Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti
'DALILI ZA KHERI KATIKA MAMBO YAMFAAYO MAITI'
MWANDISHI: MAHMUUD BIN AL-JAMIYL
MFASIRI: SA'IYD BAAWAZIR
UTANGULIZI:
Shukrani ni za Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala), swala na salamu zimwendee Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) Aali zake, sahaba zake na wote wenye kufuata uongofu na njia yake.
Risala hii fupi yenye kubainisha mambo yanayomfaa maiti katika kaburi lake na akhera yake kwa idhini ya Mola wake. Risala hii inakusanya mambo yote yenye kufanywa na watu wanaomhusu maiti na kwa wenye kumtakia kheri maiti wao katika walio hai. Hali kadhalika inakusanya baadhi ya yanayotakiwa kufanywa na mtu aliye hai kwa ajili ya nafsi yake ili imnufaishe yeye kwa Mwenyezi Mungu baada ya kifo chake.
Katika risala hii nimetanabahisha baadhi ya matendo na amali ambazo hazimfai maiti bali si hivyo tu huenda amali hizo zikamdhuru ikiwa amefanya kabla ya kifo chake au kutoka kwa jamaa zake anapokuwa katika sakarati mauti na baada ya kifo chake.
Baada ya hayo sala na salamu kwa Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) aali zake, sahaba zake na Alhamdulillah Rabil a’lamiin.
»
- Login or register to post comments
- Email this page


