Ana Tabia Za Za Kutazama Wanawake Na Picha Chafu Anashindwa Kujizuia Nazo- Afanyeje?
SWALI:
Nina tabia tatu Nimeshindwa kujizuia. Kuwatazama wanawake kwa matamanio. Kutazama picha zao kwenye t.v. Na kuwachezea. Yaani vitendo kabla ya jimai. Lakini si waingilii. Kila siku namuomba Mola anitowe katika makosa haya nashukuru amenipa nguvu za kujizuia kuwaingilia lakini hayo matatu nimeshindwa na sababu kubwa ni kuwa yanapatikana kwa urahisi. Nifanye nini.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani kwa swali lako kuhusu kushindwa kuacha baadhi ya tabia ambazo ni mbaya Kiislamu.
Awali ya yote ni kuwa mwanaadamu anaposema juu ya jambo lolote kuwa ameshindwa basi atashindwa kwa kuwa ashajiwekea udhaifu kuwa hawezi. Linalotakiwa ni kuwa na moyo thabiti na bila shaka Allaah Aliyetukuka Atakusaidia.
Allaah Aliyetukuka Anasema:
“Hakika Allaah Habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo nafsini mwao” (ar-Ra’d 13: 11).
Ikiwa unaweza kuchezecheza na wanawake bila ya kuzini nao ni kuwa wewe una uwezo wa kujizuia na hata
Kisha linalotakiwa ni uwe mbali na vishawishi vyovyote ambavyo vinaweza kukuweka karibu na zinaa. Allaah Aliyetukuka Ametumia neno kali lenye uzito wa kumfanya mtu ajiepushe na uzinzi huo pale Aliposema:
“Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya” (al-Israa’ 17: 32).
Na kila wakati unapotaka kufanya kosa usitazame kosa lakini angalia unayemkosea. Wewe unamkosea Allaah Aliyetukuka, je, utamjibu nini utakaposimama mbele Yake Siku ya Qiyaamah siku ambayo hakutakuwa na mkalimani baina yako na Allaah Aliyetukuka.
Pia inaonyesha una wakati mwingi wa kupoteza, jaribu
Chukua wakati mwingi katika kusoma Qur-aan, jua maana yake, zingatia yaliyo ndani, fanya juhudi kuyatekeleza hayo. Bila shaka ukifanya hayo utajikuta unakuwa karibu na Allaah Aliyetukuka na hivyo kujiepusha na mengi maovu.
Jikurubishe katika kufanya ‘Ibaadah na huku unamuomba Allaah Aliyetukuka kwa dhati Akuepushie matatizo hayo ya kujiingiza katika madhambi hayo makubwa. Na pia ulimi wako uwe na rutuba ya kumtaja Allaah Aliyetukuka kila wakati.
Tafadhali bonyeza viungo vifuatavyo upate maelezo na manufaa zaidi:
Anapenda Kuangalia Machafu Kisha Anatubu, Kisha Anarudia Tena, Naye Anachukiwa Jambo Hili
Nataka Kutubu Lakini Shaytwaan Kanivaa Nifanye Nini?
Tunakuombea tawfiki katika kufanikisha kujiondoa katika hayo madhambi.
Na Allaah Anajua zaidi
