Skip navigation.
Home kabah

Hadiyth Ya 33 - Mja Mwenye Kusubiri Anapoondokewa Na kipenzi Chake Hulipwa Pepo

 

 

Hadiyth Ya 33

 

Mja Mwenye Kusubiri Anapoondokewa Na kipenzi Chake Hulipwa Pepo

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَقُولُ اللَّهُ تَعَالَى مَا لِعَبْدِي الْمُؤْمِنِ عِنْدِي جَزَاءٌ إِذَا قَبَضْتُ صَفِيَّهُ مِنْ أَهْلِ الدُّنْيَا ثُمَّ احْتَسَبَهُ إِلَّا الْجَنَّةُ)) البخاري

 

Kutoka kwa Abu Hurayrahرضي الله عنه  ambaye amesema: kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Allaah Aliyetukuka Anasema: Haitokuwa jazaa ya mja wangu Muumini Ninapomchukulia kipenzi chake bora katika wakazi wa duniani kisha akastahamili kwa ajili Yangu, haitakua ila ni Pepo)) [Al-Bukhaariy]