Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Vipimo
Nyama Ya Mbuzi 1 Kilo
Mchele 4 Magi
Vitunguu 3
Nyanya 2
Nyanya kopo 3 vijiko vya chai
Pilipili mbichi iliyosagwa 1 kijiko cha supu
Garam Masala (mchanganyiko wa bizari) 2 vijiko vya supu
Hiliki 1 kijiko cha chai
Chumvi kiasi
Mafuta ½ kikombe
Zaafarani au rangi za biriani za kijani na manjano/orenji
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Sosi Ya Nyama
- Changanya nyama na thomu, pilipili, chumvi na nusu ya garam masala. Tia katika treya ya oveni uipike nyama (Bake) hadi iwive. Au iwivishe kwa kuichemsha.
- Katika kisufuria kingine, tia mafuta (bakisha kidogo ya wali) kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi, kisha tia nyanya, nyanya kopo, bizari zote nyingine zilizobakia.
Namna Ya Kupika Wali
Mchele 4 magi
Mdalasini 1 kijiti
Hiliki 3 chembe
Kidonge cha supu 1
Chumvi
- Osha na roweka mchele wa basmati.
- Tia maji katika sufuria uweke jikoni. Tia kidonge cha supu, mdalasini, hiliki na chumvi .
- Yakichemka maji tia mchele, funika upike hadi nusu kiini kisha uchuje kwa kumwaga maji.
- Tia mafuta kidogo katika mchele na zaafarani iliyorowekwa au rangi za biriani kisha rudisha mchele katika sufuria ufunike na upike hadi uwive.
- Pakua wali katika sahani kisha mwagia sosi ya nyama juu yake, pambia kwa kukatika nyanya, pilipili mboga na figili mwitu (Celery) au mboga yoyote upendayo.
- Login or register to post comments
- Chapisha
- Kutuma Kwa Email
