Biskuti Za Mayai

 

Biskuti Za Mayai

 

Vipimo

 

Unga  3 Vikombe

Sukari ya unga (icing sugar) 1 Kikombe

Siagi 250 gm

Mayai   3

Vanilla  2 Vijiko vya chai

Baking powder 1 Kijiko cha chai

 

Namna Ya  Kutayarisha Na Kupika

  1. Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe  laini (creamy).
  2. Tia mayai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini.
  3. Tia unga na baking powder changanya na mwiko.
  4. Tengeneza round upange kwenye tray utie nukta ya rangi.
  5. Nyunyuzia sukari juu ya hizo round ulizotengeneza kabla huja choma.
  6. Pika (bake) katika oven moto wa 350°F kama muda wa dakika 15 hivi huku
  7. unazitazama tazama.

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 

 

 

Share