Kusikiliza Qur-aan Huku Unafanya Kazi Zako
SWALI
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Hii haina shaka kwani kusikiliza huko kwa makini ndiko kumesisitizwa zaidi. Na linalochukiza kwa baadhi ya Maulamaa ni kuzungumza na huku Qur'an inasomwa kwa ushahidi wa aya hii:
}}وَإِذَا قُرِىءَ الْقُرْآنُ فَاسْتَمِعُواْ لَهُ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ{{
{{Na isomwapo Qur'aan isikilizeni na nyamazeni ili mpate kurehemewa}} Al-A'araaf:204
Hata hivyo pamoja na baadhi ya wanachuoni kusema kuwa aya hiyo makusudio ni popote, ila wanachuoni wengi na wafasiri kama Ibn Kathiyr katika tafsiri yake kasema: "Maana yake ni ukiwa ndani ya Swala ya Jamaa'ah, pindi Imamu anaposoma kwa sauti (swala za Alfajiri, Maghrib na 'Ishaa') kama ilivyopokewa na ((Imaam Muslim kwenye Sahiyh yake kutoka katika hadithi ya Abu Musa Al-Ash'ariy aliyesema: Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa Sallam) amesema:"Imaam amewekwa ili afuatwe, kwa hivyo akisema: "Allaahu Akbar nanyi mfuateni kwa kusema kama yeye na akianza kusoma, nyinyi nyamazeni))
Vile vile akasema tena Ibn Kathiyr: ((Ibraahiym Ibn Muslim Al-Haajriy amepokea kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu)aliyesema: Wao (maswahaba) walikuwa wakizungumza na hali ya kuwa wamo ndani ya swala, kwa hivyo ilipoteremshwa aya hii ... waliamrishwa wawe kimya))
Naye Imam At Twabariy kwenye tafsiri yake anasema kwamba ((Ibn Mas'uud amesema: Tulikuwa tukipeana salamu miongoni mwetu tukiwa ndani ya swala, kisha ikaja katika Qur'an: Na isomwapo Qur'aan isikilizeni na nyamazeni))
Kwa hoja hizo inaonyesha aya hiyo haihusiani na Qu'ran isomwayo maredioni na kwenye matelevisheni makompyuta au na watu nje ya swala, hata hivyo kwa kuyapa heshima maneno ya Mwenyeezi Mungu ni bora kunyamaza isomwapo au kuizima
Nasiha Ya Kufuata Adabu Za Tilawa (Kusoma) Qur'aan
Kwa hali yeyote ilivyo, ni bora kuipa heshima Qur'aan kwa kutimiza adabu za kusoma Quraan kwani ni maneno ya Allaah سبحانه وتعالى na kuyatukuza ni wajibu: Nazo ni:
1) Kupiga mswaki
2) Kuwa na wudhuu
3) Kujifunika vizuri (mwanamke)
4) Kuelekea kibla
5) Kusoma kwa kutafakari
6) Kusoma kwa Tajwiid na kufuata sheria zake.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha



ISALAMAALEKU MIMI
ISALAMAALEKU MIMI RAMADHAN HASSAN ,BIN THABIT FROM K ,JONGOO, NDUGU WA ALHIDAAYA , NILI KUWA NAPENDA KUU LIZA SUWALI ,HILI SUWALI LINA HUSI YANA KWA WALE WENYE WAKE ZAO, SUWALI JE MWANA MKENA MWANA MME AU MTUNA MKEWE, ENDOPO MMOJA WAPO AMETIYA UDHUU,UDUU MKIGUSANA , UDHU UNA TOKA, MGUSANO ,WA NGOZI KWA NGOZI ,NAFIKIRI NIME FAHAMIKA ,SHUKURAN,
RT ,TORONO