033-Maswali 200 Na Majibu Ya ‘Aqiydah: Ni Ipi Dalili Ya Hajj?

 

 

200 سُؤالٌ وَ جَوَابٌ فِي الْعَقِيدَة

Maswali 200 Na Majibu Ya ‘Aqiydah

 

لِلشَّيخ حافِظ بن أحْمَد الحَكمَيّ

Shaykh Haafidhw Bin Ahmad Al-Hakamiyy (رحمه الله)

Imefasiriwa na:  Alhidaaya.com

 

033-Ni Ipi Dalili Ya Hajj?

 

 

 

Swali:

 

Ni ipi dalili ya Hajj?

س: ما دليل الحج  

Jibu:

 

ج: قال الله تعالى( وأتموا الحج والعمرة لله )وقال تعالى( ولله على الناس حج البيت من استطاع إليه سبيلا )وقال النبي صلى الله عليه وسلم( إن الله تعالى كتب عليكم الحج )الحديث في الصحيحين وتقدم حديث جبريل وحديث( بني الإسلام على خمس )وغيرها كثير.

 

Ni kauli ya Allaah(سبحانه وتعالى):

وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ ۚ 

Na timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah. [Al-Baqarah: (2:196)]

 

Na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ۚ  ﴿٩٧﴾ 

Na kwa ajili ya Allaah imewajibika watu watekeleze Hajj katika nyumba (Al-Ka’bah) hiyo kwa mwenye uwezo. [Aal-'Imraan: (3:97)]

 

Na kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema:

 

( إن الله تعالى كتب عليكم الحج )

"Hakika Allaah amekufaradhishieni nyinyi Hajj". (Hadiyth ipo katika Swahiyh mbili. Bukhaariy na Muslim).[Imepokewa na Al-Bukhaariy katika Kitaabul-Iymaan mlango wa Zakkah (46), Muslim (11) katika Hadiyth ya Twalha Ibn ‘Ubaydullah]

 

Na Hadiyth ya Jibriyl imetangulia kuelezea na Hadiyth kuhusiana na:

 ( بني الإسلام على خمس )

"Uislamu umejengwa kwa nguzo tano".

 

 

Share