Aayah Ambazo Hukmu Yake Imefutwa Ni Zipi?

 

Aayah Ambazo Hukmu Yake Imefutwa Ni Zipi?

 

 Alhidaaya.com

 

 

 

 

Swali:

 

Asalaam alaykum.

 

Naomba kuorodhoshewa Aayah  zilizofutwa katika Quran (hazifanyi kazi kwa kushuka aya nyingine). Kwa upande wangu hili limekuwa tatizo kubwa sana hasa kutokana na nchi nnayoishi ni ngumu kupata watu wenye ilmu hii. Najua kuwa ni kazi kubwa kuorodhesha Aayah zote hizo lakini nakuombeni hata mungeandika makala inayohusiana na hilo.

 

Jazaka-A llahu khair.

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Kwa kifupi tunakutajia Aayah zifuatazo na kisha tunakuwekea kiungo chenye kuorodhesha An-Naasikh Wal-Mansuwkh (Kinachofuta Na Kinachofutwa) na maelezo kuhusu somo hili tukitaraji itatoa mwanga kuhusu maudhui hii.

 

 

1.     Kubatilishwa hukmu ya Aayah zifuatazo Suwrah Al-Baqarah [2]: 219 na Suwrah An-Nisaa’ [4]: 43 kwa ile Aayah ya Suwrah Al- Maa’idah [5]: 90 – 91.

 

 

2.     Kubatilishwa hukmu ya Aayah zifuatazo Suwrah Ruwm [30]: 39, Suwrah An-Nisaa’ [4]: 161 kwa zile Aayah za Suwrah Al-Baqarah [2]: 275 – 280.

 

 

An-Naasikh Wal-Mansuwkh (Kinachofuta Na Kinachofutwa): النَّاسِخُ وَالْمَنْسوخ

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share