Adkhaar Za Swalah Je, Inafaa Zisomwe Pia Katika Swalah Za Sunnah?

 

 

 

SWALI:

 

Assalaam alaykum Warahmatullah Wabarakatuh baada ya maamkizi hayo mema shukran zangu ziende kwa Mola wetu aliyetuumba Subhaana Wataala na pia alhidaaya. Sheikh nina maswali mengi kuhusu swala itakuwa vizuri kama utapata muda kunielimisha.

 

Baada ya swala ya fardhi kuna adhkaar ambazo Mtume wetu SWALA LLAH ALAYHI WASALLAM ametufundisha tuzisome JE swala za sunna nisome adhkaar zipi


 

JIBU:

 

 

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kusoma Adhkaar baada ya Swalah za Sunnah.

Hatujapata katika Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa alikuwa analeta Adhkaar kama zile za baada ya Swalah ya Faradhi kwenye Swalah za Sunnah.

 

Ile tuliyopata ni du’aa aliyokuwa akileta baada ya Swalah ya Sunnah kabla ya Alfajiri. Hii ni kutokana na mapokezi ya Ibn as-Sunniy kuwa ‘Aamir bin Usaamah kutoka kwa baba yake kuwa aliswali rakaa mbili za Alfajiri na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) yuko karibu naye aliswali rakaa mbili nyepesi kisha akamsikia anasema naye amekaa: “Allaahumma Rabba Jibriyl wa Israafiyl wa Miyka’iyl wa Muhammad an-Nabiyy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam), A‘udhu bika minan Naar”. Alikariri mara tatu.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share