Usufi
Imefasiriwa na ‘Abdun-Naaswir Hikmany
Neno Sufi inawezekana limetoholewa kutoka neno la Kiarabu “suuf”, lenye maana ya manyoya (sufi). Hii ni kwasababu ya tabia za Masufi kuvaa makoti ya sufi, mtindo ambao wameuanzisha na kupelekea amri ya Kisufi. Imani za awali za Masufi ziliaminika kwamba uvaaji wa makoti ni kujifananisha na Iysah bin Maryam (Yesu). Akijibu hili, Ibn Taymiyyah amesema:
“Kuna watu ambao wamechagua na kupendelea kuvaa nguo za manyoya, wakidai kwamba wanataka kufanana na al-Masiyh bin Maryam. Lakini mtindo wa Mtume unapendelewa zaidi kwetu sisi, na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akivaa pamba na aina nyenginezo za nguo.”[1]
Usufi unajulikana
Masufi walisifika katika kipindi cha awali cha ukuaji wa Usufi kwa kujinasibisha kwao mahsusi na dhikr (kumkumbuka Allaah) na kujiweka faragha, na pia (huo ulikuwa ni) mwanzo wa matendo ya uzushi ili ‘kutia uzito matendo ya kidini’. Hata pia mwanzoni wa ukuaji wa Usufi, (na) kabla ya kujihusisha na silka za uzushi na amri za kutengeneza, wanazuoni walikanya mkusanyiko wa matendo ya Kisufi wenye msimamo mkali.
Imaam ash-Shaafi’iy alikuwa na maoni kwamba:
“Kama mtu anafuata Usufi (Tasawwafa) mwanzo wa siku, hafikii adhuhuri ila ni mpumbavu.”
Imaam Maalik na Ahmad bin Hanbal pia walikuwa na mawazo yaliyofanana na hayo katika mwendo huu mpya uliochimbuka kutoka Basrah, Iraq. Ingawa ilianzia
Bakuli Lililochanganywa
Kutokana na kufariki Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘Anhum) na warithi wao, hapo mlango ukawa wazi kwa kuziharibu Kanuni za Kiislamu. Maadui wa Uislamu walikuwa tayari wamekwishapenya sana ndani ya vyeo vya Waislamu na kusababisha mara moja fitnah kupitia kwao kueneza Hadiyth za uongo na hapo hapo kuanzisha madhehebu mepya kama vile Khawaarij na Mu’tazilah.
Ni kipindi hichi ambapo Usufi ulipata msingi wa malezi yake, ulipata usaidizi kutoka kwa Watawala wenye nasaba ya Kifalme, ambao walikwenda kinyume na Uislamu hadi kufikia kwamba uchawi ulikuwa ukitumika kama ni starehe ndani ya mahkama zao, ingawa uchawi unatambulika
Mnamo karne ya tatu ya Kiislamu, Masufi walifasiri kazi za Kigiriki kwenda Kiarabu, tafsiri ambazo zilipelekea kuacha alama isiyofutika katika nyanja nyingi za Kisufi, zilizosababishia kuamini kwenye imani za Kigiriki kwamba ulimwengu wote ni Mungu au kwamba kuna miungu mingi iliyopelekea kukamilisha sehemu ya dhana yake ya Kisufi. Matendo ya Kipagani kama vile kuabudia watu Watakatifu, matumizi ya uchawi na kushikilia kisasi dhidi ya Mashaykh wao viliwatoa kwenye imani barabara ya vitendo vya Kiislamu na vilikuwa na mfanano mdogo kwa Uislamu uliochwa na Mtume wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa kuchunguza dhana za kuzua za Ukristo, Uhindu, Utaustu[6] na dini nyengine, inakuja wazi namna ambavyo Usufi ulivyo karibu na dini hizi kuliko Uislamu.
Ukweli ni kwamba, Usufi hauna sifa chini ya “Uislamu” kwa aina yoyote itakayopangiwa, isipokuwa chini ya “Uzushi usioelezeka”.
Sharda anabainisha mifanano hii isiohitajika kwa kueleza kwamba: “Baada ya kuanguka kwa nguvu ya Waislamu wenye imani barabara katikati ya India kwa kipindi cha karne, kutokana na uvamizi wa Taimuur, Masufi walikuja kuwa huru na kutotawaliwa (tena) na Waislamu wenye imani barabara. Hali hii, iliwapelekea kuwafanya watakatifu wa Kihindi kuwa wenzao ambao waliwaathiri kwa namna iliyo ya ajabu. Masufi walitumia Umoja (Monism)[7] na uzushi wa uke kutoka mafundisho ya matendo ya Vaishnava Vedantiki na Bakti na Yojiki. Kwa wakati huo, umaarufu wa imani za Kivedantiki kwamba ulimwengu wote ni Mungu au kwamba kuna miungu mingi ulistawi vyema ndani ya Masufi.[8]
Tofauti zifuatazo zinafafanua mifanano isiyo linganifu ambayo Usufi unafuata pamoja na dini nyengine:
Fikra Ya Usahihi Wa Dini Zote
Dhana ya Usufi ya kukubalika kwa dini zote mbele ya Allaah inatokana na imani za kuzua za dini nyengine, na sio Uislamu, kwani Allaah Anasema:
{{Bila shaka Dini (ya haki) mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.}} [3:19]
Chukulia kwa mfano Mabudha: “Hakuna Budha anayeelewa (haswa) mafundisho ya Budha mwenye fikra kwamba dini nyengine ni za makosa…. Dini zote zinatambuwa kwamba hali ya kuwepo mwanaadamu hakuridhishi. Zote zinafundisha maadili ya upendo, huruma, subira, ukarimu na uwajibikaji kwa jamii na zote zinakubali kuwepo kwa namna fulani ya Mkamilifu.”
Masufi pia wanaamini hivyo hivyo: “Allaah Hatofautishi baina ya asiyeamini na faasiq (mtendaji maovu) au baina ya anayeamini na Muislamu. Ukweli (hao) wote Kwake wapo sawa… Allaah Hatofautishi baina ya kaafir na mnafiki au baina ya mtakatifu na Mtume.”[9]
Ndani ya al-Fusuus, Ibnu ‘Arabiy hakuacha shaka kwa mnasaba wa kujitia hatiani kwenye umoja wa dini zote: “Jihadhari na kujiwekea mipaka katika dini maalum na kutoamini vitu vyengine vyote, kwani mambo mazuri yaliyo makubwa yatakosekana na wewe, hakika utakosa kufikia kwa elimu ya mambo kwa mfumo unaofuata. Isipokuwa kuwa tayari kukubali mifumo yote ya imani. Hii ni kwa sababu Allaah ni Aliye Juu na Mkubwa kuliko uwezo wa mtu kuweza kuamini kufikia kuacha dini nyengine. Isipokuwa zote ni sahihi, na kila mtu ambaye yupo (njia) sahihi anapata malipo, na kila mtu anayelipwa ameneemeka, na kila anayeneemeka ni mtu ambaye Yeye Amemridhia.” [10]
Ushirika Pamoja Na Muumba
Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ni tofauti kabisa na viumbe Vyake. Hafanani na viumbe Vyake wala Haingiliani nayo (dhana hiyo). Hata hivyo, Masufi pamoja na dhana
Hivi ndivyo Masufi walivyoenda mbali katika kufru kwasababu ya kushabihiana kwao na filosofia za Ugiriki na Mashariki, badala ya Qur-aan na Sunnah. Kwao wao Mungu sio Allaah Pekee, Ambaye hakuna chengine chochote kinachoshiriki Utawala Wake, isipokuwa kwamba kila tunachokiona kutuzunguka sisi, na hadi kufikia sisi wenyewe (basi hivyo vyote vinafaa kushirikishwa na Mungu)! Utukufu ni wa Allaah, Aliyeeleza:
{{Hakuna chochote mfano Wake; Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.}} [Ash-Shuura: 11]
Tukiangalia wapi Masufi walipopata mafundisho yao, tunaona kwamba imani hizo hizo zilizojazana: “Unapoishi kwenye nyumba ya hekima, hutoona tena kizuizi baina ya “mimi” na “wewe”, “hichi” na “kile”, “ndani” na “nje”; utakuja mwishowe, katika nyumba yako ya kweli, hali ya sivo kuwa viwili non-duality.”[12] “Mwisho, utambuzi wa kuhakikisha kwamba imani imekomaa barabara inawezekana kwa usahihi kutamkwa kwa dai la ajabu, ‘Mimi ni Shiva’ (Mungu wa Kihindu)”.[13] “Pale ninapokuwa ndani ya
Kuiharibu Tawhiyd Katika Sifa Za Allaah
Masufi wanakataa moja kwa moja Sifa zote za Allaah, kama vile Uso Wake, Mikono Yake, Istawaa n.k, wakitumia maana za kimafumbo kuelezea Sifa Zake. Ingawa Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘Anhum) na Taabi’iyn (Rahimahum Allaahu) waliziamini bila ya kuzifananisha na uumbaji Wake, Masufi wanasadiki Sifa Zake kuwa ni sehemu ya uumbaji Wake.
Ibnu ‘Arabiy ameenda mbali zaidi hadi kusema kwamba amemuona Allaah wakati mmoja aliporukwa na akili na akiwa na hali
Uingizwaji wa muziki ndani ya ibada za aina yoyote, hauna ruhusa kwa wanazuoni wengi, na inabaki kuambatanishwa nayo kwa vitendo vyengine
Muziki ulitanda katika mizani iliyo kuu katika mahkama za Mughal, wafalme Akbari, Jahangiri na Shah Jahani, na Maderweshi Wakisufi walitumia muziki
“…watakapojitokeza waimbaji wanawake wakiwa na ala zenye nyuzi, ulevi kunywiwa, na wafuasi wa mwisho wa watu hawa wanawalaani wa mwanzo, angalia wakati huo kwa kutokea upepo mkali, mtetemeko wa ardhi, kumezwa na ardhi, badiliko la umbo, mvua kubwa mno, na alama zinazofuata moja baada ya nyengine kama vipande vya mkufu vinavyoanguka kimoja baada ya chengine pindi nyuzi zake zinapokatwa.” [At-Tirmidhiy]
Ulaghai wa Kisufi unawekwa wazi kwa kuangalia maisha ya viongozi wao wanaoheshimika, Mashaykh ambao wamewekewa imani kamili ndani ya elimu iliyorithiwa na kutii kila amri
Mashekhe Wa Kisufi: Ni Mfano Wa Kuigwa Au Wapotofu?
Bayazid Tayfur al-Bistami
Bayazid anatambulika kuwa ni “miongoni mwa nyota sita zinazongaa kwenye anga za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)”, na kiunganishi ndani ya Mfuatano wa Dhahabu wa Naqshabandi Tariqah. [17]
Lakini bado maisha yake yalivunda kwa Shirin za aina zote. Bayazid al-Bistami alikuwa ni wa mwanzo kueneza uhalisi wa Uharibifu (fana’), ambapo Uzushi unammeza hadi kufikia kutojielewa yeye mwenyewe au vitu vinavyomzunguka. Kila kinachokuwepo kinaonekana kuyeyuka, na anahisi kuwa huru kwa kila kizuizi ambacho kitasimama katika njia yake ya kumuangalia Yule Mwenye Kukumbuka Pekee.
Miongoni mwa hali zake
Alisifia kwamba wenye kuamini ni sawa na wasio amini, ambao Allaah Amewaeleza kuwa ni (waovu) kuliko ngombe (Surah ya 7, aya ya 179) na mbwa[18]; ni wasio amini hao hao ambao Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitamka kwamba ameamrishwa kupigana vita hadi wale kiapo kwamba hakuna kufanya Uungu isipokuwa Allaah.
Maisha yote ya Bayazid yalienea kwenye migongano ya Iymaan. Katika umri wa ujana, alimuacha mama yake akimtamkia kwamba hawezi kumtumikia Allaah na mama yake kwa wakati mmoja.[19] Alipokuwa akitembea mitaani, mara moja alipiga kelele: “Mimi ni Mungu; kwanini hamuniabudii mimi?” Alitumia muda wake akiwa amekaa huku kichwa chake kikiwa baina ya magoti, akielezea mmoja wa wafuasi wake; kwamba alifanya hivyo kwa miaka thelathini.
Cha ajabu kuliko yote ulikuwa ni utiifu wake kwa mbwa ambaye alikutana naye mara moja. Mbwa huyo kwa uwazi alikuja kukasirika kwa tabia ya Bayazid kujaribu kumuepuka, kwa
Ibnu ‘Arabiy
Wakati wa kipindi cha mwisho mwa karne ya 12 na mwanzo wa karne ya 13, chini ya ushawishi wa uzushi ulio mbaya, Ibnu ‘Arabiy alitoa mfumo ambao ulizalisha ufa mkubwa baina ya sheria na Usufi, ndani ya jamii nyingi, kama vile Uislamu wa India, ambao ulikuwa na nguvu kabla ya kurithi mambo ya uzushi ndani ya Uislamu, ufa huu ulikuja kuwa mkubwa zaidi. [21]
Muhyiddin bin ‘Arabiy huwenda akawa anashikilia nafasi ya juu miongoni mwa Madhehebu ya Kisufi, na alikuwa kinara ndani ya mgawiko wa milele baina ya Uislamu na Usufi. Alidai kupokea amri za moja kwa moja kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) mwenyewe, ikiwemo kitabu kilicho na Hadiyth mpya kabisa ambacho hakijapatapo kuonekana wala kusikika hapo kabla. Pindi alipopokea ‘wahyi’ huu, Ibnu ‘Arabiy alikuwa anatambulika kuhudhuria mikusanyiko ya usiku night parties ndani ya Seville (Hispania). Wakati mmoja katika mikusanyiko hii, alisikia sauti (ya ulevi wake kutoka ndani?) ikimwita: “Ewe Muhammad, sio kwa sababu hii wewe umeumbwa.”
Alikimbia akikhofia ziara (yake aliyoifanya) makaburini, ambapo alidai kukutana, na kupokea muongozo kutoka kwa ‘Iysah, Muusa na Muhammad (‘Alayhi swalaatu was-salaam ajma’iyn). Kutoka kwenye vitabu vyake, misemo isiyohesabika yenye mnasaba na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) imetumika, hadi kufikia kwamba Waislamu wasio na idadi wanaiamini kuwa ni kweli. Ifuatayo ni nukuu kutoka kwa Ibnu ‘Arabiy:
“Mtu mwenye hekima daima hatojisalimisha kwa mfumo wowote au imani yoyote, kwasababu yeye ni mwenye hekima ndani yake mwenyewe.”[22]
“Vyote vilivyobaki kwetu sisi kwa mwenendo (Hadiyth) ni maneno matupu. Ni juu yetu kutafuta yana maana gani”.[23] (Hii inamaanisha mshikamano wake kwenye maana na tafsiri za Baatini (undani)
“Yeye (Ibnu Rushd) alimsifu Mungu kwamba kwenye muda wake amemuona mtu mmoja (Ibnu ‘Arabiy) ambaye ameingia katika kimbilio la ujinga na (sasa) ametoka nje mfano wa hivi (elimu ya tafsiri za Baatini) – bila ya mafunzo, majadiliano, uchunguzi au kusoma”.[24]
Junayd
Junaid alikuwa ni kiongozi wanne katika mtiririko wa Safayid ambaye alijaribu kubadili mtiririko wa nguvu za kinafsi kwenda kwenye nguvu za kisiasa. Hata hivyo, kitu ambacho kinawezekana kuwa kilikuwa hakieleweki miongoni mwa wafuasi wake ni sera zake za kijeshi zilizo hatari, zikikusanywa pamoja na wacha Mungu wa Kishia na Kisufi.[25]
Mwanawe wa kiume, Haydar, mwenyewe alijianzishia utawala wa Safayid na Shia Wakiislamu Wakumi na mbili ikawa chini ya mjukuu wake, Isma’il. Inasemekana alimpiga hadi kufa mtumishi wake wa kike, ambacho alidai kwamba alikuwa akiitawala miaka yake arobaini ya matendo yake ya kinafsi.[26] Huyu aitwaye ‘Mtakatifu’, anayetegemewa kuwa ni rafiki wa Allaah, alitoa matamshi yafuatayo: “Nimemuona mwizi ambaye amenyongwa katika mti wa kuhukumiwa kifo kwa sheria. Nilimuinamia… kwa kuwa alikuwa ni mkweli katika nyanja aliyokuwa akiifuata.” “Yeyote anayemukhofu Allaah daima hatabasamu.” “Usahaulifu mmoja wa Muumba unaharibu ibada ya miaka alfu”.
Mansuur al-Hallaaj
Mansuur ni maarufu kwa madai yake “Ana-l-Haq” (Mimi Ndie Mkweli), kutokana nayo (kauli hiyo) aliuawa kwa sababu ya kurtadi. Lakini bado anaheshimika na Masufi ingawa aliacha sheria zote zinazohusu Tawhiyd.
Inasemekana ya kwamba aliishi na vazi
Abuu Yaziyd
Mara moja Abuu Yaziyd aliswali Swalah ya Ijumaa sehemu 24,000 tofauti. Aliwaeleza wakuu wa dini sehemu moja: “Nilikuwa ninaswali ndani ya nyumba tofauti 12,000 za kuabudia hii leo.” Walimuuliza: “Namna gani?” Alijibu: “Kwa nguvu ya Mola Mtukufu.
Jee hawa ndio wakweli ambao tunaambiwa walipokea elimu ya dini yetu? Jee hawa watu wanashabihiana na mafundisho ya Uislamu? Mtu ambaye ameacha utiifu kwa mama yake, kwa ajili ya kumtii mbwa? Jee tunahitajika kufuata watu ambao wamepokea wahyi katika ziara za makubiri baada ya kutumia muda wao kumbi za usiku za starehe? Au mtu anayemuua mtumwa wake kwa ‘kuharibu’ ibada zake? Kwetu sisi, Uislamu unaita kutabasamu ni sadaka, sio kukufuru kutokana na Mapenzi ya Allaah. Uislamu unazuia unyongovu kwa mtu yeyote isipokuwa Allaah. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba du’a akitafuta muongozo wa Allaah, sio kuomba mafundisho yanayokwenda kinyume na dini. Na Uislamu unatufundisha ukweli, sio uongo.
Ushahidi Dhidi Ya Mafundisho Yao: Imani Na Matendo Yao
Hadhi Ya Shaykh Na Walii
Shaykh au Walii anapewa heshima sawa
Juu ya hivyo, Waislamu wanaamini kwamba kitendo chochote cha ibada ni lazima kithibitishwe kwa Qur-aan na Sunnah tu. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema:
{{Sema: “Leteni dalili zenu,
Na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “muumbwa asitiiwe juu ya Muumbaji.” Shaykh huyo anapewa hadhi ya Uungu ndani ya Usufi. Sifa ambazo ni za Allaah, halikadhalika zinanasibishwa kwa Mashaykh wao. Wanaomba msaada kutoka kwao, ikiwa wamekwisha fariki au wapo umbali wa kilomita alfu kumi. Wanaamini kwamba Mashaykh wao wanaelewa kila kitu ambacho wanafunzi wao wanafikiri, na kwamba wanazungumza na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kila kipindi maalum (kiuhalisi).
Uharibifu Wa Dhana Za Dhikri, Hadiyth Na Qur-aan
Kwa vile Qur-aan na Hadiyth Sahiyh haiwezekani kubadilishwa, Masufi wakageukia kwenye ta’wiil, mfumo wa kubadili maana iliyo wazi ya aya au Hadiyth na kupata (maana) iliyofichika. Mfumo huu uliwapatia mwendo wa kutosha ulio mwepesi kwenye kuthibitisha dhana yoyote wanayohitaji, kazi rahisi ni kueleza kwamba aya au Hadiyth ilikuwa na maana ya ndani ambayo Shaykh mwenyewe anaweza kuitambuwa. Ndani ya kitabu chake Ibnu ‘Arabiy, cha ‘Bezels of Wisdom’, Ibnu ‘Arabiy anawasilisha nyanja fulani kwa namna anavyotafsiri aya zenye mnasaba wa Suurat Nuuh kwa mtindo ulio mbaya kabisa, kwa vile anashauri maana zilizo halisi sawasawa zikipingana na zile zinazokubaliwa na Wanazuoni Waislamu.
Anawatafsiri “wakosaji,” “makafiri,” na “watenda dhambi” ndani ya Suurat Nuuh kama ni ‘watakatifu na Wenye elimu ya kinafsi’ kuzama na kuungua moto sio kwa adhabu ya Moto, bali kwa mwako wa moto na maji ya elimu ya Mungu. Ibnu ‘Arabiy ametambua kuabudia masanamu kwa watu wa Nuuh kama ni uungu takatifu. Allaah Amekataza matendo
{{Na waliwaambia (wafuasi wao): “Msiache miungu yenu, wala msiwaache Waddi wala Suwa’a wala Yaghutha wala Ya’uqa wala Nasra.” (Majina ya waungu wao wa kisanamu.}} [71:23]
Ambapo Ibnu ‘Arabiy aliitolea maoni: “
Kitendo cha kufanya Dhikr ndani ya maduara na kuruka au kutikisika
Lakini tendo la kukaa ndani ya maduara na kwa sauti ya juu au ya chini kupiga kelele “Allaah, Allaah” haukupata kufanyiwa kazi na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wala Salaf, na Hadiyth zote zinazoeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifanya hivo (kama mfano alipodhaniwa kwenda kwenye chumba, akawaambia Maswahaba kunyanyua mikono
Pia ameeleza kwamba kuitamka kwa “Allaah, Allaah” imezuiwa, kwani haijapatapo kutangazwa kuwa ni mfumo wa Dhikri, na haiambatani na neno lenye kuikamilisha (
Uzushi
Imaam Maalik ametanabahisha: “Kile ambacho hakikuwa dini wakati wa Mjumbe na Maswahaba zake, Allaah Awe Radhi nao wote, hakihitajiki kuwa ni dini leo. Yule anayeanzisha uzushi (bid’ah) ndani ya dini ya Kiislamu na kuamini kuwa ni kitu kizuri, kwa kufanya hivyo, anadai kwamba Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameusaliti Ujumbe.” Masufi wanaonekana kupendelea kwenye kutumia kiwango kikubwa mno cha mali kutetea vitendo vya uzushi, wakidai kuwa hivyo ni “uzushi ulio mzuri.”
Hizi zinahusisha kusherehekea kifo cha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) (kitendo kilichotokana na utawala wa Fatamidi, ambao walianzisha uzushi huu ili kupata ridhaa ya watu wengi), kusoma Qur-aan juu ya maiti na kutafuta rehma kutokana nao, na ujenzi wa misikiti yenye gharama za kupita kiasi (ingawa Mtume wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)) amekataza hili. Anas anasimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Saa haitokuja kupita hadi watu washindane na kila mmoja kwenye (kujenga) misikiti.” [Ahmad, Abuu Daawud, an-Nasai’i, Ibni Maajah].
Sababu Zinazowafanya Hadi Leo Kuwepo Wakiambatana Na Kusukumwa Kiurahisi Kwenye Mambo Ya Furaha Au Huzuni.
Masufi wamefikia hadi ya kuwa ni sehemu ya maisha kwa Waislamu walio wengi mpaka Waislamu wanaona taabu kukubali kwamba njia ya Kisufi ni ya makosa, na kumtuhumu yeyote anayebainisha makosa ya Kisufi kama ni mwenye itikadi kali au mfuasi wa dhehebu ‘lililopotoka’. Usufi unawaita watu kwenye hisia kuliko akili na ushahidi wa Kiislamu. Kwa mfano, ushairi na muziki ilikuwa ni mifumo maarufu zaidi kipindi cha miaka mia moja iliyopita, ambapo “mawazo ya Kisufi yalilowesha mioyo ya watu wote walioelekea kwenye ushairi.”[30]
Leo, Usufi unafuatwa na makundi ya watu ambao wapo tayari kuacha nyuma matatizo ya dunia hii, (na) badala ya kujenga uwezo wa kuyabadilisha. Usufi unatoa mwanya mzuri wa kukimbia, wafuasi wake wanaweza kutafakari badala ya kuwafikiria Waislamu wengine wanaopata taabu, achilia mbali kuwasaidia.
Halikadhalika, kutokana na imani za Kipagani, Usufi unafanana mno na dini nyengine, na
Usufi unawapatia wafuasi wake maisha ambayo hayajali kabisa kupigana (jihaad), siasa, hamasa ya kutafuta elimu na kuisomesha, kazi ya da’wah, na inaruhusu mtu kujipenyeza kwenye mambo ya dunia
Kiongozi wa Naqshabandi Tariqa ndani ya Marekani, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema yafuatayo: “Unahitajika kuwa sehemu zote, kinafsi na kiroho. Masufi wanaweza kuwapatia watu furaha kwenye maisha
Inatoa nguvu kwa serikali, kwa kundi lolote (jengine) kulifanya kuwa ni lazima lionekane lina utata na ambalo linalofikia kupata nguvu iliyo kinyume na Serikali ya Kiislamu. Wakati wa utawala wa dikteta Mustafa Kemal, ambapo chini ya utawala wake maelfu ya wanazuoni waliuawa na vitendo vya Kiislamu kupigwa marufuku. Idhini maalum ilipatiwa kwa serikali ya Kituruki mwaka 1954, ikitowa ruhusa kwa maderweshi wa Mawlawi kutoka
Ukweli ni kwamba, siku hizi wametokea kuwa na mvuto wa kawaida, wakitumbuiza duniani kote pamoja na kundi lao la Mambo Yanavyoonekana ya Muziki wa Kuzua wa Taifa la Uturuki (Turkish Mystical Music State Ensemble).[32] Shaykh wa Naqshandandi wa Marekani amemsalimia na kupokea sifa kutoka kwa Raisi wa Marekani Bill Clinton mwenyewe. Na kwanini asipate? Kwani ‘Uislamu’ anaouchora ni wa upole na mshikamano pamoja na Makafiri.
Kugeuzwa Kwa Ushahidi
Kwa vile Qur-aan na Hadiyth tayari zinapatikana, na haziwezi kubadilishwa, Masufi wamekimbilia kwenye ujanja mwengine unaotumiwa na Wazushi wengine:
Ta’wiil, au kubadili maana iliyo wazi ya aya au Hadiyth kuifanya kuwa ni yenye siri ya ndani ambayo ni Shaykh tu anayekubalika ndie anaweza kuielezea! Pia wanaegemea kuipatia hadhira Hadiyth za uongo, kama ile inayosema kwamba Nabii Adam (‘Alayhi swalaatu was-salaam) aling’ang’ania kwa sana kuomba (msamaha) kwa jina la Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) pale alipofanya dhambi; riwaya za Khidhri; kuibuka kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka kwenye kaburi lake ili mtu apate kuubusu mkono wake na mengineyo. Kwasababu ya kukosa elimu, makundi ya watu yaliyo mengi yamekamatana na elimu ya Hadiyth na Aqiiqah, wanaamini yale wanayoelezwa, na kuzielezea riwaya hizo kwa vizazi vyengine, zikiharibiwa zaidi njiani humo.
Njia nyengine iliyo bunifu ni kwa kusifu misemo iliyoharibiwa ikikubaliwa na Masufi kutokana na wanazuoni waadilifu. Kwa mfano, Ibni Taymiyyah amesifiwa kwamba aliwahi kuwa ni mjumbe wa mfuatano wa Qadiri na alimilikiwa, na kuzungumza maneno makubwa kuhusu Bistami na sifa zake. Lakini bado Ibni Taymiyyah ametumia muda mkubwa wa maisha yake kupigana dhidi ya mafundisho ya Kisufi, amefungwa kwasababu
Maafa Kwa Ummah
Masufi wamewaharibu Waislamu kwenye mafundisho ya Qur-aan na Sunnah na kuwapeleka katika utumwa wa Shaykh. Hivyo, Waislamu wametengwa kutokana na mafundisho ya Uislamu, na wala hawahodhi kinga kutokana na uzushi na mitego ya madhehebu ya kikafiri. Mafundisho kama: “Yeye (mfuataji) asiangalie mwengine isipokuwa Shaykh wake” hayakufanya chochote kuiziba jamii. Isipokuwa, imefanya mpira kufingirika kwa vita baina ya Madh-hab tofauti, ambayo madhehebu hayo yamepelekea kupigana, kuachana kwa kila imani tofauti, na kuswali vituo tofauti ndani ya Makkah wenyewe.
Masufi wameacha chapa iliyo mbaya katika uono wa Uislamu, wakiuchora kama ni ya amani na siasa safi[33], na mtu yeyote anayekwenda kinyume ni laghai na anatambulika kuwa ni mwenye imani kali. Kwa kuegemea kwenye Hadiyth za uongo
Bila ya shaka, Masufi wamehamasisha kuchangia
Wakati ambapo makundi ya watu yalishughulika kwenye ujenzi wa misikiti ya gharama iliyochupa mipaka na kuzunguka katika maduara (wakifanya dhikr), Utawala wa ‘Uthmaan uliangushwa na Masonsi na matokeo yake kuchanwa chanwa. Hatima ya Kisufi tokea ilipoibuka awali, ilikuwa ni kuangamiza na kuharibu, kwasababu ya kufru zake kinyume na mafundisho ya Qur-aan na Sunnah. Kuzidisha kulikokuwa kudogo, uzushi ulio mdogo, ulipelekea kuwa na athari kubwa mno,
Kwa ukweli, Uislamu unatutosha, na ni Shaytwaani peke yake anayependelea kutugeuza mbali na dini yetu, kutufanya kuchupa mipaka, na kuanguka kwenye mtego wake. Njia pekee iliyo muafaka kuepuka ni kukamatana kwa nguvu zote kwa kile kilichowachwa nyuma yetu na Mtume wetu mpenzi (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Qur-aan na Sunnah, kama inavyoeleweka na kuaminika na kufanyiwa wazi na watu bora waliopata kuishi: Salaf-us-Swaalih (Rahimahum Allaahu), Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘Anhum) na wale waliofuata nyendo zao.
[1] Al-Fataawa 11/7
[2] Encyclopaedia Britannica
[3] Kamusi ya Merriam-Webster’s Collegiate
[4] Encyclopaedia Britannica
[5] Misingi ya Tawhiyd The Fundamentals of Tawhiyd, Abuu Amiynah Bilaal Philips
[6] Taoisti (au Daoisti) unahusiana na aina tofauti za filosofia za Kichina na dini za kimila na dhana. Mila hizi zimeiathiri
[7] Kwa mujibu wa dhana ya Usufi ni kwamba; hakuna tofauti baina ya Allaah na uumbaji Wake. Vyote hivyo ni vitu vimoja, na ndipo inapopatikana hiyo kanuni ya Umoja, kuviabudia vyote hivyo ni sawa tu kwao. Kuielewa dhana ya Umoja; tofautisha na Uwili kwa kuwepo Allaah upande mmoja Peke Yake na uumbaji wake kwa upande wa pili. [Mfasiri]
[8] S. R. Sharda, Fikra za Kisufi Sufi Thought
[9] Njia ya Naqshbandi The Naqshbandi Way,
[10] Ibnu ‘Arabiy, al-Fusuus,
[11]
[12] Kitabu cha Tibetani cha Kuishi na Kufa The Tibetan Book of Living and Dying,
[13] Moyo Ulio Na
[14] Angela wa Foligno: Kazi Zilizokamilika, Angela of Foligno: Complete Works,
[15] Encyclopaedia Britannica
[16] ibid
[17] Njia ya Naqshabandi
[18] Aya hii imemfananisha na mnyama wala sio ngombe
[19] Kumbukumbu za Watakatifu, imetafsiriwa
[20] ibid
[21] Encyclopaedia Britannica
[22] Shairi lisilochapishwa kutoka kwa Ibnu ‘Arabiy ‘Diwan’, imetafsiriwa na Dr.
[23] Makala ya Stephen Hirtenstein kuhusu Muhyiddin Ibnu ‘Arabiy: Hazina ya Huruma
[24] Wasufi wa Andalusia, imetafsiriwa na R. W. J. Austin,
[25] Encyclopaedia Britannica
[26] Kumbukumbu za Watakatifu,
[27] ibid
[28] Njia ya Naqshabandi
[29] Shaykhul Islaam Ibn Taymiyyah, Majmuu’ al-Fatawaah
[30] Encyclopaedia Britannica
[31] Taoisti (au Daoisti) unahusiana na aina tofauti za filosofia za Kichina na dini za kimila na dhana. Mila hizi zimeiathiri
[32] Hivi karibuni walikuja kutumbuiza nchini
[33] Kwa ufafanuzi zaidi, soma makala ambayo inapatikana ndani ya alhidaaya; Masuala Kumi Yanayoeleweka Vibaya Kuhusu Uislamu. [Mfasiri]
[34] Ulimwengu wa
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
