Ndugu Aliyezaliwa Naye Matumbo Tofauti Hamjali Mama Yake; Amnasihi Vipi?

 

Ndugu Aliyezaliwa Naye Matumbo Tofauti Hamjali Mama Yake; Amnasihi Vipi?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Asalaam Alaikum! 

 

Maswali kuhusu Kaka yangu mie na Kaka yangu tomezaliwa Mama tofauti, Mama yake aliwachika yeye akiwa na Umri wa miaka 2, Mama yangu alipoolewa na Baba yangu akachukuliwa kulelewa ana Umri wa Miaka 3, alilelewa Tuliishi vizuri mpaka alipofika Miaka 15 akaenda kuishi kwa Bibi yake Sababu Secondary sio mbali na hapo alipofika 20 mie na Kaka yangu tukaenda Kusoma UK, Kaka yangu Allaah akamjalia kuowa nikaamuwak utoka kwenye nyumba Baadae Mama yangu mzazi akaja kukaa na mie, Toka Mama yangu amekuja tulikuwa tunaenda Kwakwe ila yeye Haji kwangu namuuliza anasema Kazi nyingi hampigii kumjulia Mama yangu hali mie kwao Nampigia Mama yake na Bibi yake nikienda nawatembelea, hajawahi kumleta Mkewe kwa Mama nasikia wanakuja wanaishia kwa Aunty yake mkewe basi. Mama yangu anajisikia Vibaya kwa nini anafanya hivyo. Je Azabu yake ni nini mie nimsaidie haraka.

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

 

Mas-ala haya ambayo umeyaelezea ni vigumu sana kuweza kuamua bila kusikia na upande wa pili, wa nduguyo.

 

Kwa kila hali jazaa ya ihsani haiwi ila ihsani kama alivyosema Aliyetukuka:

 

هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ ﴿٦٠﴾

Je, kuna jazaa ya ihsani isipokuwa ihsani tu?  [Ar-Rahmaan: 60].

 

 

Hata hivyo, mara nyingine au nyingi watu hawafanyi ihsani kama walivyofanyiwa. Na kufanya hivyo ni dhulma mbele ya Allaah Aliyetukuka. Na mwenye kudhulumu anakuwa katika kiza siku ya Qiyaamah.

 

 

Linalotakiwa kufanywa ni:

 

1.   Wewe ukabiliane na nduguyo, mkae pamoja wakati unaouona yuko katika hali nzuri ili uzungumze naye kuhusu hilo kwa uwazi kabisa. Na wakati huo kila kitu kitabainika kwa dhahiri.

 

2.    Ikiwa wewe hukuweza kupata ufumbuzi jaribu kutumia marafiki zake wa karibu ili waweze kutatua tatizo hilo.

 

3.   Ikiwa imeshindikana basi jaribu kwenda kwa Imaam wa Msikiti mnaoswali au wa karibu nanyi, au naye, kwa Shaykh au wapenda kheri wenye busara ili muweze kutatuliwa tatizo lenu.

 

 

Ikiwa yote yameshindikana basi itabidi uachilie hapo wala usikate undugu kwani kwa wema unaomfanyia huenda akakumbuka na kurudi nyuma kwa kuomba msamaha kwa mama yako. Pia usikate uhusiano na jamaa zake, kama mama yake na bibi yake kwa ajili hiyo kwani Allaah Aliyetukuka Anasema:

 

وَلَا تَسْتَوِي الْحَسَنَةُ وَلَا السَّيِّئَةُ ۚ ادْفَعْ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ فَإِذَا الَّذِي بَيْنَكَ وَبَيْنَهُ عَدَاوَةٌ كَأَنَّهُ وَلِيٌّ حَمِيمٌ﴿٣٤﴾وَمَا يُلَقَّاهَا إِلَّا الَّذِينَ صَبَرُوا وَمَا يُلَقَّاهَا إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ﴿٣٥﴾

Na wala haulingani sawa wema na uovu. Lipiza (uovu) kwa ambalo ni zuri zaidi; tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui, atakuwa kama ni rafiki mwandani. Na hapewi hayo isipokuwa wale waliovuta subira, na hapewi hayo isipokuwa mwenye fungu adhimu. [Fusw-swilat: 34 – 35].

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share