Uswuwl Al-Fiqhi

 

Uswuwl Al-Fiqh

 

Imetafsiriwa na: Naaswir Haamid

 

Utangulizi Wa Alhidaaya.com

 

 

BismiLLaah wasw-swalaatu was-salaamu 'alaa RasuuliLLaah wa aalihi wa-aswhaabihi wa ba'ad,

 

Tumeona umuhimu mkubwa wa kukitafsiri kitabu hichi kutoka somo la Uswuul Al-Fiqhi kwani wasomi wengi, Mashaykh na wanafunzi wa Dini wamekuwa hawanufaiki vilivyo na kitabu hichi kwa kukosekana elimu hii kwa lugha ya kiswahili. Hivyo, tunatarajia kwamba kitabu hichi In shaa Allaah kiwe na manufaa makubwa haswa kwa wenye uchu wa kutafuta elimu pamoja na Mashaykh kwani ni somo muhimu linalosakwa sana na watafutaji elimu.

 

Hali kadhalika maelezo yaliyomo ndani ya kitabu hichi ni mepesi kuyasoma na kuyaelewa kwani yapo kwa utangulizi na kitabu hichi hakijaenda ndani sana kuhusiana na somo hilo la Uswuul.

 

Ni materejeo yetu kwamba kutokana na tafsiri hii, itapatikana faraja kwa wasomi pamoja na kupatikana usomaji uliotanuka kwa wanafunzi wa Uswuul.

 

Na bila shaka hiki ndicho kitabu cha kwanza cha somo la Uswuul al-Fiqhi kufasiriwa kwa lugha ya kiswahili. Tunaamini In shaa Allaah Waislam wengi watanufaika kwa kazi hii na yaliyomo ndani yake.

 

Allaah Amlipe ndugu yetu mfasiri wa kitabu hiki kwa Kiswahili, Al-Akh Naaswir Haamid. Tusiwasahau kwa du'aa In shaa Allaah wahusika wa ALHIDAAYA ambao wameisimamia kazi hii.

 

Alhidaaya.com

 

 

Share