26-Hadiyth Al-Qudsiy: Usijfanye Duni Kwa Kuogopa Watu Kusema Jambo Kwani Allah Ana Haki Zaidi Ya Kuogopwa

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 26  

Usijfanye Duni Kwa Kuogopa Watu Kusema Jambo Kwani Allah Ana Haki Zaidi Ya Kuogopwa    

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لَا يَحْقِرَنَّ أَحَدُكُمْ نَفْسَهُ إِذَا رَأَى أَمْرًا لِلَّهِ فِيهِ مَقَالٌ أَنْ يَقُولَ فِيهِ، فَيُقَالُ لَهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ:  مَا مَنَعَكَ أَنْ تَقُولَ فِيهِ؟ فَيَقُولُ رَبِّ! خَشِيتُ النَّاسَ، قَالَ: فَأَنَا أَحَقُّ أَنْ تَخْشَى)) مسند أحمد

Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Asijifanye duni mmoja wenu atakapoona jambo la Allaah ambalo angeliweza kusema kitu juu yake lakini asiseme (aogope), kwa hivyo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Humwambia siku ya Qiyaamah: Kipi kilichokuzuia usiseme kitu kuhusu jambo kadhaa wa kadhaa? Husema: Nikiogopa watu. Kisha Mola Atasema: Ni mimi Ndiye ninayepaswa kuogopwa.” [Musnad Ahmad]

 

Share