Hajj (22: 6)]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ ۖ فَمَن شَاءَ فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاءَ فَلْيَكْفُرْ ۚ  

Na sema: Hii ni haki kutoka kwa Rabb wenu. Basi anayetaka aamini, na anayetaka akufuru.  [Al-Kahf (18): 29]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمُ الْحَقُّ ۖ فَمَاذَا بَعْدَ الْحَقِّ إِلَّا الضَّلَالُ ۖ فَأَنَّىٰ تُصْرَفُونَ﴿٣٢﴾

Basi Huyo Ndiye Allaah, Rabb wenu wa haki. Na kuna nini baada ya haki ila upotofu? Basi wapi mnageuzwa? [Yuwnus (10): 32]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

وَقُلْ جَاءَ الْحَقُّ وَزَهَقَ الْبَاطِلُ ۚ إِنَّ الْبَاطِلَ كَانَ زَهُوقًا ﴿٨١﴾

Na sema: Haki imekuja, na ubatili umetoweka. Hakika ubatili ni wenye kutoweka daima. [Al-Israa (17): 81]

 

 

 

Majina Mengineyo Na Sifa Ambazo Hazikutajwa Juu

 

 

الْعَالِمُ

Al-‘Aalim

Mjuzi

 

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَهُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ ۖ وَيَوْمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُ ۚ قَوْلُهُ الْحَقُّ ۚ وَلَهُ الْمُلْكُ يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ ۚ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ ۚ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ ﴿٧٣﴾

Naye Ndiye Ambaye Ameumba mbingu na ardhi kwa haki. Na Siku Atakaposema: Kun! basi (jambo) huwa! Kauli Yake ni haki.  Naye Atakuwa na ufalme Siku itakapopulizwa baragumu. Mjuzi wa ghayb na dhahiri. Naye ni Mwenye hikmah wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-An’aam (6): 73]

 

 

 

الْحَفِيُّ

Al-Hafiyy

Mwenye Kutoa Utukufu

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ سَلَامٌ عَلَيْكَ ۖ سَأَسْتَغْفِرُ لَكَ رَبِّي ۖ إِنَّهُ كَانَ بِي حَفِيًّا ﴿٤٧﴾

 (Ibraahiym) Akasema: Salaamun ‘Alayka. (Amani iwe juu yako). Nitakuombea maghfirah kwa Rabb wangu. Hakika Yeye daima ni Hafiyy kwangu (Mwenye kunihurumia sana). [Maryam (19): 47]

 

 

الأَكْرَمُ

Al-Akram

Mkarimu Kuliko Wote

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ ﴿٣﴾

Soma na Rabb wako ni Mkarimu kushinda wote.  [Al-‘Alaq (96): 3]

 

 

 

الإِلهُ

Al-Ilaah

Ilaah - Mwabudiwa Wa Haki

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 أَمْ كُنتُمْ شُهَدَاءَ إِذْ حَضَرَ يَعْقُوبَ الْمَوْتُ إِذْ قَالَ لِبَنِيهِ مَا تَعْبُدُونَ مِن بَعْدِي قَالُوا نَعْبُدُ إِلَـٰهَكَ وَإِلَـٰهَ آبَائِكَ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا وَنَحْنُ لَهُ مُسْلِمُونَ ﴿١٣٣﴾

Je, mlikuwa mashahidi wakati mauti yalipomfikia Ya’quwb alipowaambia wanawe: Mtaabudu nini baada yangu? Wakasema: Tutamwabudu Ilaaha wako (Allaah) na Ilaaha wa baba zako, Ibraahiym na Ismaa’iyl na Is-haaq; Ilaah Mmoja, nasi ni Waislamu (tunajisalimisha) Kwake. [Al-Baqarah (2): 133]

 

 

 

الْخَلاَّقُ

Al-Khallaaq

Muumbaji Wa Kila Namna Kwa Wingi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ﴿٨٦﴾

Hakika Rabb wako Ndiye Mwingi wa kuumba Atakavyo, Mjuzi wa yote. [Al-Hijr (15): 86]

 

 

 

الْمَلِيكُ

Al-Maliyk

Mfalme Mwenye Nguvu Daima

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ ﴿٥٤﴾

Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na mito.  

 

فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ ﴿٥٥﴾

Katika makao ya haki kwa Mfalme Mwenye nguvu zote, Mwenye uwezo wa juu kabisa. [Al-Qamar (54): 54-55]

 

 

 

الْمُبِينُ

Al-Mubiyn

Mwenye Kubainisha

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَوْمَئِذٍ يُوَفِّيهِمُ اللَّـهُ دِينَهُمُ الْحَقَّ وَيَعْلَمُونَ أَنَّ اللَّـهَ هُوَ الْحَقُّ الْمُبِينُ ﴿٢٥﴾

Siku hiyo Allaah Atawalipa kikamilifu malipo yao ya haki; na watajua kwamba Allaah Ndiye wa Haki, Mwenye kubainisha. [An-Nuwr (24): 25]

 

 

             الْمَوْلى

Al-Mawlaa

Maula, Bwana Mlezi, Msaidizi, Msimamizi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا ۚ رَبَّنَا وَلَا تَحْمِلْ عَلَيْنَا إِصْرًا كَمَا حَمَلْتَهُ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِنَا ۚ رَبَّنَا وَلَا تُحَمِّلْنَا مَا لَا طَاقَةَ لَنَا بِهِ ۖ وَاعْفُ عَنَّا وَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا ۚ أَنتَ مَوْلَانَا فَانصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ ﴿٢٨٦﴾  

Rabb wetu Usituchukulie tukisahau au tukikosea. Rabb wetu, Usitubebeshe mzigo kama Ulivyoubebesha juu ya wale waliokuwa kabla yetu. Rabb wetu, Usitutwike tusiyoyaweza, na Tusamehe, na Tughufurie na Turehemu, Wewe ni Mola Mlinzi wetu, basi Tunusuru dhidi ya watu makafiri. [Al-Baqarah (2): 286]

 

 

 

            الْمُقْتَدِرُ

Al-Muqtadir

Mwenye Uwezo Wa Juu Kabisa

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَاضْرِبْ لَهُم مَّثَلَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا كَمَاءٍ أَنزَلْنَاهُ مِنَ السَّمَاءِ فَاخْتَلَطَ بِهِ نَبَاتُ الْأَرْضِ فَأَصْبَحَ هَشِيمًا تَذْرُوهُ الرِّيَاحُ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقْتَدِرًا ﴿٤٥﴾

Na wapigie mfano wa uhai wa dunia kama maji Tuliyoyateremsha kutoka mbinguni, yakachanganyika kwayo mimea ya ardhi (ikasitawi), kisha yakawa makavu yaliyovurugika yanapeperushwa na upepo. Na Allaah daima ni Mwenye Uwezo wa juu kabisa kwa kila kitu. [Al-Kahf (18): 45]

 

 

 

 

              الْمُتَعَالُ

Al-Muta’aal

Mwenye ‘Uluwa Na Taadhima

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْكَبِيرُ الْمُتَعَالِ ﴿٩﴾

Mjuzi wa ghayb na dhahiri, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa, Mwenye Uluwa Aliyejitukuza kabisa. [Ar-Ra’d (13): 9]

 

 

 

الْقَادِرُ

Al-Qaadir

Mwenye Uwezo

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ هُوَ الْقَادِرُ عَلَىٰ أَن يَبْعَثَ عَلَيْكُمْ عَذَابًا مِّن فَوْقِكُمْ أَوْ مِن تَحْتِ أَرْجُلِكُمْ أَوْ يَلْبِسَكُمْ شِيَعًا وَيُذِيقَ بَعْضَكُم بَأْسَ بَعْضٍ ۗ انظُرْ كَيْفَ نُصَرِّفُ الْآيَاتِ لَعَلَّهُمْ يَفْقَهُونَ ﴿٦٥﴾

Sema: Yeye ni Muweza wa kukuleteeni adhabu kutoka juu yenu, au kutoka chini ya miguu yenu, au Akutatanisheni mfarikiane kuwa makundi na Akuonjesheni baadhi yenu (vurugu la) nguvu za wengineo. Tazama jinsi Tunavyosarifu namna kwa namna Aayaat wapate kufahamu. [Al-An-‘Aam (6): 65]

 

 

              الْوارِثُ

Al-Waarith

Mrithi Kwa Kuondosha Viumbe Wote Na Kubaki Yeye Tu

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْيِي وَنُمِيتُ وَنَحْنُ الْوَارِثُونَ﴿٢٣﴾

Na hakika Sisi Tunahuisha na Tunafisha; na Sisi ndio Warithi. [Al-Hijr (15): 23]

 

 

 

  الْوَلِيُّ

Al-Waliyyu

Walii, Aliye Karibu

 

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَمِ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ ۖ فَاللَّـهُ هُوَ الْوَلِيُّ وَهُوَ يُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿٩﴾

Je, wamejichukulia badala Yake walinzi? Basi Allaah Yeye Ndiye Mlinzi, Naye Ndiye Anayehuisha wafu, Naye Ndiye juu ya kila kitu ni Muweza. [Ash-Shuwraa (42): 9]

 

 

            النَّصِيرُ

An-Naswiyr

Mwenye Kunusuru, Msaidizi

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّـهَ لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۗ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ اللَّـهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ ﴿١٠٧﴾

Je, hujui kwamba Allaah Ana ufalme wa mbingu na ardhi. Nanyi hamna pasi na Allaah mlinzi yeyote wala mwenye kunusuru. [Al-Baqarah (2): 107]

 

 

 

[1] ‘Aliy Hasan: Imesimuliwa na Is-haaq, As-Siyrah, Atw-Twabariy., Taaryikh na vingine na Hadiyth hii si Swahiyh kwa mukhutasari.

 

[2] ‘Aliy Hasan: Imesimuliwa na Atw-Twabariy, Al-Kabiyr (8886) na wengine na imetolewa kuwa Swahiyh na Ibn Taymiyyah, Majmuw’ Fataawaa (6/3910).

 

[3] Imefupishwa kutoka Ibn ‘Uthaymiyn, Qawa-idul-Muthlaa fiy SwifaatiLLaah wa Asmaaihil-Husnaa

 

[4] Iythaar Al-Haqq ‘Alal-Khalq (uk. 219 +) ya Al-Yamaniy pamoja na mukhtasari, kama kilivyonukuliwa katika Sharh Kitaab At-Tawhid min Swahiyh Al-Bukhaariy (1/86+) cha Shaykh ‘Abdullah Al-Ghunaymaan.

 

Share