Muislamu Anayejiua Nini Hukmu Yake

Hukmu Ya Muislamu Anayejiua

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Nini hukumu ya Muislamu kujiua au kujinyonga?

 

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

 

Uislamu umetukataza kujiua na yeyote mwenye kujiua atakuwa ametenda madhambi makubwa na yatakayomsababishia kuingia motoni na kuharamishiwa Jannah (Pepo).

 

Isitoshe, ataadhibiwa kwa chombo kilekile alichotumia kujiulia. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  Atuepushe kabisa na balaa hilo la kujinyonga au kujiua kwa njia yoyote ile.

 

Anasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka katika Hadiyth iliyosimuliwa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)

 

((مَنْ تَرَدَّى مِنْ جَبَلٍ فَقَتَلَ نَفْسَهُ، فَهْوَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ، يَتَرَدَّى فِيهِ خَالِدًا مُخَلَّدًا فِيهَا أَبَدًا، وَمَنْ تَحَسَّى سَمًّا فَقَتَلَ نَفْسَهُ، فَسَمُّهُ فِي يَدِهِ، يَتَحَسَّاهُ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدًا مُخَلَّدًا فِيهَا أَبَدًا، وَمَنْ قَتَلَ نَفْسَهُ بِحَدِيدَةٍ، فَحَدِيدَتُهُ فِي يَدِهِ، يَجَأُ بِهَا فِي بَطْنِهِ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدًا مُخَلَّدًا فِيهَا أَبَدًا)) البخاري ومسلم

 ((Yeyote atakayejitupa kutoka mlimani na kujiua, atatupwa ndani ya moto milele. Atakayekunywa sumu na kujiua, basi atatupwa motoni na huko atakuwa akiinywa hiyo sumu milele. Atakayejiua kwa kipande cha chuma, atatiwa motoni akiwa na kipande hicho cha chuma akijitwanga nacho tumboni kwake humo motoni milele))].  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Kadhaalika, mtu anayejiua, au jambazi, au aliyefariki kwa kutumia madawa ya kulevya au kuuza, mlevi n.k. wote hao watatengwa kuswaliwa na Viongozi wa Dini ili iwe funzo kwa wale wenye tabia hizo waweze kujiepusha na maovu hayo. Lakini, hata hivyo, wanaweza kuswaliwa na watu wa kawaida.

 

Ingia katika kiungo kifuatacho upate majibu zaidi:

 

Nini Hukmu Ya Kujiua Kwa Sababu Ya Mateso Na Tabu Za Dunia

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share