Aliyefariki Ameacha Kaka, Dada Na Mjukuu

SWALI:

Aliyefariki amewachja kaka mmoja wa mama mmoja, kaka mmoja wa baba mmoja, madada wawili wa mama mmoja na mjukuu kwa mtoto wake wa kiume {aliyefariki kabla}. Ahsante.

 


 

JIBU: 

AlhamduliLlaah - Himdi Na Sifa Zote Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Hakika swali hili haliko moja kwa moja kwani kuna mengi ambayo hayakuelezwa lakini ikiwa muulizaji ana hakika hao ndio warithi au jamaa wa karibu kabisa kwa aliyefariki basi watarithi kama ifuatavyo:

1)     Mjukuu akiwa ni wa kiume atapata wirathi wote na hao wengine, kaka wa kwa mama, madada wa kwa mama na kaka wa kwa baba hawatapa chochote.

  2)    Ikiwa mjukuu ni msichana basi atapata nusu (1/2) ya wirathi, kaka wa kwa mama na madada wa kwa mama hawatapata chochote na kilichobaki yaani nusu (1/2) atapewa kaka wa kwa baba.

Lau huyu aliyefariki alikuwa na mzazi au wazazi walio hai na pia alikuwa na mke au mume mgawo wa wirathi utabadilika. 

 

Tanbihi kwa wenye kuuliza Maswali ya Mirathi:

 

Ili maswali yenu yajibike haraka inatakiwa kuwa wale watu wote ambao wana ukaribu wa kidamu wa aliyefariki wawe ni wenye kuandikwa ili iwe hapana utata wowote. Na katika hayo tungependa watu wafuatao watiliwe maanani sana:

1.                 Kijana mwanamume.

2.                 Kijana mwanaume wa kijana mwanaume (mjukuu).

3.                 Baba.

4.                 Babu wa kwa baba.

5.                 Ndugu mume wa kwa baba na mama (khalisa).

6.                 Ndugu wa kwa baba.

7.                 Ndugu mume wa kwa mama.

8.                 Kijana mwanaume wa ndugu mume khalisa.

9.                 Kijana mwanaume wa ndugu mume wa kwa baba.

10.             Ami wa kwa baba na mama.

11.             Ami wa kwa baba.

12.             Kijana mwanaume wa ami wa kwa baba na mama.

13.             Kijana mwanaume wa ami wa kwa baba.

14.             Mume.

15.             Binti.

16.             Binti wa kijana mwanaume.

17.             Mama.

18.             Dada khalisa.

19.             Dada wa kwa baba.

20.             Dada wa kwa mama.

21.             Bibi mzaa baba.

22.             Bibi mzaa mama.

23.             Mke.

Hii itatusaidia sana katika kujibu maswali yenu ya mirathi. Shukran.

 

 Na Allaah Anajua zaidi.

 

 

 


Share