Chapati Kavu Za Hamira

Chapati  Kavu Za Hamira

Vipimo

         

Unga - 6 gilasi

 

Maziwa ya unga - 2 vijiko vya supu

 

Hamira - 2 vijiko vya chai

 

Mafuta

                                                         

Chumvi - kiasi

  

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

 

  1. Weka vitu vyote katika bakuli kisha changanya na kanda kwa maji hadi uwe laini kama unga wa chapati.
  2. Fanya madonge madogodogo.
  3. Uache uumuke.
  4. Sukuma kama chapati, kisha choma kwenye mkaa kwa kuweka wavu juu ya makaa au katika chuma (frying pan).
  5. Geuza pande zote mbili kuwivisha. 
Share