60-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Kitabu Chake (Qur-aan) Kimepewa Majina Na Sifa Kadhaa

 

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

60-Kitabu Chake (Qur-aan) Kimepewa Majina Na Sifa Kadhaa

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Al-Qur-aan aliyoteremshiwa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ina Majina na Sifa kadhaa. Miongoni mwayo ni Uhai, Burhani (dalili za wazi) na Nuru. Majina na Sifa hizo Amezitaja Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan kwenye Aayah mbali mbali; mfano wa Kauli Zake Allaah (سبحانه وتعالى) ni: 

 

يَا أَهْلَ الْكِتَابِ قَدْ جَاءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَيِّنُ لَكُمْ كَثِيرًا مِّمَّا كُنتُمْ تُخْفُونَ مِنَ الْكِتَابِ وَيَعْفُو عَن كَثِيرٍ ۚ قَدْ جَاءَكُم مِّنَ اللَّـهِ نُورٌ وَكِتَابٌ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾

Enyi Ahlal-Kitaab! Hakika amekwishakujieni Rasuli Wetu anayekubainishieni mengi katika yale mliyokuwa mkiyaficha katika Kitabu, na anasamehe mengi. Kwa yakini imekufikieni kutoka kwa Allaah Nuru na Kitabu kinachobainisha. [Al-Maaidah: 15]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَكُم بُرْهَانٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَأَنزَلْنَا إِلَيْكُمْ نُورًا مُّبِينًا ﴿١٧٤﴾

Enyi watu!  Kwa yakini imekujieni burhani kutoka kwa Rabb wenu na Tumekuteremshieni Nuru bayana.  [An-Nisaa: 174]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَالنُّورِ الَّذِي أَنزَلْنَا ۚ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ﴿٨﴾

Basi muaminini Allaah na Rasuli Wake na Nuru (Qur-aan) Tuliyoiteremsha, na Allaah kwa yale myatendayo ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [At-Taghaabun: 8]

 

 

Na kuhusu Uhai Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ رُوحًا مِّنْ أَمْرِنَا ۚ مَا كُنتَ تَدْرِي مَا الْكِتَابُ وَلَا الْإِيمَانُ وَلَـٰكِن جَعَلْنَاهُ نُورًا نَّهْدِي بِهِ مَن نَّشَاءُ مِنْ عِبَادِنَا ۚ وَإِنَّكَ لَتَهْدِي إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿٥٢﴾ صِرَاطِ اللَّـهِ الَّذِي لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ أَلَا إِلَى اللَّـهِ تَصِيرُ الْأُمُورُ﴿٥٣﴾

Na hivyo ndivyo Tulivyokuletea Ruwh (Qur-aan) kutoka amri Yetu. Hukuwa uajua nini Kitabu wala iymaan, lakini Tumeifanya ni Nuru, Tunaongoa kwayo Tumtakaye miongoni mwa waja Wetu. Na hakika wewe (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) bila shaka unaongoza kuelekea njia iliyonyooka. Njia ya Allaah Ambaye ni Vyake Pekee vyote vilivyomo mbinguni na vyote vilivyomo ardhini. Tanabahi! Kwa Allaah Pekee yanaishia mambo yote. [Ash-Shuwraa: 52-53]

 

 

Baadhi Ya Majina Na Sifa Za Qur-aan:

 

 

Al-Kitaab

الكتاب

Al-Furqaan

الفرقان

An-Nuwr

النور

Ar-Ruwh

الروح

Al-Hadiyth

الحديث

Al-Burhaan

البرهان

Ar-Rahmah

الرحمة

At-Tanziyl

التنزيل

Adh-Dhikr

الذّكر

Al-Kalaam

الكلام

Al-Maw’idhwah

الموعظة

Al-Haadiy

الهادي

Al-Mubaarak

المبارك

Al-Haqq

الحق

Al-Bayaan

البيان

Al-Muniyr

المنير

Ash-Shifaa

الشفاء

Al-‘Adhwiym

العظيم

Al-Kariym

الكريم

Al-Majiyd

المجيد

Al-‘Aziyz

العزيز

Al-Bashiyr

البشير

Al-Muhaymin

المهيمن

An-Ni’mah

النعمة

Al-Qaswasw

القصص

As-Siraaj

السراج

Al-Habl

الحبل

Al-Hukm

الحكم

At-Tibyaan

التبيان

An-Nadhiyr

النذير

Al-Hakiym

الحكيم

Adh-Dhikraa

الذكرى

Al-Miyzaan

الميزان

At-Tadhkirah

التذكرة

Al-Yaqiyn

اليقين

Ahsanul-Hadiyth

احسن الحديث

Al-Mathaaniy

المثاني

Al-Kitaab Al-Mutashaabihah

الكتاب المتشابه

Al-Qayyim

القيّم

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share