Sindano ya Ganzi na Kung'oa Jino Inavunja Swawm?
SWALI:
Assalam alykum
Naomba mnifahamishe kuhusu shindnao ya gazi.
Ikiwa mtu kapigwa shindano ya gazi anapotolewa jino, na alikua kafunga sasa aendelee na kufunga au itambidi alipe funga yake
Assalam Alyku.
JIBU:
Sifa zote njema anastahiki Allah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Jibu ni kwamba unapoomuwa na jino na inapobidi ungo'lewe basi huna budi kufanya hivyo ili usitaabike zaidi na maumivu. Na kupiga sindano ya ganzi haina tatizo na Swam yako. Kwa hiyo unaweza kupiga sindano ya ganzi na kutolewa jino na Swam yako itaendelea kukubaliwa. Tahadhari tu usimeze mate kwa wingi, au damu au dawa ya kusukutuwa ikasababisha kuharibu Swawm yako.
Tunakuombea shifaaun ya haraka.
Na Allah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


