031-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kumsahihisha Imaam Na Kujikinga Na Shaytwaan

 

 

KUMSAHIHISHA IMAAM

 

Ametoa  (صلى الله عليه وآله وسلم)mfano katika kumsahihisha Imaam anapobabaika au anapochanganyikiwa na kisomo chake. Mara moja aliswali, akasoma ndani yake kisomo, akasahau. Alipomaliza alimwambia Ubayy: ((Uliswali na sisi?)). Alijibu: "Ndio". Akasema: ((Hivyo nini kilichokuzuia [kunisahihisha]?))([1]).

 

 

 

KUJIKINGA NA SHAYTWAAN NA KUTEMA MATE KIDOGO WAKATI WA SWALAH ILI KUONDOSHA WASIWASI

 

'Uthmaan bin Abil-Aasw (رضي الله عنه) alimwambia: "Ewe Mjumbe wa Allaah! Shaytwaan ameingia baina yangu na baina ya Swalah yangu na kisomo changu, ananibabaisha katika kisomo changu!" Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Huyo ni Shaytwaan anayeitwa Khinzab, hivyo utakapomuhisi jikinge kwa Allaah naye, na tema mate kidogo([2]) upande wa kushoto kwako mara tatu)). Akasema: "Nikafanya hivyo, na Allaah Akamuondoshelea mbali nami".([3]).

 

 





[1] Abu Daawuud, Ibn Hibbaan, Atw-Twabaraaniy, Ibn 'Asaakir (2/296/2) na Adhw-Dhwiyaa katika Al-Mukhtaarah kwa isnaad Swahiyh.

[2] "At-Tafl" ni mpulizo ikiwa na mate kidogo, hivyo ni zaidi ya kupuliza.  (An-Nihaayah).

[3] Muslim na Ahmad. An-Nawawiy (رحمه الله) amesema: "Hadiyth hii ina mapendekezo ya kujikinga na Shaytwaan anaposhawishi, pamoja na kutema mate upande wa kushoto mara tatu".

 

Share