18-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Kuichelewesha Zakaatul-Fitwr

 Kuichelewesha Zakaatul-Fitwr

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

Nilikuwa katika safari na nikasahau kutoa Zakaatul-Fitwr. Nikuwa nasafiri usiku wa 27 Ramadhwaan na hatukutoa Zakaatul-Fitwr hadi leo.

 

JIBU:

 

 

 

Ikiwa mtu amechelewesha Zakaatul-Fitwr japokuwa alikumbukua kuitoa, basi atakuwa ni mtenda dhambi na itampasa atubie kwa Allaah na kuilipa kwa sababu ni kitendo cha ibada ambacho kinabakia kuwajibika japokuwa muda wa kutoa umepita kama mfano wa Swalaah. Lakini kama muulizaji huyu alivyotaja kuwa alisahau kuilipa kwa wakati wake, hivyo hakuna dhambi juu yake lakini lazima ailipe.

Kusema kuwa hakuna dhambi juu yake ni maana kwa ujumla kutokana na dalili inayoonyesha kuwa hakuna dhambi kwa mtu anayesahau lakini bado atakuwa amewajibika kuilipa kutokana na sababu zilizotolewa juu.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah  (2867)]

 

 

Share