Siku Za Kiislamu Zinaazia Saa Ngapi?
SWALI:
siku kwa waislam inaanza na kwisha saa ngapi?
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Swali lako la kwanza ni kwamba siku za Kiislamu zinaanza kuhesabika jua linapozama yaani wakati wa Magharibi hivyo kama mfano leo ni siku ya Alkhamiys na Magharibi inapoingia, basi usiku huo huitwa tena Laylatul-Jumu'ah (Usiku wa Ijumaa) na hali kadhalika kwa masiku mengine.
Na si saa sita ya usiku kama ilivyo hali ya siku au tarehe za ki-Gregorian ambayo ni marekebisho ya tarehe zilizokuwa zikijulikana zamani
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
