08-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Mavazi Na Mapambo Na Hukmu Za Kuangalia: Hukumu Za Kuangalia: Mwanamke Anaruhusiwa Kumtembelea Mwanaume Mgonjwa Kwa Sharti Ajisitiri Na Pasiwepo Fitnah

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ اللِّبَاسِ وَالزِّيْنَةِ  وَأَحْكَامُ النَّظَرِ

 

 Kitabu Cha Mavazi Na Mapambo Na Hukmu Za Kuangalia 

 

 

أَحْكَامُ النَّظَرِ

Hukumu Za Kuangalia 

 

  

Alhidaaya.com 

 

 

08-Mwanamke Anaruhusiwa Kumtembelea Mwanaume Mgonjwa Kwa Sharti Ajisitiri Na Pasiwepo Fitnah:

 

‘Aaishah:

 

"لَمَّا قَدِمَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الْمَدِينَةَ وُعِكَ أَبُو بَكْرٍ وَبِلاَلٌ ، فَدَخَلْتُ عَلَيْهِمَا فَقُلْتُ: يَا أَبَتِ كَيْفَ تَجِدُكَ؟ وَيَا بِلاَلُ كَيْفَ تَجِدُك؟َ"

 

“Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuja Madiynah, Abu Bakr na Bilaal walipigwa na homa.  Nikaingia waliko nikasema:  Ee baba yangu kipenzi! Vipi hali yako? Wajisikiaje? Na ee Bilaal! Vipi hali yako? Wajisikiaje?....”[Al-Bukhaariy (3926) na Muslim (1376), na tamshi ni la Al-Bukhaariy].

 

Vile vile, mwanamke anaruhusiwa kumtibu mwanaume kama kuna dharura.  Ni kwa Hadiyth iliyotangulia ya Ar-Rubayyi’u bin Mu’awwidh aliyesema: 

 

"كُنَّا نَغْزُو مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ نَسْقِي الْقَوْمَ، وَنُدَاوِيْ الْجَرْحَى وَنَرُدُّ القَتْلَى إِلَى الْمَدِينَةِ"

 

“Tulikuwa tunakwenda vitani pamoja na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na tulikuwa tunawapatia maji wanaume, tunawatibu majeruhi, na tunawarejesha waliouawa Madiynah”.  [Swahiyh Al-Bukhaariy (2883)]

 

Lakini sharti ya hili ni kutopatikana mwanaume anayeweza kutoa huduma hii ya matibabu.  Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.

 

 

 

Share