Mama Yake Muislamu, Baba Mkristo, Je Anaweza Kuoa Mwanamke Wa Kiislamu?

SWALI

 

 


Baada ya salamu. .naomba jibu tafadhali,nina rafiki yangu amekuja kupwoswa,lakini kijana aliyemposa mamake ni muislama na babake ni mkristo  .lakini yeye kijana ni muislama sasa inamruhusu sheriya huyu msichana kuolewa na huyu kijana. .tunaongoja majibu
 
Wasalamu alaikum warahmatullahi wabarakatu
 
ndugu yenu mwislamu

 


 

 

JIBU:

 

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Jibu ni kwamba inafaa kijana huyo kumuoa mwanamke wa Kiislamu, na hata ingelikuwa wazazi wake wote wawili sio Waislamu anaweza kuoa kwani inatosha yeye pekee kuwa Muislamu kuruhusiwa kuoa mwanamke wa Kiislamu. Isiyopasa ni mwanamke wa Kiislamu kuolewa na mwanamume asiyekuwa Muislamu.

 

 

Ni neema kwake huyo kijana kuwa yeye amefuata dini ya haki, hivyo inampasa amshukuru Mola wake kwa kumhidi katika haki. Mahusiano ya wazazi, ndugu, jamaa, hayamfai mtu siku ya Qiyaamah, kila mtu atakuwa pekee, atabeba madhambi yake na atahisabiwa pekee bila ya kunasibishwa na waliomhusu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

 

 

 

((إِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ فَلَا أَنسَابَ بَيْنَهُمْ يَوْمَئِذٍ وَلَا يَتَسَاءلُونَ)) ((فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ)) (( وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُوْلَئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ))

 

((Basi litapopulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana))  

 

((Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa))

 

((Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio waliozitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu)) [Al-Muuminuun: 101-103 ]

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share