Anamrusha Roho Katika Harusi, Anataka Ugomvi Naye, Vipi Azuie Shari Zake?

 

Anamrusha Roho Katika Harusi, Anataka Ugomvi Naye, Vipi Azuie Shari Zake?

 

Alhidaaya.com

 

Swali:

 

Kuna mtu anatafuta ugonvi na mimi, sikijui ni nimemkosea, tukiwa maharusini anajaribu kunirusha roho na taarab, na mimi sio mtu wa kugombana. Je nifanye nini? Au kuna dua yoyote ambayo naweza kusoma nikajiepusha nae kwa sababu ni mshari sana.

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho. 

 

Kulingana na swali lako inaonekana mkosa ni wewe kwani unajipeleka mahali ambapo hufai kuwepo kishari’ah. Tufahamu kuwa sherehe zozote ambazo zinakuwa na muziki au kurusha roho hazifai kuhudhuriwa na Waislamu.

 

Allaah Aliyetukuka Anasema:

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴿٦﴾

Na miongoni mwa watu, yuko ambaye hununua maneno ya upuuzi ili apoteze (watu) njia ya Allaah bila elimu, na huichukulia mzaha. Hao watapata adhabu ya kudhalilisha. [Luqmaan: 6].

 

Swahaba ‘Abdallaah bin Mas‘uud (Radhwiya Allaahu ‘anhu) aliapa mara tatu kwa kuielezea Aayah kuwa maneno ya upuuzi yanamaanisha muziki.

 

Suluhisho kwa tatizo lako ni kuwa ujiepushe kwenda maharusini na kurusha roho na utaepukana na ugomvi wa huyo na mwengineo yeyote na pia utabakia katika taqwa, utalinda heshima yako na utatulia roho yako

 

Tafadhali bonyeza viungo vfutavyo upate maelezo zaidi:

 

Hukmu Ya Muziki Katika Qur-aan Na Sunnah - Ewe Upendaye Nyimbo Na Muziki,

 

Haujafika Wakati Wa Kuogopa Adhabu Kali Za Allaah?

 

Muziki, Ngoma, Haramu

 

Tambua Kwamba Muziki Ni Haramu

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share