Skip navigation.
Home kabah

Nini Tofauti Ya Mitihani Ya Binaadamu Na Mitihani Ya Allaah?

Mitihani ya Binaadamu

Mitihani ya Allah

 

Inahitajika kusoma vitabu vingi na mwanafunzi inambidi afanye juhudi kubwa na mashaka kusoma hadi apasi mitihani yake

 

 

Kitabu kimoja tu  chepesi kukisoma nacho ni Qur-aan

 

Mitihani ya binaadamu haijulikani ni maswali yepi yatakayokuja kabla ya mitihani

 

Maswali tayari yameshajulikana kama;

Nani Mola Wako

Ipi Dini Yako

Nani Mtume wako?

Umeutumiaje ujana wako?

Umeipata vipi mali yako na umeitumiaje?

Umri wako umeutumia vipi?

Elimu yako umeitumiaje?

 

 

Hupewi majibu kabla ya mitihani

 

Unapewa majibu tayari hapo hapo unaweza kujua vipi kuyapata na kuyafanyia kazi.

 

Waalimu waliochaguliwa kufundisha masomo ya mitihani hiyo wanaweza kukosea

 

Waalimu waliochaguliwa na Allaah kusimamia na kufundisha mitihani, ni Ma’aswumiyn (Wamelindwa na makosa) [nao ni Mitume]

 

Muda wa mitihani haizidi masaa

 

Muda wa mitihani unaweza kufika hadi miaka 70 au zaidi ambao ni umri wa mwana Aadam!

 

Fursa ya kurudia mtihani baada ya kufeli ni mara chache tu, hata hivyo hakuna dhamana kuwa ndio kufuzu

Fursa ya kurudia mtihani ipo wazi hadi kabla ya mauti ya bin Aadam na dhamana ya kufuzu ipo madamu tu utajaribu!

 

Daraja unayopewa haizidi 100%

Daraja yake kubwa ni 700 na Allaah Huzidisha zaidi Atakavyo

 

Matokeo yake yaani kufuzu kwake ni ya kidunia pekee

Matokeo/kufuzu kwake ni duniani na Akhera pia.

 

Husahau mtihani baada ya muda

Hausahauliki kwani umehifadhika katika Lawhum Mahfuudh (ubao uliohifadhiwa)

 

Zawadi yake ni karatasi na wino (shahada) ambayo itatoweka tu

 

Zawadi yake ni Pepo ya kudumu daima bila ya kubadilika hali yake

Inabidi utoke uende masafa shuleni au chuoni

 

Unaweza kufanya mtihani ukiwa nyumbani kwako kwa kufanya ibada na kuomba ufuzu

Wakati au tarehe yake ni fulani tu

 

Wakati wowote, siku yoyote katika uhai wako

Masikini anaweza asijimudu kulipia mtihani

 

Masikini au fakiri wote wanaweza kutekeleza mtihani wa Allah

Kunaweza kutokea upendeleo akadhulumiwa bina Aadam asipewe natija anayostahiki

 

Hadhulumiwi mtu hata chembe ya khardal, atalipwa bin Aadam kila kitu!

Kwa hiyo ni maajabu makubwa kwa mtu kufuzu mitihani ya Binaadamu na kufeli mitihani ya Mola Mtukufu!