111-Al-Masad: Utangulizi Wa Suwrah

 

111-Al-Masad: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com

 

 

Imeteremka: Makkah kwa itifaki ya ‘Ulamaa.

 

Idadi Za Aayah: 5

 

Jina La Suwrah: Al-Masad

 

Suwrah imeitwa Al-Masad (Msokoto Madhubuti), na inayodalilisha ni kutajwa kwake katika Aayah namba (1).

 

Miongoni Mwa Makusudio Ya Suwrah:

 

1-Kubainisha khasara aliyoipata Abuu Lahb pamoja na mkewe. [Al-Mukhtaswar Fiy Tafsiyr Al-Qur-aan Al-Kariym]

 

2-Kutaja dhulma ya Abuu Lahab na mkewe waliomfanyia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na kubainishwa adhabu zao.

 

Miongoni Mwa Maudhui Ya Suwrah:

 

Suwrah imeelezea khasara ya Abuu Lahab na kuangamia kwake pamoja na mkewe na kupata khasara, kwa sababu ya kumfanyia maudhi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم). Ikatajwa kwamba mali ya Abuu Lahab haikuweza kumnufaisha katika kumkinga na Adhabu ya Allaah. Basi ameahidiwa yeye kuingizwa moto uwakao vikali mno! Na mkewe, ambaye alikuwa akibeba miba na kuiweka katika njia anayopita Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ili imchome na kumjeruhi, ameahidiwa kuingia motoni akiwa amefungwa shingoni mwake, kuti kavu la mtende lililo madhubuti, abebwe nalo kwenye moto wa Jahannam, kisha arushwe nalo mpaka chini humo.

 

 

 

Share