19-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Kuongeza Kitu Ziada Katika Zakaatul-Fitwr

  Kuongeza Kitu Ziada Katika Zakaatul-Fitwr

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Je, Zakaatul-Fitwr imewekewa mipaka ya swaa’aa moja kwa kila mtu mmoja katika familia yangu bila ya kuongeza kitu zaidi? Nnachomaanisha ni kwamba kuiongezea sadaka ili nibakie katika usalama wa shaka kwamba saa' yangu imetosheleza. Kufanya hivyo bila ya kumwambia maskini nnayempa kwamba hiyo ziada ni sadaka. Mfano nnao watu kumi katika familia lakini nikanunua gunia la mchele ambalo lina kilo khamsiyn kisha nikalitoa lote kama ni Zakaatul-Fitwr kwa ajili ya watu kumi bila ya kuhesabu swaa’aa kwa kila mmoja kwa sababu najua kuwa huo mchele una zaidi ya kilo ishirini ziada nikizitilia nia kuwa ni sadaka na bila ya kuwaambia kuwa hiyo ziada ni sadaka bali niseme: "Pokeeni Zakaatul-Fitwr yetu" hivyo hatojua mtu kama gunia hilo lina zaidi ya kiwango cha Zakaah, hivyo achukue na afurahie. Nini hukmu yake?

 

JIBU:

 

 

Zakaatul-Fitwr ni swaa’aa moja ya ngano au tende, au mchele n.k. ambayo ni chakula kinachotumika na watu katika mji. Nayo ni kwa ajili ya mtu mmoja mwanamume au mwanamke, mkubwa au mdogo.

Hakuna ubaya kuzidisha Zakaatul-Fitwr kama ulivyofanya kwa nia ya kutoa ziaida kama ni sadaka japokuwa hutowaambia.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah (9386)]

 

 

Share