08-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Wasia kwa wasiorithi katika ndugu na jamaa wa karibu

 
Wasia kwa wasiorithi katika ndugu na jamaa wa karibu:
 
 
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) amesema, “Mnalazimishwa mmoja wenu anapofikwa na mauti, kama akiacha mali kufanya wasia kwa wazazi (wake) na jamaa (zake) kwa namna nzuri inayokubaliwa na Sheria. Ni wajibu haya kwa wamchao Mungu.” (2:180)
 
Katika aya hii ni wajibu kuusia kwa kiasi cha mali kwa jamaa wa karibu ikiwa mtu huyo ni mwenye wasaa na uwezo wa hilo.
 
Share