Tanabahi! Kwa Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) Nyoyo Hutulia!

 

Tanabahi! Kwa Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) Nyoyo Hutulia!

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Anasema Allaah (‘Azza wa Jalla):

 

  الَّذِينَ آمَنُوا وَتَطْمَئِنُّ قُلُوبُهُم بِذِكْرِ اللَّـهِ ۗ أَلَا بِذِكْرِ اللَّـهِ تَطْمَئِنُّ الْقُلُوبُ ﴿٢٨﴾

Wale walioamini na zikatua nyoyo zao kwa kumdhukuru Allaah. Tanabahi!  Kwa kumdhukuru Allaah nyoyo hutulia!  [Ar-Ra'ad 13: 28]

 

 

Fadhila za kumdhukuru Allaah (‘Azza wa Jalla)    ni nyingi mno; zimetajwa    katika Qur-aan na Sunnah, mojawapo ni utulivu wa moyo kama ilivyo katika Aayah hiyo tukufu.

 

Vile vile Hadiyth kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash'ariyy  (Radhwiya Allaahu 'anhu)  kwamba  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

  ((مَثَـــلُ الـــذي يَـــذكُرُ ربَّـــهُ وَالـــذي لا يـــذكُرُهُ ، مَثَـــل الحـــيِّ والمَيِّــتِ))

 ((Mfano wa anayemdhukuru  Rabb wake na asiyemdhukuru ni mfano wa alie hai na maiti)) [Al-Bukhaariy  pamoja Al-Fat-h (11/208) na Muslim kwa tamshi kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:  

 

((مَثَلُ البَيْتِ الذي يُذكَرُ اللهُ فيه، والبيت الذي لا يذكرُ الله فيه مَثَلُ الحيِّ والميِّت))

((Mfano wa nyumba ambayo Allaah Anatajwa na ambayo hatajwi humo ni kama aliyehai na maiti)) (1-539)

 

 

Na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:

  

 فَاذْكُرُ‌ونِي أَذْكُرْ‌كُمْ وَاشْكُرُ‌وا لِي وَلَا تَكْفُرُ‌ونِ ﴿١٥٢

((Basi nidhukuruni na Mimi Nitakukumbukeni; na nishukuruni wala msinikufuru.))  [Al-Baqarah:152]

 

 

 

Na pia Ametuamrisha tumdhukuru kwa wingi:

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُ‌وا اللَّـهَ ذِكْرً‌ا كَثِيرً‌ا ﴿٤١﴾ وَسَبِّحُوهُ بُكْرَ‌ةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

 

((Enyi mlioamini!  Mdhukuruni Allaah kwa dhikri ya wingi. Na Msabbihini asubuhi na jioni))    [Al-Ahzaab: 41-42]

 

Na Anasema:

   وَالذَّاكِرِ‌ينَ اللَّـهَ كَثِيرً‌ا وَالذَّاكِرَ‌اتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَ‌ةً وَأَجْرً‌ا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

((na Wanaume wanaomdhukuru Allaah kwa wingi na Wanawake wanaomdhukuru Allaah (kwa wingi); Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu)) [Al-Ahzaab 35]

 

  

Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni katika ’amali bora kabisa kama ilivyo katika Hadiyth ifuatayo:

 

 ((أَلَا أُنَبِّئُكُمْ بِخَيْرِ أَعْمَالِكُمْ وَأَزْكَاهَا عِنْدَ مَلِيكِكُمْ وَأَرْفَعِهَا فِي دَرَجَاتِكُمْ وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ إِنْفَاقِ الذَّهَبِ وَالْوَرِقِ وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ أَنْ تَلْقَوْا عَدُوَّكُمْ فَتَضْرِبُوا أَعْنَاقَهُمْ وَيَضْرِبُوا أَعْنَاقَكُمْ؟)) قَالُوا: بَلَى. قَالَ: ((ذِكْرُ اللَّهِ تَعَالَى))

 ((Hivi niwaambieni habari ya matendo yenu bora, na ambayo ni masafi mno, mbele ya Rabb wenu, na ambayo ni yajuu mno katika daraja zenu, na ambayo ni bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na fedha, na ambayo ni bora kuliko kukutana na adui zenu, mkawapiga shingo zao, nao wakakupigeni shingo zenu?))  Wakasema: [masahaba]: Ndio. Akasema: ((Ni kumdhukuru Allaah Ta’aalaa))    [Hadiyth ya ‘Abu Dardaa ‘Uwaymir bin ‘Aamir (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/459), ibn Maajah (2/1245), na angalia: Swahiyh ibn Maajah (2/316) na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/193]

 

 

Baadhi ya dhikru-Allaah katika Hadiyth:

 

 

 

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayesema:

 

سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ

 Subhaana Allaahi Wa Bihamdihi 

[Ametakasika Allaah na Himdi Anastahiki Yeye] kwa siku mara mia, atafutiwa madhambi yake hata kama yalikuwa mfano wa povu la bahari)) [Al-Bukhaariy na Muslim]  

 

Na amesema pia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  ((Kusema kwangu:

 

 سُبْحَانَ اللهِ، والحَمْدُ للهِ،  وَ لاَ إِلَهَ إلاَّ اللهُ واللهُ أَكْبر  

 

Subhaana Allah Wal-HamduliLLah, Wa La Ilaaha Illa Allaah, Wa Allaahu Akbar [Ametakasika Allaah na Himdi Anastahiki Allaah na hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah na Allaah ni Mkubwa] ni bora kwangu kuliko kila kilichoangaziwa na jua))  [Muslim]

 

 

Na amesema pia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

 

 ((Atakayesema:

لا إِلهَ إِلَّا اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْد، وهُوَ عَلى كُلِّ شَيءٍ قَديرٌ

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah  peke Yake, hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza

-

… mara kumi, ni kama (thawabu za mtu) aliyewacha huru nafsi nne katika wana wa Ismaa’iyl))  [Hadiyth ya Abu Ayyuwb Al-Answaariyy (رضي الله عنه) -  Al-Bukhaariy (7/67), Muslim (4/2071) kwa tamshi yake na angalia fadhila zake  nyingine: “Atakayesema mara mia kwa siku, mara kumi, mara moja”  katika ‘Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni’ Du’aa  [92, 93]   

 

 

Na amesema pia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  ((Hivi anashindwa mmoja wenu kuchuma kila siku thawabu elfu?)). Mtu mmoja miongoni mwa waliokaa akamuuliza “Atachuma vipi mmoja wetu thawabu elfu?  Akamjibu ((Aseme:

 

سُبْحَانَ اللهِ

Subhaana Allaah  

 

[Ametakasika Allaah] mara mia moja, basi ataandikiwa thawabu elfu moja,  au atafutiwa madhambi elfu moja)) [Muslim]

 

 

 

Share